Haya Ndiyo Malengo Ambayo Hupaswi Kuwa Nayo

Kila binadamu ana malengo yake, na furaha kubwa ya mtu ni pale anapoona lengo aliloweka amefanikiwa na hili ndiyo hitaji la watu wengi kwenye malengo, kuwa na malengo ni sawa na kuwa na shamba, haitoshi kuwa na shamba tu ndiyo utaweza kuvuna mazao, bali utahitaji maandalizi ya shamba, kupanda, kufanya palizi mbalimbali na hatimaye kuvuna. …

Hii Ndiyo Kazi Yako Kubwa Katika Mahusiano

Binadamu wote ni viumbe wa hisia na kila mmoja wetu yuko katika mahusiano kadiri ya vina saba.Hakuna mtu ambaye yuko hai halafu hana mahusiano na watu wengine.Kila mmoja wetu amejikuta amezaliwa katika mahusiano ya vina saba. Katika mahusiano ambayo tunayo, yana kitu kimoja cha uhakika ambacho ni udhaifu. Ni kawaida yetu sisi binadamu kuona madhaifu …

Pale Mtu Anapokuambia Jambo lake…

Msaidie kama liko ndani ya uwezo wako, katika maisha yetu vile tunavyoishi tunajikuta tunatengeneza jamii ya wale watu wanaoendana na sisi bila hata sisi kujua. Ila hivi ndivyo asili ilivyo, kama vile sumaku inavuta vitu vyenye asili ya chuma tu huwezi hata siku moja ukakuta imekamata vitu vya asili ya plastiki. Mtu anapokuja kwako kukuomba …

Usijione Mjanja Kwenye Hili

Huwa tunajiona sisi ni wajanja pale tunapokuwa tunamshawishi mtu na kukubaliana na sisi vile tunavyotaka. Tunafikiri kuwa kwa kuwa wameshakubaliana na sisi hivyo tayari tumeshawatawala kwa kila kitu. Unaweza kumtawala mtu kwenye vitu vyote lakini iko sehemu moja pekee ambayo huwezi kumtawala ni kwenye fikra. Usijione mjanja eti unaweza kumtawala mtu kiakili kwa sababu ni …

Kama Gharama Za Maisha Zimepanda, Chukua Hatua Hii

Kamwe hatujawahi kumpata mshindi kwa njia ya kulalamika, kulalamika kuwa gharama za maisha zimepanda ni kupoteza muda kwani huwezi kuondoa gharama za maisha kwa njia ya kulalamika. Iko njia pekee ya kufanya hivyo, maisha hayasimami hata siku moja, kama tunavyoona mabadiliko yanavyotokea kila siku, kila zama zinakuja na mabadiliko yake. Kama gharama za maisha zimepanda …

Usipoteze Muda; Chagua Kufanya Au Kutokufanya

Kama umeamua kufanya kitu basi unayo machaguo mawili tu kufanya maisha yako yote au kutokufanya maisha yako yote. Usipoteze muda wako kwa kuzuga unafanya kitu fulani halafu ukifanyi vile inavyotakiwa kufanywa. Kama umejitoa katika kazi fulani basi jitoe kweli kufanya kazi hiyo na wala usipoteze muda wako. Unayapoteza maisha yako kwa kutokufanya vile inavyotakiwa, ni …

Hii Ndiyo Kazi Inayolipa

Kila mmoja wetu anajua umuhimu wa kazi katika maisha yake. Licha ya watu wengi kufanya kazi wasizozipenda wanafanya tu ili mradi wapate fedha za kuendesha maisha yao. Siyo watu wote ambao wako duniani wanajua wamekuja kufanya nini, wengi hawajui kusudi la maisha yao hapa duniani. Laiti kama kila mmoja wetu akijua haswa amekuja kufanya nini …

Hiki Ndicho Kinachowapoteza Watu Wengi Kwenye Zama Hizi

Tuko kwenye zama za maarifa na taarifa, ili ufanikiwe unahitaji uwe na maarifa sahihi na taarifa sahihi. Kwenye zama hizi, maarifa na taarifa zimekuwa nyingi sana kiasi kwamba zinawavuruga hata watumiaji, hizi ni zama za mafuriko na taarifa, unahitaji uwe na vigezo vya kuchuja kila aina ya maarifa na taarifa unazopata ili uweze kuzitumia vizuri. …

Usifikie Mahali Ukajiuliza Swali Hili Kwenye Maisha Yako

Ukitafuta sababu kwanini maisha yako yamekuwa jinsi yalivyo leo huwezi kukosa sababu wala watu wa kuwalaumu ambao wamesababisha wewe kuwa hivyo ulivyo, hata kama utawapata kweli na kuwatupia kila aina ya lawama haiwezi kusaidia kitu kwani matokeo ya maisha yako ya leo, mchangiaji mkubwa ni wewe mwenyewe wala siyo mtu mwingine. Tuwe watu wa kujikamata …

Hii Ndiyo Sababu Inayokufanya Uyumbishwe Kwenye Maisha Yako

Kama umeamka asubuhi na hujui nini unakwenda kufanya utajikuta siku inakuyumbisha na huku ukiendelea kuendeshwa na matukio na siyo kadiri ya ratiba ya siku yako. Hapa ndiyo inakuja ile dhana kwamba usipoipangilia siku yako na kusema unataka nini na hutaki nini utajikuta unapata kile ambacho hata hukutegemea kukitaka kwenye maisha yako. Kama unaishi maisha ambayo …

Design a site like this with WordPress.com
Get started