Ukiwa Mstaarabu Kwenye Maisha Hutoboi

Rafiki yangu nikupendaye, Kwenye maisha ukiwa mstaarabu sana hutoboi kwa sababu ustaarabu utakuzuia kufanya vitu vingi na hata kuona aibu fulani. Kwa mfano, wewe kama muuzaji, utajiona mstaarabu kumwambia mteja anunue kile unachouza. Una mdai mtu, unaogopa kumwambia akulipe, hivyo unakuwa mstaarabu na kukaa kimya. Kuna watu ambao wanapaswa wakamilishe kitu fulani ili uweze kukamilisha …

Kabla Hujaenda Kasi Hakikisha Hiki Kwanza

Rafiki yangu nikupendaye, Kila mtu anapenda kwenda mbele. Ni lengo la kila mmoja wetu. Hakuna mtu anayeamka na kusema leo ninataka kurudi nyuma. Kwenye maisha yako, kama unataka kujua kama unaenda mbele au unarudi nyuma ni kwa kujifanyia tathmini. Ukitaka kujua unaenda mbele, ni pale unapokuwa haurudi nyuma. Kabla hujafanya maamuzi ya kwenda kasi, kwanza …

Kuwa Mtu Wa Namna Hii Mwaka 2025

Rafiki yangu nikupendaye, Mungu aliumba dunia na vitu vyote vinavyoonekana na visivyoonekana kwa kutamka.Vivyo hivyo, mwaka huu mpya unaoanza leo, ukawe mwaka wa kujitamkia matashi mema. Jitamkie heri haijalishi Utakutana na magumu gani mbeleni, lakini jitamkie mazuri, hakuna njia isiyokuwa na kona. Kazi yako kubwa ni kubariki watu katika siku hii ya leo.Anza kujibariki wewe …

Hukosi Kitu Cha Kushukuru

Rafiki yangu nikupendaye, Kama uko hai mpaka siku ya leo, ni zawadi nzuri ya kushukuru Mungu. Kama hata mipango yako haijaenda vile ulivyokuwa unataka, lakini hukosi Kitu cha kushukuru. Leo unapoumaliza mwaka 2024, fanya zoezi la kuandika mambo ya kushukuru kwenye maisha yako ndani ya mwaka huu. Mwaka 2024, umekuwa mwaka wa namna gani kwako.Yapi …

Kama Huna Hichi Kitu Usiongee Kabisa

Rafiki yangu nikupendaye, Mmoja wa mwanafalsa wa Ustoa anatushauri kwamba, kama watu wanakusema juu ya kitu fulani, kama ni kweli badilika. Na kama siyo kweli endelea na maisha yako. Naye baba wa falsafa Plato aliwahi kunukuliwa akisemaWerevu huongea kwa sababu wana kitu cha kuongea, ila wapumbavu huongea kwa sababu inabidi waseme kitu. Wakati wowote unapotaka …

Kama Siyo Sahihi Usifanye

Rafiki yangu nikupendaye, Njia nzuri kuishi falsafa au asili ni kuishi katika msingi ambao ninakwenda kukupendekezea hapa. Msingi huo ni, kama kitu siyo sahihi usifanye. Na kama kitu siyo kweli usiseme. Pale tu unapofanya kitu, jiulize tu je, hiki ninachofanya ni sahihi? Kama ni sahihi fanya na kama siyo sahihi usifanye. Kila mmoja wetu amepewa …

Ukifanya Kazi

Rafiki yangu nikupendaye , Ukifanya kazi, kazi yako itakusaidia kufanya kazi. Kazi nzuri huwa inajitangaza yenyewe bila kukutegemea wewe. Unapofanya kazi nzuri, inakuwa ni njia nzuri ya kujiuza kwa wengine. Acha kazi yako iwe msemaji wako. Kama unafanya kazi nzuri, utapunguza kujielezea na badala yake kazi yako itakuwa msemaji wako. Kazi yoyote ile inayopita mikononi …

Jaribu Kwanza

Rafiki yangu nikupendaye, Huwa tunatengeneza vikwazo mbalimbali kwenye maisha yetu, huku sisi wewe wenyewe tukiwa ndiyo vikwazo vyenyewe. Mara nyingi huwa tunahalalisha kitu kwa mdomo na siyo kwa vitendo.Tukiambiwa kitu, tunaishia KUHUKUMU tu kwamba hiki hakifanyi kazi au hakuna kitu. Njia nzuri ya kujua kama kitu kinafanya kazi au hakifanyi kazi ni kukifanyia kazi kitu …

Unapotafuta Furaha Zingatia Hili

Watu huwa wanaweka juhudi ili kutafuta furaha na hata wengine raha.Yote hii ni kutaka kujisikia vizuri.Kupata ile hali fulani ridhiko kutoka ndani. Katika kutafuta huko raha au furaha huwa tunazalisha homoni inayoitwa dopamine. Hii huwa inazalisha kilele cha raha fulani unayoitafuta. Rafiki, ni vizuri kutafuta furaha au raha lakini furaha au raha yako unayoitafuta, isiwaumize …

Asiwepo Mtu Akuzidi Hapa

Rafiki yangu nikupendaye, Kwenye haya maisha, asiwepo mtu ambaye anachukua hatua kuliko wewe. Mtu anayechukua hatua mara zote huwa anakuwa mshindi. Kama kuna mtu anachukua hatua kubwa kuliko unazochukua wewe, mtu huyo yupo mbele yako mbali sana, kwa sababu kwa hatua kubwa anazochukua, anajiweka kwenye nafasi ya kufanikiwa kuliko wewe. Hakikisha wewe unakuwa ndiye mtu …

Design a site like this with WordPress.com
Get started