Hiyari Yashinda Utumwa

Rafiki, USIPENDE kuwa mtu wa kukumbushwa kufanya kila kitu.Ukitaka kuwashawishi watu kuwa mtu wa kujituma na kufanya bila kuambiwa.Ukiona kitu ni wajibu wako basi jitume bila kusubiri kuambiwa. Kama uko kwenye mahusiano, fanya kile ambacho unapaswa kufanya kwenye mahusiano uliyopo.Ukijituma na kufanya bila kuambiwa, dunia itakuheshimu. Hakuna utumwa mbaya kama wa kuambiwa kila kitu.Ili ufanye …

Msaada Ambao Hauwezi Kukusaidia Wewe

Rafiki, Duniani hakuna jeshi la mtu mmoja. Kwa sababu, tunawategemea watu wengine ili kukamilisha mambo yetu muhimu. Msaada ni muhimu sana kwenye maisha yetu. Lakini, msaada wa nje hauwezi kumsaidia mtu yeyote ambaye ameshajiwekea ukomo ndani yake. Mtu ambaye ameshajiwekea ukomo ndani yake, ni ngumu kumsaidia. Kwenye fikra zetu, huwa tunajifunga na fikra zetu wenyewe. …

Mtu Ambaye Hajawahi Kuzuiwa Na Chochote Kile

Rafiki, Kama hujapata kile unachotaka kwenye maisha yako, maana yake bado hujajitoa vya kutosha kupata kile unachotaka. Mtu anayedhamiria kukitaka kitu, huwa anakipata kweli bila kuzuiwa na chochote kile. Mtu mwenye nia ya kufanya kitu au kutaka kitu fulani kwenye maisha yake, hajawahi kuzuiwa na chochote kile.Kwenye maisha yako, ukitaka kitu ongozwa na tamaa ya …

Vitu Viwili Muhimu Sana Utakavyovipata Kwenye Mauzo

Rafiki yangu nikupendaye,Lengo kubwa la kila mmoja wetu hapa duniani anapokuwa anafanya kitu ni kupata matokeo fulani. Mtu anapokuwa anafanya kazi, anategemea kupata fedha na hata kujega koneksheni mbalimbali na watu wengine.Habari njema ni kwamba, hata kwenye biashara au ajira tunafanya ili tupate fedha hilo ndilo linakuwa lengo letu kuu. Sasa kwenye mauzo, ambapo kila …

Komesha Tabia Ya Watu Hawa

Rafiki, Sina uhakika kama itakufaa lakini, kuna watu watakuja kwako wakiwa wanataka kitu kutoka kwako. Kuna mtu ambaye hamjawahi kuwasiliana kwa miaka mingi, siku moja anakupigia simu, anakuambia nakusalimia tu, halafu kwenye simu hiyo hiyo anakuomba umfanyie kitu, au umsaidie kitu. Hii ni tabia ya watu ambayo unapaswa kuijua, kwamba watu watajaribu kukutumia, watu watakuja …

Rafiki Ambaye Hawezi Kukusaliti

Rafiki yangu nikupendaye, Watu ambao unapaswa kuwaheshimu sana hapa duniani ni wateja wako na bosi wako.Kwa sababu hao ndiyo wanafanya maisha yako yaende kwa kukupa fedha ya kuendesha maisha yako.Bila fedha, hata watu wako wa muhimu utashindwa kuwahudumia na hata kukosa heshima yako. Waswahili wanasema, mkono mtupu haulambwi. Bila fedha utakua ni wa kupuuzwa.Ni bora …

Kitu Bora Ambacho Binadamu Anaweza Kufanya

Rafiki, Ili mwili ufanye kazi vizuri, basi lazima kila kiungo kwenye mwili kifanye kazi yake na tena kwa ushirikiano. Asili ya binadamu ni kushirikiana. Ndiyo maana hapa duniani hauko peke yako, bali uko na wengine katika kujega mambo mengine.Aliyekuwa Bilionea Charlie Munger aliwahi kunukuliwa akisema, kitu bora ambacho binadamu yeyote anaweza kufanya ni kuwasaidia binadamu …

Utajiri Wa Mtu Uko Hapa

Huwa tunajua kwamba utajiri wa uko kwenye vile anavyomiliki, kile alichonacho. Utajiri wa mtu, uko kwenye kile anachojua na siyo kile alichonacho. Kile anachojua mtu ndiyo kinampa utajiri wa kile kinachowezekana. Utaweza kumnyang'anya mali lakini kile anachojua ambacho ni akili na maarifa aliyonayo atakitumia kukirudisha. Hata leo hii watu wote wakipewa fedha sawa duniani, haitochukua …

Kazi Yako Kubwa Ni Hii Hapa

Rafiki yangu nikupendaye, Kwenye maisha yako, kazi yako kubwa ni kupata unachotaka. Hakuna kitu kingine. Kama kazi yako ni kupata unachotaka, unatakiwa kuweka fokasi kwenye kile unachotaka mpaka ukipate kweli. Unatakiwa kupambana na dunia na kuionesha kwamba kila kitu kinawezekana. Kama kwenye ukoo wenu, hakuna aliyeenda hatua ya ziada, nenda wewe kwa kuwaonesha kwa mfano. …

Bora Kuchukiwa Kuliko kupuuzwa

Ni bora watu wakuchukie kwa sababu ya wewe unajituma kwenye kile unachopaswa kufanya kwenye maisha yako kuliko kupuuzwa. Kupuuzwa maana yake ni kwamba huna unachofanya. Kupuuzwa kunauma kuliko hata kuchukiwa. Watu ambao wanakufanyia ndivyo sivyo kwenye maisha yako, dawa yao ni kuwapuuza. Unapowapuuza watu, kwenye kile wanachokufanyia, wanapoteza nguvu ya kutokuendelea na kile wanachofanya.Kupuuza ni …

Design a site like this with WordPress.com
Get started