Tumia Mbinu Hii Kama Hutaki Kupata Kile Usichotaka

Kama unataka usipate kile usichotaka usikifikirie kitu hiko badala yake fikiria kile unachotaka. Siku zote ukifikiria kile usichotaka ndiyo unakipata. Kwa mfano, kama una madeni usifikirie madeni badala yake fikiria namna ya kupata fedha zaidi. Akili ya kutekeleza yaani subconscious mind huwa haina utambuzi hivyo chochote kile kinachokuja akilini kinatekeleza bila kujua ni sahihi au …

Hii Ndiyo Hatua Ya Kuchukua Pale Unapoona Kitu Hakikupi Faida

Siyo kila kitu unaweza kukomaa nacho mpaka mwisho na kikakupa faida uliyokuwa unataka. Hakuna mtu ambaye anaweza kufanya kazi isiyokuwa inamlipa kwa sababu kila mtu anahitaji fedha ili aendeshe maisha yake. Maneno hayajawahi kulipa bili hata siku moja bali fedha pekee. Hatua muhimu unayopaswa kuichukua pale unapoona kitu hakikupi faida ni kuacha. Usiogope kuacha kitu …

Huu Ndiyo Utajiri Pekee Unaodumu

Huwa tunajidanganya sana kuwa pale tunapomiliki vitu vingi ndiyo tunajiona kuwa sisi ndiyo matajiri. Kumbe siyo, utajiri hauko kwenye kuwa na vingi bali utajiri uko sehemu moja pekee ambayo ni utajiri wa kutoa. Utajiri unaotoa ndiyo utajiri unaodumu. Unapomsaidia mtu wewe unaweza kuona kama ni kawaida lakini wale wanaopokea msaada wako ndiyo watu wanaokumbuka sana …

Jinsi Ya Kuepuka Kuwa Na Maadui Wengi

Wape watu nafasi ya kujielezea wao zaidi kuliko wewe. Usiwe mtu wa kupenda kujisifia sana pale unapokuwa na watu huwa wanakereka na tabia hii. Usipende kuibua wivu usiokuwa wa maana kwa kitendo cha kujisifia mafanikio yako mbele za watu.Mafanikio binafsi usiyaanike kwa watu maana utaibua wivu na matokeo yake mahusiano yanavunjika. Unapokuwa mtu wa kuongea …

Jinsi Ya Kuepuka Maumivu Ya Fedha Baada Kupoteza Fedha Zako

Ni kawaida watu kupigwa kwenye suala la fedha. Wale wanaotafuta mafanikio ya haraka kwao kupigwa fedha ni jambo la kawaida sana. Wengi wamelizwa na matapeli kwenye eneo la fedha, wengine wameibiwa na kutapeliwa fedha kwa njia ya simu na nk. Baada ya kutapeliwa fedha huwa tunakua na maumivu makubwa sana. Kama tunavyojua tena kutoa pesa …

Dalili Ya Kwanza Inayoonesha Unafanya Makubwa

Mtu pekee ambaye ameshamaliza changamoto zake hapa duniani ni marehemu tu, lakini kama unaishi bado changamoto zitaendelea kuwa na wewe na zitakoma pale tu mwili ukapojitenganisha na roho. Kiukweli, kila mtu kuna changamoto anayopitia katika maisha yake, hata ukiwaona watu wako kimya, wanafurahia usije ukasema kuwa hawana kitu kinachowasumbua, kila binadamua kiasili kuna kitu kinamsumbua. …

Tulia Na Akili Yako Itakupa Jibu

Imeshawahi kukutokea hali fulani ambayo unajikuta umesahau kabisa kitu unachojua? Unailazimisha akili yako ikupe jibu lakini wala haikupi. Wakati mwingine unaweka kitu mahali halafu unajikuta umesahau wapi ulipoiweka lakini baadaye ukikaa ukitulia unakuja kukumbuka. Mara nyingi akili ikitaharuki inakosa ufanisi wake wa kazi. Akili yako itajibu maswali yote kama utajifunza kutulia na kusubiria jibu aliwahi …

Hawa Ndiyo Watu Wanaojenga Ufalme

Unaposikia neno ufalme unapata picha gani?Na picha uliyopata unafikiri ni nani anayehusika kujenga ufalme? Chochote kile unachotaka kutawala hapa duniani unatakiwa uwe na kitu kimoja ambacho ni nguvu. Ufalme wowote ule unajengwa na watu wenye nguvu kwani kama huna nguvu yoyote ile hakuna atakayeweza kukusikiliza. Nguvu ni nyenzo muhimu sana kwa binadamu. Kama huna nguvu …

Kama Huwezi Kufanya, Chukua Hatua Hii

Siyo lazima kufanya kila kitu, na kitu ambacho kimekushinda hakiwezi kuwashinda watu wote bali kutakuwa na mtu ambaye anaweza kukifanya kitu hiko. Kama huwezi kile ambacho huwezi kufanya kaa pembeni waachie wale wanaoweza kufanya na wewe nenda kafanye kile unachoweza kufanya wala usijibe shida wakati kuna mambo ambayo yako ndani ya uwezo wako. Usiseme kitu …

Huwezi Kuzuia Tukio Lisitokee Bali…

Huwa tunapambana na vitu vingine ambavyo viko nje kabisa ya uwezo wetu. Lakini wengine hatulijui hilo. Sisi binadamu tunao ukomo wa vitu hapa duniani, viko vile ambavyo viko ndani ya uwezo na viko vile ambavyo viko nje ya uwezo wetu. Mtu anayependa kitu fulani kisitokee ni kitu ambacho kipo nje ya uwezo wake, kwa mfano, …

Design a site like this with WordPress.com
Get started