Ukiwa Na Vitu Hivi Viwili, Mafanikio Kwako Ni Lazima

Ukikimbiza sungura wawili, hutampata hata mmoja.Hii ina maana kwamba, ukifokasi na mambo mengi, huwezi kukamilisha hata moja kwa ubora. Ukijua wapi unakwenda, huwezi kupotea njia. Kwenye maisha, ukiwa unajua nini unataka, lazima utakipata. Jua unachotaka, kisha watafute watu ambao wameshafika kule unakotaka kufika au wenye ndoto kama wewe na wanapambana kwenda kule unakotaka kufika. Ukishakuwa …

Usishangae

Kwenye haya maisha hupaswi kujiumiza, kulaumu au kushangaa pale mambo yanapokwenda tofauti na ulivyopanga. Kila unapoamka jua kwamba wewe umepanga lakini na dunia imepanga pia.Ni vizuri sana kujiandaa pia kwa upande wa pili wa matokeo. Kama ULIPANGA leo lazima ushinde kwenye kile ulichopanga, jua nayo dunia inapanga. Unapaswa kuwa na ukomavu wa hali ya juu. …

Anza Na Haya Kwanza

Huwa tunapenda kuhangaika na mambo makubwa wakati mambo madogo yenyewe hatuyafanyi vile inavyotakiwa kufanywa. Kabla hujakimbilia mambo makubwa, angalia yale ya msingi kwanza umeshayafanya? Tunayo mambo mengi ya msingi kabisa hatuyafanyi halafu tunataka mambo makubwa. Anza na mambo ya msingi kwanza UNAYOPASWA kuyafanya ndiyo ukimbilie mambo makubwa. Unakwama kwenye mambo makubwa kwa sababu hata yale …

Watu Wakichoka Huwa Wanafanya Vituko

Ni asili ya binadamu kama hapendi au hataki kitu, hawezi kukuambia wazi. Atakuonesha kila aina ya vituko au vipingamizi vya kuepukana na wewe.Unaweza kuwa na mtu unajua mko pamoja kumbe hapana. Kama mfanyakazi amechoka kufanya kazi na wewe, ataanza kukuonesha drama mbalimbali. Kama uko kwenye mahusiano vile vile mchezo ni ule ule, mtu ataanza kukuonesha …

Tegemea Kuangushwa

Wewe siyo kiranja wa dunia. Kwamba mambo yako kila siku yataenda kama vile unavyotaka. Unapaswa kuwa na unyenyekevu kwamba, dunia haiwezi kwenda vile unavyotaka wewe hata iweje.Uwe na mamlaka au huna, dunia haijali sana kuhusu hilo. Kuna uhakika fulani huwa tunajipa kwenye maisha yetu. Kwa sababu nina mamlaka juu ya kitu fulani au mtu fulani …

Kabla Ya Kuongea Jiulize Hivi

Rafiki yangu nikupendaye, Mwanafalsafa Plato anasema Werevu huongea kwa sababu wana kitu cha kuongea, ila wapumbavu huongea kwa sababu inabidi waseme kitu. Kama huna kitu cha kuongea, ni vema usiongee kitu. Kaa kimya, utaonekana mtu mwenye hekima. Wakati wowote unapotaka kuongea, jiulize je una kitu cha kuongea au na wewe unataka usikike tu kwamba umeongea? …

Majadiliano Yanatokea Wapi Tena?

Kabla hujapata fedha, unakuwa na mawazo mazuri sana. Unapanga kabisa ukipata fedha, kitu cha kwanza kufanya ni kuwekeza. Chakushangaza ni kwamba, pale tu unapoishika pesa, majadiliano ya ndani yanaanza. Utoe au usitoe.Majadiliano hayo yanatoka wapi? Kama ulishapanga kabla ya kupata fedha, tekeleza haraka na wala usiruhusu majadiliano.Hisia za kutokuwekeza huwa zina nguvu sana. Utaanza kujadiliana …

Kuwa Daraja La Wengine

Mafanikio yetu hapa duniani yanategemea wengine.Tunapaswa kuwa watu wa msaada kwa wengine, kuwasaidia wengine kwenye kile wanachopitia. Mafanikio yetu yanatokana na wengine. Kwa sababu chochote kile ambacho sisi hatuna, tunakipata kutoka kwa wengine. Wewe unaweza kuwa kikwazo kwa mtu mwingine kutokufanikiwa pale unaposhindwa kutimiza wajibu wako vizuri. Wewe unaweza kuwa daraja la wengine kufanikiwa pale …

Jifunze Kuwa Na Hivi Vitu

Mafanikio siyo kupata hiki na kukosa kile, siyo kutumia muda mwingi kwenye kazi na kukosa muda na familia, siyo kuwa bize na kazi na kusahau afya yako. Mafanikio ni kuwa na kila kitu, kuwa na fedha nyingi, kuwa na afya bora, kuna na mahusiano mazuri na wengine, kuwa vizuri kiimani na kuweza kushirikiana na wengine. …

Unaipeleka Wapi Nguvu Yako?

Rafiki yangu nikupendaye, Kila mtu ana nguvu ya kupenda kitu ndani yake. Changamoto ni kwamba nguvu hiyo unaipeleka wapi? Wapo ambao wanapeleka nguvu hiyo kwenye kufanya kazi, wapo wanaoipeleka kwenye kusaka fedha na wapo wanaopeleka nguvu hiyo kwenye ulevi na uteja. Wapo pia wanaopoteza nguvu hiyo kwa kupenda vitu ambavyo havina faida kwao, mfano kufuatilia …

Design a site like this with WordPress.com
Get started