Maswali Mawili Yanayochokoza Fikra Za Uvumbuzi

Dunia isingekuwa hivi ilivyo leo kama watu wasingekuwa wanafanya uvumbuzi. Dunia inazidi kuwa bora kwa sababu watu wanazidi kuvumbua vitu vipya kila siku. Uvumbuzi unasaidia maisha ya watu kuwa bora. Leo nimekuandalia maswali mawili yanayokwenda kuchokoza fikra za kivumbuzi ndani yako. Swali namba moja, Kwa nini. Kila unapokutana na kitu mbele yako jiulize kwa nini.Ukiwa …

Kitu Kimoja Cha kujifunza kutoka kwa Leonard Da Vinci

Yako mambo mengi tunayoweza kujifunza kutoka kwa Leonard Da Vinci. Leonard alikuwa ni mtu wa subira. Alikuwa si mtu wa kuharakisha kufanya kazi zake bali alijipa muda kutosha katika kufanya kazi zake na hilo lilimwezesha kuzalisha matokeo makubwa. Watu wamekosa subira karibu kwenye kila eneo la maisha. Watu wamekosa subira kwenye eneo akili. Wanataka kusoma …

Tumia Kila Fursa Kuyafurahia Maisha

"Siku moja mwandishi Robin Sharma alikuwa Dubai akitoa mafunzo kwa wakurugenzi wa makampuni. Sasa wakati yuko kwenye lifti alikutana na mtu aliyevaa kofia aliyoipenda sana. Ndani yake akasukumwa na kumsifia mtu huyo, lakini akasita kwa kuona huenda mtu huyo asilipokee hilo vizuri. Lakini, akajiambia, ni bora tu aseme, maana hatari kubwa kwenye maisha ni kutochukua …

Mbinu Ya Kufanya Makubwa Kwenye Maisha Yako

Kama unataka kufanya makubwa kwenye maisha, geuza kila maumivu unayopitia au uliyopitia kuwa mwalimu wako. Yatumie maumivu unayokutana nayo kama sababu ya kufanya makubwa. Kwa mfano, kama unateseka katika nyumba za kupanga tumia maumivu hayo kama msukumo wa kujenga nyumba yako.Kama unapata shida kwenye usafiri wa umma, tumia hayo maumivu kupata usafiri wako binafsi. Mateso …

Njia Rahisi Ya Kubadili Fikra Zako

Mwanasaikolojia mmoja amewahi kusema ni rahisi kubadili fikra zako kwa kuchukua hatua kuliko kubadili hatua zako kwa kufikiri. Huwa tunataka kubadili maisha yetu kwa kufikiri kumbe siyo sawa. Unapochukua hatua unakuwa siyo yule wa mwanzo tena. Kwa mfano, unasema unataka kuanza biashara kila siku na huanzi, unalalamika mtaji unakusumbua ambao ndiyo umekuwa wimbo wa watu …

Kuna Mtu Anakutegemea, Endelea Kufanya

Kila mmoja wetu ana upekee wake. Hata mtu akufananishe na mtu mwingine bado utabaki kuwa wewe. Tena watasema uko kama fulani lakini siyo. Ndiyo maana katika maisha yako, furahia kuwa wewe maana kila mtu ana hadithi yake ambayo mtu mwingine hana. Endelea kuishi vile unavyoishi, endelea kufanya yale unayofanya kwa sababu kuna watu wananufaika na …

Design a site like this with WordPress.com
Get started