Haya Ndiyo Malengo Ambayo Unapaswa Kujiwekea

Kila mmoja wetu ana malengo yake ambayo anayafanyia kazi kila kukicha. Bila kuwa na malengo tunakuwa hatuna tofauti na wanyama lakini sisi ni binadamu tunayo akili inayotuongoza kufanyia kazi malengo yetu. Haya malengo ambayo watu wanajiwekea huwa muda mwingine yanakuwa yanawaletea watu maumivu na hata kukatisha tamaa kabisa. Na miongoni mwa malengo ambayo yanawakatisha watu …

Hiki Ndiyo Kitu Kinachotibu Mahusiano Yetu

Rafiki yangu, Yako mambo mengi ambayo yanajenga sana mahusiano yetu. Na moja ya mambo hayo ni kama vile muda. Mahusiano yetu yanakuwa yana njaa kama hayana muda. Katika karne ya sasa mahusiano mengi yanalia kwa sababu ya njaa. Watoto wanalia njaa ya kukosa kupewa muda wa pamoja na wazazi. Wanandoa wananjaa ya kutopeana muda, kila …

Hiki Ndiyo Kitu Ambacho Huwezi Kumzuia Mtu Kusema Juu Yako

Huwezi kuwapangia watu waseme nini juu yako. Huwezi kuwazuia watu kuongea. Huwa tunapata shida kufikiria watu wanatusemaje kwani haya ni mambo ambayo yako nje ya uwezo wako. Watu wanaweza kuongea lolote juu yako aidha uwe unataka au la. Hutakiwi kujipa mawazo je watu wanakusemaje bali unatakiwa kuishi maisha ya uaminifu. Wewe fanya kile ambacho unaona …

Kitu Pekee Ambacho Unapaswa Kuchelewa Kukifanya Kwenye Maisha Yako

Mpendwa rafiki yangu, Huwa tunaambiwa kuwa tusichelewe kufanya yale tunayoweza kufanya katika maisha yetu. Kuna vitu ambavyo hutakiwi kuchelewa kuvifanya kabisa maana muda wetu ni mfupi sana kama vile kuchelewa kuandaa maisha mapema kabla hujazeeka. Watu wanapoteza muda wanafikiri kuwa watabakia hivyo hivyo milele wakiwa na muda na nguvu. Wanachelewa kufanya makubwa kwenye maisha yao …

Jinsi Ya Kukutana Na Bahati Kwenye Jambo Lolote Kwenye Maisha Yako

Kila mtu ana bahati katika hii dunia, kama tu uko hai ni kiashiria kizuri kuwa una bahati. Kwani kitendo cha kuendelea kuvuta pumzi ni bahati sana na siyo kwamba sisi tuna stahili sana. Wanasema hivi kuwa bahati ni pale fursa inapokutana na maandalizi. Unaweza kuwaona watu fulani wana bahati sana kwenye maisha yako kumbe basi …

Usiseme Hali Ni Nguvu Siku Hizi

Rafiki yangu, Kama huna tatizo unalotatua ni rahisi sana kusema hali ngumu siku hizi. Dunia haijawahi kubadilika hivyo kama hali ni ngumu sasa hivi vipi kipindi cha nyuma mbona hukiweka vizuri ili sasa usipate shida? Utamkuta mtu anakuambia awamu hii vyuma vimekaza, je kipindi cha nyuma hali ilikuwaje? Ina maana watu walikuwa wanapata mafanikio kirahisi? …

Huu Ndiyo Ukweli Unaofichwa Kwenye Kilevi

Rafiki yangu, Natumaini umeshawahi kuona au kusikia mtu akilewa baada ya kutumia kilevi huwa anaongea vile anavyojua yeye kadiri ya kilevi kinavyomtuma. Unaweza kujiuliza je yale maneno anayokuwa anayaongea mtu baada ya kulewa ni kweli au si kweli. Mtu anaweza kuwa mstaarabu sana pale anapokuwa hajanywa pombe lakini akinywa na kulewa ataanza kuongea vitu vya …

Jambo La Kuzingatia Pale Unapokuwa Unaongea Mbele Za Watu

Rafiki, Kila binadamu yuko katika sekta ya mauzo. Hivyo unapokuwa unaongea mbele ya watu unakuwa unauza mawazo yako kwa wengine. Kila mmoja wetu ana kitu ndani yake, hivyo tunatumia mauzo kama sehemu ya kuweza kuwauzia wenzetu kile ambacho tunacho ndani yetu. Unapoamka mpaka unaporudi kulala, unakua unafikiria mauzo, ufanye nini ili uweze kuuza na kupata …

Hii Ndiyo Faida Ya kuwa Mwaminifu Kwenye Kile Unachofanya

Mpendwa rafiki yangu, Sisi binadamu tunatabia ya kuwa wanafiki, kuna watu tukiwa nao tunajifanya waaminifu na watu wema. Lakini kuna watu tukikutana nao wala hatuwapi heshima kama tuliyokuwa tunawapa watu wa mwanzo. Huu ni ukinyonga sasa, kwanini mtu mmoja uwe na badilika? Rafiki, kama umeamua kuwa mwema basi kuwa mwema kwa watu wote, na wala …

Njia Bora Ya Kutokuangushwa Na Watu Kwenye Suala La Fedha

Rafiki, Fedha ni jawabu la mambo yote. Ni muhimu katika maisha yetu ya kila siku. Hakuna ubishi juu ya fedha kama ni muhimu au la. Fedha ndiyo inalipa bili katika maisha yetu hivyo ukisema fedha siyo muhimu huenda akili yako haiko sawa. Njia bora ya Kutokuangushwa na watu katika suala la fedha ni kutotegemea fedha …

Design a site like this with WordPress.com
Get started