Mtu Huyu Akikuita Acha Kile Unachofanya Nenda Kamsikilize

Kuna watu wawili muhimu sana hapa duniani. Hao ni watu ambao wanafanya maisha yetu ya kila siku yaende. Siyo kwamba watu wengine siyo muhimu hapana, kila mtu ana umuhimu wake. Kuna watu ambao wakikuita tu, unatakiwa kuacha mara moja kufanya kile ulichokuwa unafanya na kwenda kuwasikiliza. Watu hao ni bosi au mteja wako. Bosi na …

Hii Ndiyo Raha Ya Kuanza Kile Ulichopanga Kufanya

Tumekuwa ni watu wa kuweka malengo lakini siyo watu wa kufanya. Kama ungekuwa unaweka kazi kwenye kile ulichopanga kufanya leo hii ungekuwa mbali sana. Huenda ukawa unajilaumu muda huu kwa kujiambia laiti ningelijua. Lakini laiti ningelijua haina msaada wowote kwako, kitu pekee cha kufanya ni kufanya maamuzi ya kuanza upya pale ulipokosea. Kuna raha kubwa …

Jinsi Mabadiliko Yanavyokuua

Leo asubuhi nilivyokuwa nasoma kwenye kitabu 5 ZA MAJUMA 50 YA MWAKA nilikutana na tafakari ya kufikirisha kutoka kwa Ray Norda. Ray Norda anasema, sababisha mabadiliko na ongoza mabadiliko.Kubali mabadiliko na utapona kwenye mabadiliko hayo.Kataa mabadiliko au yapinge mabadiliko na mabadiliko yatakuua na kukupoteza kabisa. Mwandishi wa kitabu cha 5 Za Majuma 50 YA MWAKA …

Kabla Hujalala Leo Usiku Jiulize Swali Hili

Watu wengi huwa hawapendi kujifanyia tathimini binafsi je ulishawahi kujiuliza ni kwanini? Kwa sababu, watu wengi hawapendi kujua ukweli. Wanapenda waendelee kujidanganya kwa kujikimbia kila siku. Ukiwa unajifanyia thathimini lazima utakua unajua ni wapi unaenda? Ni bora ujifanyie tathimini halafu ukaujua ukweli. Ukishajua jua ukweli utakusaidia sana kwenye safari ya maisha yako hapa duniani. Watu …

Changamoto Kubwa Ya Mafanikio Iko Hapa

Kila mmoja wetu ana maana tofauti tofauti ya mafanikio. Kila mmoja anapenda kufanikiwa kwenye kile alichopanga kufanikiwa. Leo ni tarehe 4 Januari , huenda umeshaweka malengo yako na mipango yako mbalimbali. Hivi tarehe 4 Disemba utakua bado umesimama kwenye malengo uliyojiwekea? Au utakua umeshaachana nayo? Kumbuka mipango siyo matumizi. Siyo kila kitu kitaenda kama ulivyopanga. …

Hivi Ndivyo Familia Yako Inapaswa Kuwa Mwaka 2021

Kila mmoja wetu ametokea katika familia. Ni nani kati yetu ambaye hajatokea katika familia? Unafikiri ni kwanini kila mtu anatokea katika familia? Kwa sababu ni mpango wa Mungu kila mmoja wetu kutokea katika familia. Lakini sasa, watu wengi hawauenzi mpango huu wa Mungu kiuaminifu. Familia ndiyo mlango mkuu wa maadili duniani. Familia ikioza na jamii …

Huu Ndiyo Mtaji Ambao Tayari Unao Wa Kuongeza Kipato Chako

Aliyekuwa kiongozi wa kanisa katoliki duniani, Papa John Paul wa pili, enzi za uhai wake aliwahi kunukuliwa akisema,"Hakuna mtu ambaye ni masikini sana ambaye hana kitu cha kutoa, na hakuna mtu ambaye ni tajiri sana ambaye hana kitu cha kupokea" Kwanza kabisa, nikupe siri moja ambayo ulikuwa huijui, duniani hakuna mtu masikini bali kuna akili …

Haya Ndiyo Maamuzi Mazuri Ya Kufanya Na Kuyaepuka mwaka 2021

Heri ya mwaka mpya 2021,Kama hakuna mabadiliko ya kweli yanayotoka ndani, basi mwaka mpya utabaki kuwa kwenye kalenda lakini siyo kwako. Hivi ulishawahi kujiuliza ni kwanini wakurugenzi yaani CEO, mameneja kwenye kampuni au taasisi wanalipwa kiasi kikubwa cha fedha? Lakini kazi kubwa inafanywa na watu wa chini? Iko siri inayowafanya walipwe zaidi. Na siri hiyo …

Orodha Ya Vitabu Nitakavyosoma Mwaka 2021 Kuanzia Mwezi Januari Mpaka Juni

Habari rafiki yangu, Leo nilipata muda wa kutafakari maendeleo yangu binafsi kwenye nyanja mbalimbali.Nimetafakari mwaka 2020 umekuwa ni mwaka gani kwangu, umenipa somo gani na kupanga mipango ya mwaka 2021.Ila Mimi mwaka mpya 2020/2021 nilishaunza tangu mwezi novemba pamoja na wanamafanikio wote wa kisima cha maarifa. Nimeamua kuvisoma upya baadhi ya vitabu vya nakala ngumu …

Acha Kukimbizana Na Kila Kitu

Hakuna mtu ambaye amebobea kwenye kila kitu. Kila mbobezi amebobea kwenye kitu kimoja tu. Daktari bingwa wa moyo, hawezi kuwa mbobezi kwenye macho wakati huo huo. Unapoamua kubobea unapaswa kuchagua kitu unachopenda na kufanya na kuwa vile unavyotaka kuwa. Sasa iweje wewe unataka kuwa kila kitu? Unataka kufanya kila kitu peke yako, wewe ni nani? …

Design a site like this with WordPress.com
Get started