Dakika Kumi Na Tano (15) Tu Zinakutosha Kufanya Kitu Hiki Hapa

Hizi ni zama ambazo kila mtu yuko bize lakini ukipima matokeo hakuna kitu. Wimbo wa niko “bize” umekuwa unaimbwa karibu kila siku. Ukimwambia mtu afanye kitu fulani atakuambia sina muda yaani niko “bize”kweli.Ni rahisi kusema huna muda kama hujaupangilia muda wako vizuri. Kila dakika inayoenda lazima uwe umeipangilia kufanya kitu lakini unakuta watu wanasema hawana …

Hivi Ndiyo Vitu Ambavyo Haviwezi Kukuongezea Furaha

Vile ambavyo unaona kwa wengine ni bora na vya thamani siyo bora kama unavyofikiria. Huenda maisha yako ni bora kuliko kile ambacho unachotamani kwenye maisha ya wengine. Kununua vitu zaidi hakukuongezei furaha.Kwanini?Kwa sababu baada ya muda unazoea vile vitu ulivyonunua. Kwa mfano pata picha kwenye maisha yako, kuna vitu ulikuwa unavitamani ukaweka kazi na ukavipata …

Haya Ndiyo Mahusiano Yanayochosha

Ni yale ambayo upande mmoja unanyonya upande wa pili na kuutegemea kwa kila kitu. Mahusiano yasiyochosha ni yale ambayo kila mmoja anakuwa na kitu cha kutoa. Ukitaka mahusiano yaende vizuri, kila mtu awe na kitu cha kutoa. Kama uko kwenye mahusiano fulani halafu wewe unakuwa tegemezi basi anza kuchangia. Usipochangia utachokwa na utakua mzigo. Mama …

Usipokuwa Makini Huyu Hapa Atakunyang’anya Mafanikio Yako

Unyenyekevu ni mama wa fadhila zote. Mtu ambaye amekosa unyenyekevu katika maisha hawezi kufika mbali. Usipokuwa makini na kiburi utaanguka chini. Kiburi ndiyo kitu cha kwanza kinachowaangusha watu katika kile wanachokifanya. Iwe ni kipaji, kazi au biashara ukiwa umeweka kiburi tu kinakunyang’anya mafanikio uliyonayo. Hata ukifanikiwa kiasi gani, usiwe na majivuno au kiburi. Hivi ni …

Jinsi Ya Kufanya Pale Unapokutana Na Jambo Ambalo Hukutegemea Kutokea

Mwandishi Deepak Chopra anatuambia kwamba kwenye maisha hakuna ajali. Na hili ni kweli. Kila kinachotokea huwa kinakuja na kusudi ambalo sisi tunakuwa hatulijui ila asili inajua hilo. Kila kinachotokea kwenye maisha yako, iwe ni kizuri au kibaya, kaa ukijua kimekuja na kusudi fulani. Hivyo basi, badala ya kulia au kushangilia unahitaji kukaa chini na kujiuliza …

Furaha Ya Maisha Yako Inategemea Ubora Huu Hapa

Wewe ni kile unachofikiri. Wewe ni kile unachokula. Unakuwa vile unavyotaka kuwa kadiri unavyoitumia akili yako. Kile kinachoingia ndani ya akili yako ndicho kinachotoka. Je unaingiza vitu chanya? Kama jibu lako ni ndiyo basi hata kutoa utatoa kitu chanya. Usitegemee kupokea kile ambacho huna. Na hii ni sheria ya asili. Aliyekuwa mtawala wa Roma na …

Kwenye Kile Unachofanya Shabaha Yako Iwe Hapa

Kama unafanya kazi yoyote ile fokasi yako isiwe muda bali matokeo. Fokasi kwenye matokeo na siyo kwenye muda. Pima ufanisi wako wa kazi au wa kitu chochote kile unachofanya kwa kiasi gani umeweza kufanikiwa. Na siyo masaa mangapi uliyotumia kufanya kazi. Utawakuta watu wanajisifia muda waliofanya kazi badala ya kujisifia matokeo waliyozalisha. Kwenye kazi yoyote …

Ijue Methali Ya Kijapani

Wajapani wana methali yao inayosema kile ambacho hutaki kikutoe jasho ukiwa kijana, kitakuja kukutoa machozi ukiwa mzee. Hii ina maana gani kwetu?Maana kubwa ya kuondoka nayo hapa ni kwamba, ni rahisi kukwepa kile unachotakiwa kufanya sasa lakini kamwe matokeo yake huwezi kuyakwepa. Matokeo utayapata tu baadaye kama kwa sasa hutaki kulipia gharama kubwa. Usikwepe kile …

Ili Usiwapoteze Watoto Fanya Hiki

Ni zama za ajabu sana mtu unaweza kumaliza siku huna kikubwa ulichofanya pale unapojipima kwa matokeo uliyozalisha. Kuna wakati tunakuwa bize kiasi kwamba tunasahau majukumu ya kifamilia. Ni kweli lazima tujitume ili tuingize fedha ya kuendesha maisha. Ila siyo kila ubize unaleta matokeo chanya. Unapaswa kujichunguza uko bize kiasi gani kiasi kwamba unasahau kujua hata …

Vitu Viwili Vya Kuwa Navyo Kwenye Zama Hizi

Bilionea na mwekezaji Warren Buffet aliwahi kusema, uaminifu ni zawadi ya ghali sana, usitarajie kuipata kwa watu wa kawaida. Kwa zama hizi tunazoishi kuna vitu viwili vimekuwa adimu ambavyo huwezi kuvipata kwa kila mtu bali ni watu wachache tu. Navyo ni; Moja, uaminifu. Watu wengi siku hizi siyo waaminifu. Hata kama wewe ni mwaminifu kiasi …

Design a site like this with WordPress.com
Get started