Siku Zote Huwezi Kupata Ukinzani Kwenye Vitu Kama Hivi

Ulishawahi kuona mtu anapata ukinzani kwenye kuangalia TV, kutembelea mitandao ya kijamii, ulevi, na mengine mengi yanayofanana na hayo? Mara nyingi tunashindwa kufanya vitu vigumu kwa sababu vitu vigumu huwa vinadai kazi. Tunapata ukinzani kwenye kazi tu kwa sababu kazi siyo rahisi huwa inahitaji kazi kufanyika. Ndiyo maana ni rahisi kuahirisha kazi na kupata ukinzani …

Tumia Mbinu Hii Pale Unaposhindwa Mapambano

Hakuna mtu ambaye hashindwi katika maisha yake. Kila mtu anaanguka na hakuna ubaya katika kuanguka bali kuendelea kubaki chini ndiyo kuna ubaya. Changamoto siyo mwisho wa maisha, tunapitia mapito kwa muda baada ya hapo maisha yanaendelea. Kwa mfano, tunapatwa na msiba, tunapitia kipindi cha majonzi na baada ya muda maisha yanarudi kawaida. Moja ya nukuu …

Usianike Mambo Yako Kwa Kila Mtu

Binadamu sisi tunatabia moja, ambayo ni kupenda kujua kila kitu kuhusu mtu na hii ndiyo maana tabia ya umbea huwa haikomi. Ukiruhusu watu wajue kila kitu kuhusu wewe utashangaa unaibua wivu na watu ambao mlikuwa mnaheshimiana tu. Wivu huwa unatabia ya kuzaa kila aina ya chuki unayoijua wewe. Watu wakishajua sana mambo yako kuna haya, …

Kama Huna Cha Kufanya, Fanya Hiki

Hakuna watu wanaotujua vizuri zaidi ya sisi wenyewe. Tumekuwa ni viumbe wa kutafuta sababu, kujipiga “saundi” sisi wenyewe pale tu tunapotaka kuahirisha mambo. Kwa mtu ambaye uko hai na mwili wako uko kwenye mwendo kusema huna cha kufanya ni dhambi na ni uvivu mbaya sana.Mtu makini na mwenye thamani atakosaje cha kufanya? Kama huna cha …

Hii Ndiyo Bidhaa Yenye Soko

Karne ya 21 imepoteza bidhaa moja muhimu sana. licha ya watu kufanya kazi, biashara lakini ndani yao hawana, hawauzi bidhaa yenye soko na inayofanya vizuri sokoni. Watu wanapewa kazi lakini wanashindwa kuuza ile bidhaa ambayo inatakiwa na dunia. Tumekuwa tunauza vile tunavyojua sisi ndiyo maana dunia huwa inatupa kile tusichotaka kwa sababu ya kushindwa kuuza …

Hii Ndiyo Kazi Kubwa Ya Wanafalsafa

Sisi binadamu tumekuwa tuna udhaifu sana katika kufanya maamuzi. Tumekuwa tunaongozwa zaidi na hisia kuliko kufikiri kwa akili. Tafiti zinaonesha kuwa hata maamuzi mengi yanayofanywa kila siku watu wanayafanya kwa kutumia hisia na mara nyingi maamuzi ya hisia tunayofanya yanakuja na gharama kubwa baadaye. Huwa tunawaamini sana wataalamu tunapotaka kufanya maamuzi tena eneo ambalo sisi …

Kitu Kinachopatikana Kwa Urahisi

Kama kuna kitu huwa unakipata kiurahisi basi jua thamani yake ni ndogo. Kitu chochote kinachopatikana kwa urahisi thamani yake ni ndogo. Ila kinachopatikana kwa shida thamani yake ni kubwa. Kwa mfano, sukari kwa sasa imekuwa adimu hivyo inapelekea kuwa na thamani kubwa. Ukilinganisha chumvi na sukari utaona kuwa chumvi inapatikana kwa urahisi na wala hujawahi …

Njia Ya Kupata Vitu Vyote Vizuri Duniani

Hivi unaweza kaa chini na kuweka mipango ya kupata vitu vibaya? Vitu vibaya vinakuja vyenyewe pasipo kutafutwa kwa sababu yule anaye tafuta vitu vizuri anavipata lakini yule ambaye hatafuti vizuri havipati kweli anaishia kupata vibaya. Kila kiumbe kinapambana kutafuta kitu kizuri, kwa sababu kitu kizuri kinakuwa kinampa mtu kile ambacho moyo wake unataka. Vitu vizuri …

Hiki Ndicho Kinachogundua Ukweli

Hakuna hata mmoja wetu anayeweza kuhodhi ukweli, yaani kuumiliki na kusema ni wake hivyo aufiche. Ukweli haufichiki, ukweli uko kama moshi, unapika ndani moshi unatoka nje. Tunaweza kuuficha kwa muda tu lakini yuko bwana mmoja anayefichua na kugundua ukweli wote tunaoficha.Anayeweza kuufichua ukweli wa mambo au jambo lolote lile ni muda. Muda unaponya kila kitu …

Uchambuzi Wa Kitabu; UMEIWEKA WAPI TALANTA YAKO? Je umejiajiri, umeajiriwa au huna ajira?

Kitabu hiki kimeandikwa na Albert Nyaluke Sanga na kuchambuliwa na mwandishi Mwl. Deogratius Kessy Mwandishi anaanza na kusema ;πŸ‘‰Ajira zinafanana na kuweka fedha benki. Unapochukua talanta zako yaani fedha na kwenda kuziweka benki kwa muda maalumu , tafsiri yake ni kwamba unasema, jamani eeh, mwenzenu nina talanta (fedha) hapa lakini sielewi nitazifanyia nini kwa muda …

Design a site like this with WordPress.com
Get started