Penda Hatima — Amor Fati

Falsafa ya Ustoa Inayokupa Uhuru, Utulivu na Ujasiri wa Kuishi Maisha Halisia Kwenye falsafa ya Ustoa (Stoicism), kuna wazo moja la kipekee, lenye nguvu kuliko malalamiko yote ya mwanadamu, na lenye uwezo wa kubadilisha maisha yako kabisa.Wazo hilo linaitwa Amor Fati, tafsiri yake: “Penda hatima yako.” Si kukubali tu kinachokupata.Si kuvumilia tu kinachotokea.Ni zaidi ya …

Ukichaa Wa Muda

Rafiki yangu nikupendaye, Hisia zinapokuwa juu, fikra zinakuwa chini. Na fikra zikiwa chini, uwezo wetu wa kufanya maamuzi unakuwa chini. Kila mmoja kuna wakati anakua na ukichaa wa muda. Na ukichaa wa muda ni hasira. Hasira ni ukichaa wa muda, wakati una hasira, fikra zinakuwa chini ndiyo maana inapelekea kufanya maamuzi yasiyofaa. Ndiyo maana unashangaa …

Usiende Kinyume Na Asili

Mpendwa rafiki yangu, Kama utayaendesha maisha yako kadiri ya asili basi hautakuwa na maisha magumu. Kinachofanya maisha kuwa magumu, ni watu kuhangaika na vitu vingi. Kiasili, mahitaji ya msingi ni machache lakini anasa ndiyo zinafanya maisha kuwa magumu. Maisha tayari ni magumu, usiyafanye kuwa magumu zaidi kwa kuhangaika na mambo mengi.Jitafute na ukishajipata, tulia kwenye …

Jinsi Ya Kukabiliana Na Hali Pale Mambo Yanapoenda Vibaya

Ni wazi kabisa mambo hayawezi kwenda kama vile unavyotaka wewe. Dunia haiwezi kwenda kadiri ya matakwa yako. Dunia inaenda kadiri ya vile inavyotaka. Mambo yanatokea kama yalivyopangwa kutokea. Unawezaje kukubaliana na mambo pale yanapokwenda vibaya? Jibu, ni wewe kutokwenda vibaya kama mambo yalivyoenda. Kumbuka, mambo yameenda vibaya usikubali na hayo mambo yakuendeshe na wewe uwende …

Wakati Mzuri Wa Kununua Mwamvuli

Wakati mzuri wa kuandaa paa lako ni wakati jua linawaka. Hii ina maana kwamba muda mzuri wa kujiandaa na kitu ni kabla ya kile kitu hakijatokea. Unaona wazi jinsi mvua inaponyesha miamvuli inauzwa kwa bei kubwa. Kama hutaki kununua mwambie kwa bei kubwa basi nunua kabla ya mvua.Muda mzuri wa kujiandaa na dharura ni kabla …

Usimwambie Mtu, Nimekuambia Wewe Tu

Ni maneno ambayo watu huyatumia kujihakikishia usalama pale wanapotoa jambo lao kwa watu wengine. Usijidanganye kwamba ukimwambia mtu hivyo ndiyo mambo yatakuwa safi bali ndiyo kama vile umemwambia fanya. Kama una jambo lako na unataka watu wasijue ni bora usiseme kabisa kuliko kusema halafu unamwambia nimekuambia wewe tu lakini usimwambie mtu mwingine.Wimbo unakuwa ni mmoja …

Swali Muhimu Sana La Kujiuliza Pale Tu Unapokutana Na Kitu Usichotegemea

Mwandishi Deepak Chopra anasema hakuna ajali, ila kuna kusudi ambalo bado hatujalijua. Mara nyingi mambo yanapotokea kwenye maisha yako bila ya wewe kutegemea kutokea huwa yanapotokea unasema ni ajali. Lakini Chopra anatuambia hakuna ajali, badala yake kuna kusudi ambalo bado hatujalijua. Kila kinachotokea kwenye maisha yako, iwe ni kizuri au kibaya jua kimekuja na kusudi …

Sheria Unayopaswa Kuiogopa Kwani Haina Huruma Na Mtu

Kiasili hakuna kitu kibaya wala kizuri hapa duniani. Mara nyingi huwa tunapokea kile tunachotoa. Leo nataka nikupe sheria moja ambayo ukiifuata utakua na maisha mazuri na ukienda kinyume nayo utakua na maisha magumu. Sheria hiyo inaitwa karma. Karma ni sheria ya asili ambayo inamrudishia mtu kile ambacho amekitoa kwa mwingine. Kwa mfano, ukimfanyia mtu kizuri, …

Hakuna Kifo Kibaya Kama Hiki

Memento Mori#2Death is not the greatest loss in life. The greatest loss is what dies inside us while we live. – Norman Cousins Kifo kibaya na kikubwa ni kile ambacho watu huwa wanakufa na utajiri ndani yao wakati wakiwa hai.Kifo siyo kitu kikubwa kama kufa ukiwa hujatimiza ndoto yako ambayo iko ndani yako. Fikiria vitu …

Design a site like this with WordPress.com
Get started