Ukishakuwa Na Fedha Utakutana Na Hiki Hapa

Rafiki yangu nikupendaye, Huu ni msimu wa sikukuu. Na watu wengi tunaongozwa na hisia ya kufanya manunuzi kwa kipindi hiki. Fedha ikiwepo, huwa haikosi matumizi. Kila mmoja anaingia kwenye mtego wa manunuzi. Huwa tunanunua vitu na baadaye tunakuja kujilaumu. Kitu kikubwa unachotakiwa kuzingatia kwa kipindi hiki ni umakini tu. Unajua kwa nini? Kwa sababu, ukishakuwa …

Acha Watu Wakuzidi Maeneo Yote Lakini Siyo Kwenye Hili

Rafiki yangu nikupendaye, Asiwepo mtu yeyote ambaye anafanya kazi kukuzidi wewe. Hakikisha unafanya kazi kuliko wengine wote, weka juhudi kubwa kwenye kazi zako, iwe ni kwenye ajira, kujiajiri au biashara. Hakikisha watu wanapotaka kitu fulani kikamilike basi wanakuja kwako. Na hili linawezekana kama utaweka muda na umakini kwenye kila unachofanya, na kama utaacha kutafuta njia …

Ijue Kanuni Ya Mafanikio Makubwa

Rafiki yangu nikupendaye, Kanuni ya mafanikio makubwa inasema hivi, ushawishi wako ni matokeo ya jinsi gani unaweka mbele maslahi ya wengine kabla ya maslahi yako. Hii ni kanuni inayohusu mtandao wako, wale watu wanaojua kuhusu wewe, wanaokuamini na ambao wanapenda kukuona wewe unafanikiwa. Hawa ni watu ambao watakutetea kwa lolote na kwa yeyote. Kadiri unavyokuwa …

Ung’ang’anizi Unaleta Bahati

Rafiki, Unaweza kusema watu wana bahati na wewe labda una kisirani, lakini bahati au kuwa na kisirani ni chaguo lako mwenyewe. Ukikaa kwenye, bahati inakuja yenyewe. Hata kama mchakato haujakulipa leo, utakuja kukulipa kesho. Ung'ang'anizi wa kukomaa kwenye mchakato, huwa unaleta bahati. Bahati ni pale fursa inapokutana na maandalizi.Endelea kukaa kwenye mchakato, utashangaa siku isiyokuwa …

Shirikiana Na Watu Muhimu Kufikia Ndoto Zako./20/12/2024

Rafiki, Watu ambao hawajafanikiwa huwa wanafikiri wanapaswa kufanya kila kitu wao wenyewe ili wafanikiwe. Hivyo wanapokuwa wamekwama kwa kukosa ujuzi au uzoefu fulani huona ndiyo mwisho wa safari yao ya mafanikio. Usikubali ukosefu wa ujuzi au rasilimali kukuzuia wewe kufikia ndoto zako. Kama kuna kitu hujui, au kuna kitu huna tafuta mtu kwenye kujua au …

Njia Bora Za Kukuletea Matokeo

Rafiki, Ujinga ni kufanya kitu kile kile, kwa mtindo ule ule, huku ukitegemea kupata matokeo ya tofauti. Kama umepanda mahindi, tegemea kuvuna mahindi na siyo vinginevyo.Kwenye maisha, matokeo unayopata sasa ni juhudi ambazo umeweka. Hatua muhimu unayopaswa kuichukua na kukufanya kuwa bora kila siku ni kujifunza kila siku. Jifunze kupitia mafunzo mbalimbali yaliyoandaliwa kuhusu kila …

Misingi Mitatu Ya Kuishi Kila Siku

Rafiki yangu nikupendaye, Chochote kile ambacho hakina msingi ni rahisi kuanguka.Kwenye maisha yako, unapaswa kuwa na misingi ambayo inakuongoza. Kama huna misingi, basi ishi misingi hii hapa ; Nidhamu; kuwa na nidhamu kwako wewe binafsi, kwa kufanya yale uliyopanga kufanya, kuwa na nidhamu ya muda kwa kutokupoteza muda wako kwa mambo yasiyo sahihi. Kuwa na …

Jinsi Ya Kupata Ushindi Wa Siku

Rafiki, Kila mmoja wetu anahitaji ushindi fulani kwenye maisha yake.Ushindi huwa unaleta raha fulani kwenye maisha. Na ushindi hauji bila maandalizi.Na maandalizi yanaanza na mchakato fulani. Ukitaka ushindi, jenga tabia ya kupata ushindi huo. Kwa mfano, ushindi wa siku unapaswa kuanza na kuwa na orodha ya majukumu ya kufanya. Kama huna orodha ya majukumu, ni …

Shida Anayetafsiri

Rafiki, Mtu anayeongea anapaswa kuwa makini na kila neno analotoa kinywani mwake, kwa sababu unapoongea, ni kama unarusha jiwe gizani na hujui nani litampata. Yale unayoongea yanaweza kuwa ya kawaida tu, lakini shida inakuja kwa yule anayetafsiri neno.Atalitafsiri neno kwa namna anavyooelewa yeye.Huwezi kumpangia mtu cha kutafsiri juu ya kile ulichoongea. Unapoongea na kadamnasi pendelea …

Design a site like this with WordPress.com
Get started