Kama Unataka Kufika Mbali, Fika Kwanza Hapa

Rafiki yangu nikupendaye, Hakuna kitu ambacho kinatukwamisha kwenye maisha yetu kama ukomo ambao tumejiwekea kwenye kila eneo la maisha yetu. Tumeshajiwekea ukomo kwenye akili zetu kiasi kwamba hata mtu atuambie vipi akili zetu zinakataa. Kama akili yako umeshaiwekea ukomo, hakuna kitakachotokea mpaka pale utakapoifungua. Akili yako inakupa kile ambacho umekiaminisha.Kama unataka kufika mbali, anza kwanza …

Una Hangaika Na Mambo Gani?

Rafiki yangu nikupendaye, Kuna wakati huwa tunajikuta ni watu ambao tunajali sana matatizo ya watu.Tunashindwa kufanya yale tunayopaswa kufanya, nakujikuta ni viranja wa dunia. Wewe ni biashara iliyokamilika, unapata wapi muda wa kuhangaika na mambo ya yasiyo na tija kwako? Pambana na yale ambayo tija kwako. Kama kitu hakikusaidii wewe kupata fedha zaidi, achana nacho. …

Sheria Ya Asili Ambayo Watu Hawapendi Kuisikia

Rafiki yangu nikupendaye, Dunia huwa inatupa vitu, wakati mwingine kwa juhudi ambazo tumeweka na wakati mwingine kwa bahati tu. Bahati kwa mfano kupata fedha kwa njia ya bahati nasibu. Lakini dunia pia huwa inatunyang’anya chochote ambacho hatutajifunza jinsi ya kukipata, hatutajifunza kulipa gharama zake. Jua gharama unayopaswa kulipa kwenye kila kitu na kuwa tayari kuilipa. …

Mbinu Moja Ya Kuimarisha Mahusiano Yako

Rafiki yangu nikupendaye, Mahusiano ni sehemu ya maisha yetu.Elimu nyingi tunazopata kila siku ni jinsi ya kuishi na binadamu katika mahusiano ambayo tupo. Tunayo mahusiano ya ndoa, kazi, biashara na nk. Tunayo kila sababu ya kulinda mahusiano tuliyokuwa nayo. Unaweza kuona mahusiano uliyonayo hayana maana, lakini ukiyapoteza utaumia. Ipo mbinu moja ambayo ukiitumia katika mahusiano …

Mbinu Ya Kupata Ushindi Kwenye Zama Za Mambo Mengi

Rafiki yangu nikupendaye, Mambo uliyokuwa nayo ni mengi, na muda wa kufanya yote hayo hakuna.Na watu wako bize kweli, hata uliongea na mtu, uwepo wake unakuwa haupo pale.Hivyo ni rahisi sana kusahau kile ulichomwambia. Kwa zama hizi watu hawapumziki wala hawafanyi kazi.Hii ina maana kwamba, muda wa kazi watu wafikiria KUPUMZIKA.Muda wa KUPUMZIKA mtu anawaza …

Usishangae Haya Yakitokea

Rafiki yangu nikupendaye, Huwa tunashangaa sana pale tunapoona watu tunaohusiana nao wanapobadilika.Tunaona ni kitu cha ajabu sana wao kubadilika. Kama ulikuwa hujui, asili ya watu ni kubadilika.Mtu uliyekuwa kuwa naye sasa na utakayekutana naye kesho kisaikolojia ni mtu mwingine tena. Ili usijiumize na haya maisha kwa sababu ya watu kubadilika, ishi dhana kwamba yule uliye …

Maana Halisi Ya Thamani

Rafiki yangu nikupendaye, Huwa tunasema sana au umeshasikia watu wakisema kwamba ili ufanikiwe unapaswa kutoa thamani. Swali la kujiuliza je, unajua nini kuhusu thamani? Unasikia ukiambiwa kwamba, toa thamani kwa mteja.Ni kweli, kwenye biashara, kazi au huduma, unapaswa kutoa thamani kwanza ndipo uweze kupokea. Watu kwa asili ni wabinafsi, hivyo usipokuwa mtu wa kujali maslahi …

Vitu Viwili Vinavyokuzia Kupata Unachotaka

Rafiki yangu nikupendaye, Kwa haya yote unayojifunza, kwamba unaweza kupata chochote unachotaka, mawazo yako yanavuta chochote unachofikiria, unaweza kuhisi ni uongo kwa sababu labda wewe umejaribu lakini hujapata ulichokuwa unataka. Kama hivi ndivyo unavyofikiria, basi kuna vitu viwili vinakuzuia usipate kile unachotaka; Moja; hujakomaa na kitu hicho kwa muda mrefu kiasi cha kuweza kupata unachotaka, …

Laiti Ungelijua Hili

Rafiki yangu nikupendaye, Kila mmoja wetu kuna hali ya majuto fulani anayo ndani yake.Majuto haya tukiyafikiria, yanatufanya tuumie zaidi. Majuto haya yamekuja kwa sababu mbalimbali, labda pengine ulipaswa kuchukua hatua fulani na hukufanya hivyo.Labda ulipaswa usichukue hatua fulani na hukufanya hivyo. Kuna wakati tunawaahidi watu ambao tunahusiana nao kwamba tutawasaidia katika hitaji walilotuomba, na tuna …

Rudi Kwenye Mstari

Rafiki yangu nikupendaye, Kwenye maisha kuanguka siyo dhambi. Bali dhambi ni kubaki kwenye anguko.Ukishajikuta umeanguka kwenye kitu fulani, usione aibu kutoka, kwa sababu ujinga ni kuendelea kubaki. Sehemu yoyote ambayo umejikuta umeanguka, wahi haraka kurudi kwenye mstari. Kila mmoja wetu ana utashi wa kujua mema na mabaya.Kuna wakati unaweza kwenda ndivyo sivyo, hivyo unapojikuta katika …

Design a site like this with WordPress.com
Get started