Fanikiwa Kwenye Kile Unachotaka Kufanikiwa

Rafiki yangu nikupendaye, Fanikiwa kwenye kile unachotaka kufanikiwa. Inawezekana kabisa, ni wewe tu ndiyo unajizuia kupata kile unachotaka. Ukiamua unafanikiwa. Kama umeshajua kile unachotaka kwenye maisha yako, weka juhudi zaidi ili ukipate. Kinachowasumbua watu ni kwamba hawajajua wanataka nini, kama wewe umeshajua kile unachofanya, basi weka juhudi kukipata. Mwenye nia ya kutaka kitu, huwa hashindwi. …

Kama Bado Hujajipata

Rafiki yangu nikupendaye, Kama bado hujajipata, sema ndiyo kwa kila kitu. Unasema ndiyo kwa sababu unahitaji fursa ya koneksheni mbalimbali ili ujipate. Unasema ndiyo kwa mambo ambayo ni sahihi na yanayokupa mchongo fulani. Kama hujajipata kanuni ni moja tu mtumikie kafiri, upate unachotaka. Lakini kama umeshajipata sema hapana kwa kila kitu. Sema hapa kwa mambo …

Unawajibika Kwa Nani?

Rafiki yangu nikupendaye, Kwenye hii dunia lazima kila mtu awajibike kwa mtu fulani. Hakuna mtu ambaye hawajibiki kwa mtu fulani. Kwa sababu asili yetu sisi binadamu ni uvivu, bila kuwajibishana hakuna maendeleo yatakayotokea. Kwenye maeneo mengi ya maisha yetu, tunao mifano ya watu wengi ambao wanawajibishana. Kama unajikuta mvivu au huna nidhamu juu ya kitu …

Njia Bora Ya Kufanikiwa Zama Hizi

Rafiki yangu nikupendaye, Kwa zama tunazoishi huwezi kujisifia kwamba umesoma shule nzuri, ulienda chuo kizuri au una elimu nzuri kiasi gani. Watu kwa sasa wanahitaji kitu kimoja tu ambacho ni Onyesha kazi yako, SHOW YOUR WORK. Onyesha watu nini umefanya na siyo maneno ya nini unaweza kufanya na siyo ELIMU gani unayo. Hivi karibuni, nimeona …

Jinsi Ya Kujua Njaa Ya Watu Na Namna Ya Kuitibu

Rafiki yangu nikupendaye, Iko namna nzuri ya kuweza kuwashawishi watu WAKUBALIANE na wewe. Ni njia rahisi ambayo hutumii hata nguvu. Watu wa zama hizi wana NJAA, na NJAA hiyo waliyonayo siyo ya chakula bali ni kuthaminiwa. Watu wana NJAA ya kusifiwa,Unapokutana na watu, wasifie kweli, Sifia Uwezo Wake. Kila mtu anapenda kuonekana ni muhimu. Watu …

Ustaarabu Pekee Unaopaswa Kuwa Nao Zama Hizi

Rafiki yangu nikupendaye, Kadiri siku zinavyozidi kwenda, watu wanakuwa na mambo mengi na muda ni mchache wa kukamilisha yote.Kifupi hatuna muda wa kufanya kila kitu, ila tunao muda wa kufanya vitu muhimu tu. Watu wa zama hizi wanapoteza umakini. Kuna wakati tunashindwa kupata kile tunachotaka kwa sababu ya kukosa umakini wa ufuatiliaji. Zama hizi tunakabiliwa …

Huwezi Kukwepa Matokeo Ya Kitu Hiki

Rafiki yangu nikupendaye, Ni rahisi kukwepa majukumu yako lakini ni ngumu kukwepa matokeo yake. Kwa mfano, unaweza kuwa mvivu kwenye majukumu yako ya kazi lakini kamwe huwezi kukwepa matokeo yake. Yote tunayoyapata kwenye maisha ni matokeo ya juhudi ambazo tumeziweka. Maisha huwa yanamwadhibu mtu kulingana na juhudi anazoweka.Ukiweka kazi utapata matokeo mazuri yanayoendana na wewe. …

Tafuta Kitu Kinachokupa Sababu

Rafiki yangu nikupendaye, Sisi binadamu tuna asili ya uvivu ndani yetu.Ili tuende mbele, tunahitaji kusukumwa. Watu wengi wanaofanya makubwa, huwa wana kitu kimoja ambacho kinawasukuma na kuwawajibisha juu ya kitu fulani. Mafanikio ni kuwajishana kwa sababu kwa asili yetu sisi binadamu bila kufanya hivyo ni ngumu watu kufanya. Timu yoyote ya mpira, huwa inakusukumwa na …

Ukitaka Usiahirishe Kitu

Huwa tunapoianza siku yetu huwa tuna nguvu ya kutosha.Ni kama vile unapoamka simu yako inakuwa ni ina chaji fuli. Kama unataka usiahirishe kitu, jambo lako la kwanza na la muhimu, anza nalo pale tu unapoamka. Ni rahisi sana kuahirisha kama ukifanya jambo lako usiku.Kama unataka usiahirishe kitu, basi pale tu unapoamka na kuianza siku yako. …

Mauzo Yanashinda Kila Kitu

Rafiki, Kama kuna kitu ambacho unataka kukifanikisha na bado hujafanya hivyo, basi wewe uza tu. Kwa sababu mauzo yanashinda kila tu nakuambia. Utaweza kupata kile unachotaka kwenye maisha yako, kama utaweza kuuza zaidi. Ni kupitia kuuza, ndiyo fedha inaingia kwenye mifuko yetu. Ukitaka maisha mazuri, utayapata kupitia kuuza.Kuuza ni taaluma moja ambayo ina hela sana. …

Design a site like this with WordPress.com
Get started