Jenga Utamaduni Huu Kwenye Maisha Yako

Rafiki, Kila sehemu inapaswa kuwa na utaratibu na watu wanafuata utaratibu huo.Hakuna sehemu ambayo huwa inajiendea tu kienyeji, bali kuna kuwa na utaratibu ambao unakuwa ni utamaduni wa eneo hilo na watu wanafuata. Kama una biashara yako, jenga utamaduni wa biashara yako, ambapo kila mtu anapaswa kufuata utamaduni huo na siyo kila mtu kuja na …

Hawa Ndiyo Watu Wanaotaka Wewe Ufanikiwe

Rafiki, Kwenye maisha yako, usiwe na mtu au watu ambao wanakuzuia wewe usifanikiwe.Mtu ambaye anakuzuia wewe usifanikiwe ni adui yako huyo hupaswi hata kumpa nafasi ya kumsikiliza.Watu wanaokujali ni wale ambao wanataka wewe ufanikiwe. Mtu anayetaka wewe ufanikiwe ni yule anayekujali wewe kwa kukupa sapoti ili mambo yako yaende. Ambaye yuko kinyume na wewe, huyo …

Ijaze Akili Yako Haya

Rafiki, Pata picha umekaa sebuleni kwako na akaja mtu na kifurushi cha uchafu na kukumwagia hapo je, utafanyaje? Utamwachia kweli? Pale mtu anapopataka kutuharibia mazingira yetu ya nje, huwa hatukubali hata kidogo. Lakini, tuko tayari kuharibiwa akili yetu na akili ndiyo imebeba kila kitu. Tunakubali kuingiza kila kitu kwenye akili zetu bila hata ya kuchukua. …

Usijali

Rafiki, Kwenye watu kuna mengi na ukisema ufuatilie kila mtu anachofanya au kusema huenda ukakosa hata muda wa kufanya mambo yako binafsi. Mtu akikusoa wala hata usijali, Mtu akikusema vibaya wala hata usijali, Kwa sababu, hiyo ndiyo kazi waliochagua kuifanya. Wewe unachotakiwa kujali ni kazi yako.Kila mtu hapa duniani anajichagulia kazi ya kufanya, wengine kazi …

Hiki Kitu Hakiwezekani

Rafiki, Kwenye maisha kila kitu kinahitaji uwekezaji mzuri ili kukuletea matokeo mazuri. Na uwekezaji wowote ule utakaofanya lazima unahitaji muda, fedha na uvumilivu. Hakuna sehemu ambayo utavuna bila kupanda. Kila mtu anajua jinsi kilimo kilivyo na wengi wetu tunatokea au tumekulia katika shughuli za kilimo. Tunajua kwamba kilimo kinahitaji uwekezaji, muda , fedha na uvumilivu. …

Hii Siyo Maana Ya Mafanikio Kwako

Rafiki, Huwa tunaamini kuwa, mafanikio siyo kupata hiki na kukosa kile, siyo kutumia muda mwingi kwenye kazi na kukosa muda na familia, siyo kuwa bize na kazi na kusahau afya yako. Mafanikio ni kuwa na kila kitu, kuwa na fedha nyingi, kuwa na afya bora, kuna na mahusiano mazuri na wengine, kuwa vizuri kiimani na …

Breki Ya Mahusiano Inayokuzuia Usifanikiwe

Mwanamafanikio, Hakuna kazi kubwa hapa duniani kama kuishi na kuhusiana na watu. Watu ni wagumu kuelewa na unakutana na watu ambao wana mitazamo tofauti na wewe. Mazingira tofauti ambayo anayajua yeye mpaka mje kuelewana inakuwa ni kazi kubwa. Hakuna mtu ambaye anaweza kusema yeye kwenye eneo la mahusiano amelipatia, yaani anao uwezo wa kusema na …

Usivumilie Kitu Hiki Kwenye Maisha Yako

Rafiki, Usivumilie kitu chochote ambacho hukipendi kwenye maisha yako, hata kama kila mtu anavumilia, hata kama kila mtu anachukulia kawaida.Kama kitu hukipendi, au kama unaona siyo viwango vyako, usikubaliane nacho, wewe fanya kazi kupata kile unachotaka, kile ambacho ni viwango vyako.Nenda hatua ya ziada kuhakikisha unapata kile unachotaka kwenye maisha yako na siyo kuvumilia. Waliozoea …

Kesho Utavaa Nguo Gani?

Rafiki, Siyo mara moja ukiamka asubuhi huwa unaanza kujiuliza swali hivi leo nitavaa nguo gani? Siyo kwamba nguo hauna, nguo unazo nyingi kiasi kwamba hujui hata uvae ipi kulingana na mahitaji ya siku yako. Kitendo cha kuamka na kuanza kufikiria utavaa nguo gani tayari kinakuwa ni breki kwako katika uzalishaji wa siku na hata mafanikio …

Athari Za Kwenda Kinyume Na Makubaliano

Rafiki, Ukiona watu wanagombana basi jua mmoja kashindwa kwenda kadiri ya makubaliano au ameenda kinyume na makubaliano. Kwenda kinyume na makubaliano ndiyo chanzo cha matatizo mengi kwenye maisha yetu. Kwenye mahusiano, kila mtu anakuwa na makubaliano na mwenzake kwamba, tumekubaliana hivi, na tutaenda hivi na endapo mtu atakwenda kinyume na matatizo ndiyo yanaanzia hapo. Kila …

Design a site like this with WordPress.com
Get started