Huyu Ndiyo Mtu Anayekuchelewesha

Kuna familia, jamii, taasisi na maeneo mengi yanashindwa kupiga hatua kwa sababu moja tu. Na sababu hiyo ni kukosa mtu wa kufanya maamuzi. Watu wengi hawaendi mbele au hawarudi nyuma kwa sababu ya kufanya maamuzi. Maendeleo ya mtu mmoja mmoja yanaamuliwa na maamuzi anayofanya mtu na hatua anazochukua. Watu wanaogopa kufanya maamuzi, kitu kinachopelekea watu …

Hujachelewa Bado

Pale tunapokuwa tumejua kitu kwa mara ya kwanza, huwa tunajihisi kama tumechelewa vile. Tunakuwa tunajilaumu kabisa nilikuwa wapi, ningekuwa nimejua haya mapema ningekuwa mbali. Katika hali ya kawaida unaweza kuona umechelewa. Lakini hujachelewa. Kwa sababu kwa sasa ndiyo muda wako mzuri wa kufanya kile ambacho umejua sasa. Wanasema miaka 20 iliyopita ndiyo ulikuwa muda mzuri …

Kile Kinachokupa Amani Kinalipa Bili ?

Watu wengi wanapenda kufanya kile wanachopenda. Na ni kweli kabisa, mtu anayefanya kazi anayoipenda huwa haoni kama ni kazi tena. Kama unataka kupata amani basi fanya kazi unayoipenda. Je, kama kwa sasa kile unachokipenda kufanya na hakikupatii fedha za kulipa bili unafanyaje? Jibu ni fanya kile usichopenda ili upate mahitaji.Pale unapopata pesa, na unajiweza kiuchumi …

Tatizo Ni Wewe

Huwa tunaajiri watu wa kutusaidia majukumu yetu. Kwa sababu peke yetu hatuwezi kufanya kila kitu.Umoja ni nguvu. Na kidole kimoja hakivunji chanya. Huwezi kupiga hatua kubwa kwenye maisha yako, kama unafanya kila kitu wewe. Lazima upate watu wa kukusaidia. Hata kama unajitegemea kiasi gani, kumbuka kujitegemea siyo kujitosheleza. Unapoajiri mtu, anakuwa hajui nini unataka wewe …

Kila Maamuzi Unayofanya Yana Vitu Hivi Viwili

Rafiki, Uko hapo ulipo kwa sababu mbili,Moja kwa maamuzi ambayo uliwahi kufanya huko nyumaNa mbili ni kwa sababu ya kushindwa kufanya maamuzi ambayo yamepelekea leo kuwa na maisha ambayo unayo sasa. Kwa kila maamuzi utakayofanya, jua kuna maumivu ndani yake. Hivyo basi, mara zote fanya maamuzi ambayo utakuwa tayari kuvumilia maumivu yake. Kila maamuzi unayofanya, …

Hakuna Kazi Ngumu Kama Hii

Waswahili wanasema ukiona vya elea, ujue vimeundwa.Matunda mazuri ambayo unayaona kwa mtu jua kuna kazi kubwa nyuma yake imefanyika. Ukiona mtoto wako anafanya vizuri katika masomo yake, jua kuna kazi ambayo imefanyika kwa wazazi wenyewe au walimu shuleni. Na kazi hiyo ni ufuatiliaji endelevu. Matokeo ya kitu chochote kile, hakiji mara moja, bali yanahitaji ufuatiliaji …

Ukitaka Kujiona Huna Maana Hapa Duniani

Njia rahisi ya kujiona kama vile huna maana hapa duniani ni kujifananisha wengine. Tunapoteza ubora wetu, pale tu tunapoanza kujilinganisha na wengine.Kila mtu ana upekee wake, hivyo kutaka mtu afanane na mwingine maana yake ni kutaka apoteze upekee wake na kuishi upekee wa mwingine. Jikubali vile ulivyo. Watu watakupenda na kukukubali vile ulivyo kwa sababu …

Majaribu Yanapimwa Na Hiki

Rafiki, Hakuna mtu ambaye yuko salama. Kila mtu anapimwa kulingana na kiwango cha imani yake. Majaribu mengi huwa yanapimwa kulingana na kiwango cha imani yetu.Majaribu yanakuja kupima kiwango cha imani yetu. Ubora wa mtu unaonekana wakati wa changamoto. Namna anavyozitatua kwa utulivu. Tuzipokee changamoto kadiri zinavyokuja na kuzitatua. Kwa sababu maisha yetu hapa duniani yapo …

Fanya Kazi Na Wateja Hawa

Rafiki, Siyo kila mteja ni mteja kwako.Kuna wateja wengine wanaweza kuja kwako lakini siyo sahihi. Na siku zote kwenye biashara na hata maisha kwa ujumla.Fanya kazi na kitu kinachofanya kazi tayari. Wateja wazuri ni wale ambao wana uwezo wa kumudu gharama ya kile unachouza.Usihangaike na wateja ambao hawana hela, ambao hawana uwezo wa kumudu gharama …

Kazana Kuwa Wewe

Huwezi kuona ladha ya maisha yako, kama kila siku unakazana kujikimbia. Ni ajabu mtu kuwasikiliza watu wengine lakini anashindwa hata kujisikiliza yeye mwenyewe. Ndani yako kuna maisha ambayo unayataka kuishi lakini unashindwa kuishi kwa nini? Kuna mambo ambayo unayafanya, unajua kabisa hayakupendezi, ila unafanya tu ili kuwafurahisha watu wengine. Mpaka unaondoka hapa duniani, hautakuja kufanikiwa …

Design a site like this with WordPress.com
Get started