Ukifanyia Kazi Kitu Hiki Kamwe Huwezi Kubaki Kama Ulivyo.

Mpendwa rafiki, hongera sana kwa zawadi nzuri ya siku hii ya leo. Leo siku bora sana kwako hivyo ichukulie ni yako ya kipekee sana kwani ndiyo unauhakika nayo. Mpendwa rafiki, nakualika tuweze kusafiri pamoja katika makala yetu ya siku hii ya leo ili tuweze kujifunza wote kwa pamoja. Kumbuka rafiki kujiunga na mtandao wetu kwa …

Jinsi Ya Kujidharau Wewe Mwenyewe

Mpendwa rafiki, Huwa tunajiwekea utaratibu au ratiba ya kuifuata ndani ya siku husika. Pengine unakuwa na mambo ambayo umeyapanga kuyatekeleza lakini cha ajabu mambo unapanga mwenyewe lakini huyatekelezi. Unapokuwa unapanga kitu halafu unashindwa kukitekeleza bila sababu ya msingi huko ni kujidharau mwenyewe. Kama unashindwa kusimamia mambo yako unayopanga mwenyewe na kuyatekeleza utawezaje kusimamia ya wengine …

Thubutu Na Futa Nadharia Hii Kwenye Akili Yako

Tukisema tuanze kumtafuta adui mkubwa wa maisha yetu jibu la haraka ni sisi wewe wenyewe. Tumekuwa ni watu wa kujikwamisha kweli sisi wenyewe, watu wanakuwa na hamasa kweli lakini wakifikiria kuanza na ile picha ya hofu waliyojijengea akilini utakuta moja kwa moja  wanashindwa kuanza. Ziko hofu nyingi sana ambazo zinawasumbua watu kutochukua hatua, kuna wengine …

Kwanini Hupati Matokeo Unayoyataka Kwenye Kile Unachofanya?

Mpendwa rafiki, Watu wengi hawapati kile wanachokitaka katika maisha yako ni kwanini? Kwa mfano, mtu anawaza mafanikio makubwa badala ya kuwaza kufanya kazi. Bila kazi utawezaje kupata mafanikio unayoyataka? Mtu yeyote anayetaka mafanikio lazima akubali kufanya kazi hilo halina ubishi, hata ukeshe ukiomba ili upate mafanikio lakini kama hakuna juhudi yoyote unayoweka lazima tu utashindwa. …

Jinsi Ya Kupata Madeni Mbalimbali Kwenye Maisha Yako

Huwa tunajitengenezea sisi wenyewe madeni. Hakuna mtu aliyeamka anadaiwa milioni moja bali alianza kidogo kidogo mpaka ikafikia hicho kiwango kikubwa. Huwa tunapokopa tunafurahia lakini wakati wakulipa tunajihisi uchungu sana na mpaka muda mwingine tunasema kwanini nilikopa kwa ile adha ambayo mtu anakuwa anaipata. Licha ya kuwa na madeni ya kifedha lakini pia tuna madeni mbalimbali …

Amini Katika Hili Hata Kama Hakuna Anayekusapoti

Habari gani mpendwa rafiki  na msomaji wa mtandao wa Kessy Deo? Hongera sana kwa siku hii nyingine bora  ya leo na nenda kaitumie vizuri rafiki yangu. Nikualike katika makala yetu ya leo ili tuendele kujifunza rafiki. Aliyekuwa mtawala wa roma na mwanafalsafa wa falsafa ya ustoa Marcus Aurelius aliwahi kusema kuwa sisi tunajipenda wenyewe kweli …

Madhara Ya Kushindwa Kutimiza Majukumu Yako Kwenye Mahusiano Uliyonayo

Ukiangalia kwenye mitandao ya kijamii au watu wanavyoonesheana upendo kwa nje ili watu wajue wanapendana unaweza kusema kweli hakuna matatizo katika mahusiano. Lakini mambo yanakuwa ni tofauti, kuna wengine ni mabingwa wa kumwaga sifa za wenzi wao katika mitandao ya kijamii na kudai kuwa wanawapenda lakini uhalisia unakuwa hauko kwenye maisha ya kweli. Kama mtu …

UCHAMBUZI WA KITABU; Hand Book of Epictetus( Misingi Muhimu Ya Falsafa Ya Ustoa)

Unaendeleaje rafiki? nimekuwa sikushiriki uchambuzi hapa kwa muda mrefu na hii ni baada ya kuamua kubadilisha mfumo kama utakua unapenda uchambuzi wa vitabu basi jiunge moja kwa moja katika mimi ni mshindi utakua unapata uchambuzi wa vitabu kila wiki kujiunga na mimi ni mshindi nimezaliwa kushinda bonyeza hapa na pia jiunge katika mfumo wetu wa …

Kijue Chanzo Kikuu Cha Ubinafsi Hapa Duniani

Kuna bahari moja ambayo iko pale mashariki na kati hii bahari kazi  yake ni kupokea tu maji kutoka kwenye vyanzo vingine vya maji lakini yenyewe haitoi maji kwa wengine. Matokeo yake yale maji yake yamekuwa ni machafu na yananuka hayafai tena kwa matumizi ya binadamu. Sifa ya dunia ni kutoa na kupokea na hii ndiyo …

Hii Ndiyo Gharama Sahihi Unayopaswa Kulipia Kwenye mipango Yako

Tumeshazoea kuwa tukitaka kununua kitu fulani ndiyo tunalipia lakini ukijaribu kuangalia kwa jicho la tatu kila kitu hapa duniani unalipia. Kila kitu kina bei yake hata kama hutoi fedha moja kwa moja lakini kuna gharama unalipia kwa kujua au kutokujua. Ukitaka kuwa na afya bora kuna gharama yake hivyo lazima ukubali kulipia bili au bei …

Design a site like this with WordPress.com
Get started