Kila Gumu Unalopitia Kwenye Maisha Kuna Fursa Nzuri Ndani Yake

Huwa tunaona magumu kama balaa kwenye maisha yetu lakini siyo kweli Seneca Mwanafalsafa wa kistoa anasema, kila gumu unalopitia kwenye maisha kuna fursa ndani yake. Hakuna jambo ambalo linatokea bila kuwa na faida kabisa. Kumbe basi, wajibu wetu ni kujiuliza kwenye kila ugumu ni faida gani ipo ndani yake?Ni fursa zipi nzuri tunazoweza kuzitumia kwa …

Usifanye Jambo Ukiwa Na Kitu Hiki

Kila mmoja wetu anajua ni namna gani hasira zinavyoleta athari katika mahusiano yetu na wengine. Ili kuweza kuzuia hasira kwa namna fulani, basi usifanye jambo ukiwa na uchovu uliopitiliza wa mwili na akili. Kwa sababu, uchovu wa mwili na akili vinakufanya uwe rahisi kukasirika. Rafiki yangu nikupendaye, ni rahisi sana kukasirishwa na kitu pale unapokuwa …

Sababu iliyonifanya Niache Kuwasikiliza Watu

Sisi binadamu ni wazuri sana kwenye kuongea, na kama ingekuwa maneno ndiyo yanaleta mafanikio basi kila mtu angekuwa ameshafanikiwa kwenye kile anachopenda kwenye maisha yake.Kwa miaka mingi watu wamekuwa na ndoto mpaka wanaishia kuzeeka na kufa lakini hawajawahi kuzifanyia kazi. Watu wanaambiwa unatakiwa kuwekeza na anajua umuhimu lakini hafanyi ila kwenye kuongea ni mabigwa wazuri. …

Unachagua Kupoteza Kipi Kati Ya Hivi?

Matatizo mengi ya kifedha ambayo watu wengi wanayo yanasababishwa na tabia.Watu wanakopa kwa sababu ni tabia yao kukopa. Inapokuja kwenye swala la kukopesha, kuna vitu viwili unaweza kuvipoteza. Moja, unaweza kupoteza urafiki. Unapomkopesha mtu unaweza ukapoteza urafiki kwa sababu ya kukopesha. Kwa hiyo, kama unataka kupoteza urafiki kwa sababu ya Kiko fanya hivyo na kama …

Furaha Ya Kweli Inatoka Hapa

Shabaha ya kila mmoja wetu hapa duniani ni kuwa na furaha. Wengi tunajikuta tukifanya hiki au kile ili tupate furaha. Tunajiambia tukiwa na vitu fulani basi tutakua na furaha lakini kitu kama hicho hakiji kutokea kwenye maisha. Tumekuwa ni watu wa kukimbizana na vitu kuanzia mwanzo wa mwaka mpaka mwisho wa mwaka. Tumekuwa tunakimbizana na …

Kuna Sababu Mtu Kufanya au Kutokufanya Kitu

Kwenye maisha unapaswa kujua saikolojia ya watu. Usipojua saikolojia ya watu utapata shida, lakini utakapoijua wala hawatakusumbua. Watu wanafanya kitu au kutokufanya kitu kwa kuu mbili;Moja, hawajui. Ukiona mtu anashindwa kufanya kitu sababu ya kwanza huenda ikawa hajui. Kabla hujamlaumu na kumgombeza kaa chini muulize je, unajua unachopaswa kufanya? Wakati mwingine mpaka unaona mtu anafanya …

Kitu Muhimu Cha Kufanyia Kazi Kwenye Mauzo.

Kama tulivyojifunza kwenye kitabu cha CHUO CHA MAUZO, kwamba mauzo ndiyo moyo wa biashara. Na ushindi mkubwa kwenye mauzo ni pale mteja anapotengana na fedha zake. Mteja anapokuja kwenye kile unachouza, punguza chenga nyingi na hakikisha unafunga goli la haraka ili upate ushindi. Chenga hazina maana kama hujapata ushindi. Usiogope kuuza, pale unapogundua maumivu ya …

Njaa Inayowasumbua Watu Wengi

Watu wana njaa ya kusifiwa. Ni kawaida yetu sisi binadamu kupenda kusifiwa. Kila mtu anapenda kusifiwa, kama utaweza kuwasifia watu kwa kile wanachofanya au walichofanya utaweza kujenga ushawishi na kukubaliana nao.Kwa kila mtu unayekutana naye, tafuta kitu cha kumsifia. Maisha ni mauzo, hivyo wewe kama muuzaji unatakiwa kuwasifia wateja wako. Wasifie watu wako wa karibu, …

Njia Rahisi Ya Kupata Matokeo Ya Tofauti

Njia hiyo ni kufanya kitu cha tofauti. Wanasema, ujinga ni kufanya kitu kile kile halafu unategemea kupata matokeo ya tofauti. Ili upate matokeo ya tofauti kanuni ni moja tu, fanya kitu cha tofauti. Kwa mfano, hujawahi kujifanyia tathmini ya kujua kama unaenda mbele au la, fanya kitu cha tofauti kwa kujifanyia tathmini. Hujawahi kutabasamu, fanya …

Unafanya Nini Kwenye Biashara Yako?

Rafiki yangu nikupendaye, Uko kwenye biashara kwa lengo kutoa thamani kubwa kwa wengine kupitia kile unachofanya. Na uhai wa biashara yako ni MAUZO. Kwa sababu mauzo ndiyo yanayoleta fedha kwenye biashara na fedha ndiyo damu ya biashara bila fedha biashara haiwezi kwenda mbele. Chochote ambacho hakikui huwa kinakufa. Hivyo, kama kile unachofanya kwenye kazi au …

Design a site like this with WordPress.com
Get started