Hakuna Kitu Kirahisi Kufanya Kama Hiki

Habari ya leo mpendwa rafiki? Hongera sana kwa zawadi ya siku hii ya leo ni nafasi ya kipekee sana kwetu kwenda kufanya kile kilicho bora ili kupata matokeo bora. Kufanya na kuona ni vitu viwili tofauti kabisa kwani watu wengi wanavyoona watu wakifanya jambo fulani wanaona ni rahisi sana kufanya. Lakini ukiingia kufanya kazi kwa …

Hii Ndiyo Haki Yako Ya Msingi Unayopaswa Kuwa Nayo

Mpendwa rafiki, Kila mmoja wetu yuko duniani kwa sababu fulani. Kila mtu ana kitu cha kipekee ambacho mwingine hana. Swali la kujiuliza je umezaliwa kuvumilia maisha au kufurahia maisha? Watu wengi sana wamekuwa ni watu wa kuvumilia maisha badala ya kufurahia maisha. Shida zimetawala badala ya furaha, kazi wanazofanya watu wanazichukia licha tu zinawapatia kipato, …

Kama Unatamani Kuwa Mwema Anza Na Kufanya Kitu Hiki Kwanza

Anayesema hana dhambi ana jidanganya mwenyewe. Kila mtu anafanya makosa ila unapoona wewe huna makosa na wengine ndiyo wanamakosa huwezi kuwa na unyenyekevu wa kukubali na kutubu kuwa hata wewe unakosea. Kuna wengine wanajiona wao hawana dhambi na wengine ndiyo wanadhambi. Kadiri unavyojiona wewe unadhambi ndivyo unajitengenezea njia ya mtu kuwa mwema, kwani ujiona pia …

Ukiwa Na Kitu Hiki Tu,Umepata Vyote

Mfalme suleimani aliomba hekima tu lakini Mungu akampa vyote, kupitia hekima tunaweza kupata yote lakini ukikosa hekima umekosa maisha na matokeo utaona dunia ni chungu kwako. Hekima inatumika kile eneo la maisha yetu hivyo tunapokuwa na hekima tunaweza kutawala mambo yetu. Unaweza kuwa na kitu fulani lakini ukakosa hekima ya kukitumia kile kitu, je ukijiuliza …

Hii Ndiyo Siku Inayoonewa Na Kubebeshwa Mizigo Na Watu Wengi

Tunapochelewa kufanya maamuzi huwa mara nyingi tunakuja kupata hasara baadaye, watu wengi wameshazoea kutumia msemo huu laiti ningelijua ningelifanya yale maamuzi mapema na kwa sasa hivi ningekuwa mbali. Kila mmoja wetu hapa kuna mahali alishawahi kuchelewa kufanya maamuzi hivyo kilichofuata ni majuto tu. Hauna haja sasa ya kuendelea na kukumbuka nay ale makosa uliyofanya kwa …

Ukiambatana Na Huyu Lazima Utakua Mshindi Tu

Habari gani mpendwa rafiki? Mtoto mmoja alizaliwa msituni  katika nchi fulani, baada ya mzazi wake kukimbia makazi na familia yake kwa sababu ya vita. Hivyo ilivyotokea mlipuko wa bomu kule msituni yule mama alikimbia na kuondoka na watoto wakubwa na kumuacha yule mtoto mdogo kule msituni. Mtoto yule alikuwa ni mchanga sana kwani alikuwa na …

Chochote Tunachokitafuta Katika Maisha Yetu Kipo Hapa

Habari gani rafiki? Natumaini unaendelea vizuri sana. leo ni siku nyingine bora nay a kipekee sana kwetu, hakika sisi ni washindi na tumezaliwa kushinda ndiyo maana hata leo tunaendelea kuvuta pumzi. Kila mtu mmoja wetu kuna kitu anachotafuta hapa duniani je kile tunachokitafuta kinatoka wapi sasa? Chochote ambacho tunakitafuta yawe ni mafanikio au yawe ni …

Zawadi Muhimu Ya Kumpatia Mtu Aliyekuamini

Mpendwa rafiki? Kama ni sehemu ambayo mtu unatakiwa kumuonesha kuwa unaweza ni pale anapoamua kufanya maamuzi umfanyie kitu fulani. Sehemu ya kujiuza ni pale mtu anapoamua kukukabizi kazi yako kwa sababu tu amekuamini, ameacha watu wote na kuja kwako hivyo ni nafasi ya kipekee na wewe kumtendea haki. Watu wakikuamini hutakiwi kufanya kosa unatakiwa kufanya …

Kama Unataka Watu Wakupende Fanya Kitu Hiki Kimoja Tu

Tunaishi kadiri ya sheria ya asili hapa duniani. Unapokea kile unachotoa kwa wengine hivyo usitegemee kupokea kama hakuna unachotoa chochote. Tunapenda watu watufanyie vile tunavyotaka lakini sisi hatutaki kujifanyia sisi wenyewe vile tunavyotaka kufanyiwa. Hakuna mtu atakayeweza kuvutiwa na maisha yako kama wewe mwenyewe huyapendi na kuyajali maisha yako. unaweza ukamkuta mtu anakujali au kukupenda …

Chezea Vitu Vyote Kutoka Kwa Mtu Lakini Usichezee Kitu Hiki

Habari ya leo rafiki na mpendwa msomaji wa mtandao wa Kessy Deo? Natumaini uko vizuri na leo ni siku bora sana kwetu kwenda kufanya kile tulichopanga kufanya na kutegemea kupata matokeo bora sana. Kila mmoja wetu kula kile anachoamini kadiri ya imani yake. Mimi nina imani yangu na wewe unaimani yako. licha ya kila mtu …

Design a site like this with WordPress.com
Get started