Kitakachokufanya Ufanikiwe Ni Hiki Hapa

Waswahili wanasema hiyari ya SHINDA utumwa. Kama mtu akiwa anafanya mambo yake bila kuambiwa au kukumbushwa huwa inapunguza utumwa. Ukifanya bila kuambiwa hutaona kama ni utumwa lakini ukifanya mpaka uambiwe utaona ni utumwa. Wote tunajua kwamba, mafanikio siyo kitu rahisi kwenye maisha yetu. Ili ufanikiwe kwenye jambo lolote lile, inahitaji kazi kubwa. Mafanikio hayahitajiki mtu …

Kinachotoa Mrejesho

Rafiki, Unaweza ukajiandaa vizuri sana na muda mwingine ukajiona uko bora kabisa. Umezalisha bidhaa yako na ukawa unajiamini kwamba utakwenda kuuza lakini mambo yasiende tofauti. Unaweza kuandaa na kutoa thamani, lakini soko ndiyo linaamua na kutoa mrejesho juu ya thamani yetu. Unaweza ukajiandaa vizuri na mchezo lakini asili ikaamua tofauti na mipango yako. Kinachotoa mrejesho …

Unaingia Gharama Kwa Kufanya Hivi

Unaingia gharama kwa kutokufanya maamuzi. Kwa mfano, kama kuna kitu unataka kukifanya na hukifanyi tayari unakuwa unalipia gharama kwa sababu ya kutokufanya maamuzi. Kama kuna gharama unapaswa kulipa na hulipi jua tayari unalipa gharama hiyo bila wewe mwenyewe kujua. Hutakiwi kukwepa kitu, kama unapaswa kufanya, fanya tu kwa sababu hakuna namna unavyoweza kukwepa. Leo kaa …

Utalivuka Daraja Pale Utakapolikuta

Watu huwa wanateseka na mambo yajayo kiasi kwamba wanashindwa hata kufanya yale wanayopaswa kufanya sasa.Kitendo cha kufikiria kesho itakuwaje, inachosha zaidi kwa sababu hakuna mtu ambaye ana uhakika wa kesho. Huwa tuna mambo mengi ambayo yanatusumbua lakini hatupaswi kuyapa uzito sana hayo mambo kiasi kwamba yatuvuruge kufanya yale tunayopaswa kufanya sasa. Najua una mambo mengi …

Hii Ndiyo Injini Ya Biashara Na Viwanda

Rafiki, Mauzo ndiyo injini ya mfumo wa biashara na viwanda. Kiwanda hakiwezi kuendelea kuzalisha kama hakuna mauzo, biashara haziwezi kufanyika kama hakuna mauzo. Mauzo ndiyo kila kitu kwenye maisha yetu. Bila mauzo hakuna kitu kinachofanyika. Hivyo mauzo ni injini inayoendesha mfumo mzima wa biashara na viwanda, ndiyo kitu kinachochochea uzalishaji zaidi wa bidhaa na huduma. …

Jifunze Kwa Watu Hawa

Rafiki,Jifunze kwa walioshindwa. Angalia watu wako wa karibu, wameshindwa kufanya nini na wewe epuka kuwa kama wao au kufanya kama wao. Angalia baba, mama, mjomba, watu wa karibu kwako, marafiki na kadhalika yako walishindwa kwa sababu gani na wewe usiwe kama wao. Kuna mambo mengi ambayo tunaweza kujifunza kwa walioshindwa na sisi tutakawa bora.Habari njema …

Bado Hujamaliza Kazi

Maisha ni mwendelezo wa mabadiliko, kazi na ni kazi ambayo haina mwisho. Kama upo hapa duniani, unaweza kusema umemaliza kazi lakini bado hujamaliza kazi. Ukiwa na jukumu fulani kwenye maisha yako, unakuwa unajipa moyo kwamba nikimaliza, basi nitakuwa nimemaliza kazi.Mwingine atakuambia nikimaliza kusomesha nitakuwa nimemaliza kazi. Kwa mfano, mzazi kumpeleka mtoto shule na kulipa ada …

Kuwa Bingwa Kabla Hujawa Bingwa

Mchezo mzima wa ushindi huwa unaanza kujengwa kwa mtu hata kabla hajawa mshindi.Na sehemu nzuri ya kuanza kuwa mshindi kabla hujawa mshindi ni kuanza kujijengea ile picha ya kuwa unayemtaka mapema. Ushindi huwa unaanza picha kubwa iliyojengwa kwenye akili ya mtu. Kabla mtu hajaingia kwenye mchezo, anakuwa tayari ameshashinda kiakili. Kuwa bingwa kabla hujawa bingwa …

Hivi Ndivyo Unavyofanya Vitu Vyote

Rafiki yangu nikupendaye, Watu wakitaka kukupima kwa namna unavyoyaendesha maisha yako, wanakupima kwa kitu kimoja tu na wala siyo vingi.Mtu akikuangalia tu kwa kitu kimoja kwa namna unavyofanya, anakuwa amepata picha ya wewe ni mtu gani. Iko hivi, jinsi unavyofanya kitu kimoja, ndivyo unavyofanya vitu vyote. Watu wakitaka kuona huwa unafanyaje mambo yako, huwa wanaangalia …

Jifunze Kwenye Kila Kosa

Rafiki, Lengo siyo kuepuka makosa kwenye maisha yetu bali ni kujifunza kutokana na makosa tunayofanya. Kila mtu anakosea na utakosea mara nyingi kwenye maisha yako, lengo siyo kuepuka kukosea bali kuhakikisha unajifunza kwenye kila kosa unalofanya ili usirudie tena kosa la aina hiyo. Waelewe wengine pale wanapokosea kwa sababu hata na wewe mwenyewe unakosea.Wafundishe watu, …

Design a site like this with WordPress.com
Get started