Hawa Ndiyo Watu Watatu Wanaohusika Katika Maisha Ya Ndoa

Mpendwa rafiki yangu, Roma haikujengwa kwa siku moja vivyo hivyo tabia nzuri haijengwi kwa siku moja. Ili uwe na ndoa bora ni mchakato unatakiwa kufanya kila siku wala siyo cha siku moja. Huwezi ukachukua kipaza sauti na kusema kuwa mimi ndoa yangu ni bora haina matatizo. Kila ndoa ina changamoto yake, kila maisha uliyochagua kuishi …

Hii Ndiyo Dawa Ya Uvivu

Mpendwa rafiki yangu, Mtu mvivu ni sawa na mtu aliyepakwa kinyesi kila mtu anayepita au anayekaa naye karibu naye lazima atamkimbia kwa sababu ananuka. Hakuna mtu ambaye atapenda kukaa sehemu moja na mtu aliyepakwa kinyesi mwili mzima, wengi watamkimbia kwa sababu ananuka. Tukianzia hata katika vitabu vya kiroho mvivu amelaaniwa,kama umasikini unavyopigwa vita vivyo hivyo …

Hiki Ndiyo Kitu Ambacho Kinaweza Kukuongezea Au Kukupunguzia Heshima Yako

Mpendwa rafiki yangu, Kila taaluma ina uvaaji wake, kwa mfano ukiwaangalia tu madaktari wanavyovaa unapata picha na kujua wale ni madaktari kadiri ya vazi walilovaa. Siku hizi mavazi wanayovaa watu hayawauzi kadiri ya taaluma yao. Unaweza kukutana na mtu jinsi alivyovaa na kile anachokuambia haviendani kabisa. Watu wanakupima kwa mara ya kwanza wewe ni mtu …

Mambo Pekee Ambayo Huwezi Kuyafanya Kwenye Maisha Yako

Mpendwa rafiki, Dunia ya leo ina mambo mengi kiasi kwamba huwezi hata kuyamaliza hata ukipewa masaa 24 kwa siku huwezi kumaliza habari zote. Watu wanataka kukimbizana na kila kitu, wanataka kubadilisha kila kitu mwisho wa siku wanajikuta wanachoka na kushindwa kufanya kile wanachotaka kufanya. Katika maisha ya falsafa ya ustoa kuna mambo makuu mawili, kuna …

Haya Ndiyo Mahusiano Mzigo Katika Maisha Yako

Mpendwa rafiki  yangu, Kila mmoja wetu amezaliwa katika mahusiano hakuna mtu ambaye anaweza kujitokeza na kusema kuwa yeye hayuko katika mahusiano. Mahusiano yetu ya kwanza kabisa yanatoka kwa wazazi waliotuzaa, wazazi ndiyo watu kwanza katika maisha yetu kujitoa upendo wa usadaka bila kujibakiza ili sisi tuweze kuishi, tukifikiria fadhila walizotutendea wazazi hakuna hata mmoja wetu …

Hiki Ndiyo Chanzo Cha Matatizo Mengi

Mpendwa rafiki yangu, Ukichunguza karibu kila eneo la maisha yetu utagundua kuna kitu ambacho huwa kinatawala na kikikosekana maisha yetu yanakuwa ya hovyo sana. Ukiona mtu kachelewa kazini basi hapo ujue kuna kitu kimekosekana, ukiona mtu ameshindwa kujisimamia ujue hapo kuna kitu kimekosekana. Hicho kitu kimekuwa kinawaumiza sana watu wengi hususani katika karne hii ya …

Haya Ndiyo Mategemeo Makubwa Ambayo Wazazi Wanayaweka Kwa Watoto Wao

Mpendwa rafiki yangu, Wazazi wametumika kama daraja kwetu kuingia duniani, wao ndiyo walibeba dhamana ya maisha yetu kwa sababu kama wangependa kutufanya chochote wangeweza ila kwa upendo wao mimi na wewe leo tunaishi. Kuna nadharia hasi iliyojengeka kwa wazazi wengi juu ya watoto wao. Ukiwasikiliza wazazi wengi wanakuambia wanazaa ili watoto wao waje wawasaidie. Ni …

Hakuna Biashara Ngumu Kama Hii Katika Dunia Ya Leo

Mpendwa rafiki yangu, Nilipokuwa nasoma kitabu cha mwalimu Julius Kambarage Nyerere kiitwacho binadamu na maendeleo nilijifunza mambo mengi sana. Natumaini kila mmoja wetu anajua Mwalimu Nyerere alikuwa ni nani katika nchi yetu ya Tanzania. Kupitia kitabu chake cha binadamu na maendeleo amegusia maeneo mbalimbali likiwemo eneo la serikali. Hivyo nakushirikisha kile nilichojifunza kupitia kitabu hiki …

Neno Litakalokusaidia Kuwa Na Nidhamu Ya Fedha

Mpendwa rafiki yangu, Unaweza kuwa mkusanyaji mzuri wa fedha lakini kama huna nidhamu ya fedha bado utakuwa unashida kubwa sana. Tajiri mmoja sehemu fulani aliwakuta vijana wamekaa bar wanakunywa na kula nyama choma, yule tajiri akawauliza mbona mnatumia kiasi kikubwa sana cha pesa, je ni nani leo kati yenu amezalisha kiasi cha elfu 30 hakuna …

Kama Unamiliki Kitu Chochote Jiandae Na Hili Kisaikolojia

Mpendwa rafiki yangu, Tunaweka juhudi kweli za kutafuta ila tunapaswa kujua asili ya dunia jinsi ilivyo. Wengi tunapopata mali au chochote kile tunakuwa tunaweka mioyo yetu yote pale kiasi kwamba mali zinakuwa zinatutawala badala ya sisi kuzitawala mali. Wako wengine wanaokosa hata usingizi wakifikiria mali zao na vitu vingine vinavyohusiana na hivyo. Iko hivi rafiki, …

Design a site like this with WordPress.com
Get started