Maisha Yangekuwaje Kama Kusingekuwa Na Kitu Hiki?

Pata picha kama kungekuwa na mtu ambaye hafi, anaweza kufanya kila kitu peke yake, yupo kila mahali. Huyo mtu angekuwa wa namna gani?Kwenye maisha, ukomo ndiyo unaleta ladha ya maisha. Hata uhai wetu una ukomo. Unapopata nafasi, unatakiwa kuishi vizuri kwa sababu unajua utakufa. Ukomo ndiyo unaleta maana ya kitu kwa sababu kitu chochote ambacho …

Kama Kitu Ni Kibaya Utajitajidi Kukiepuka

Kwenye jamii zetu, tumeaminishwa kwamba utajiri ni kitu kibaya. Matajiri ni watu wabaya ambao wao ndiyo wanafanya maisha ya wengine kuwa mabaya kwa sababu ya wao kumiliki vitu vingi. Tumeaminishwa kwamba umasikini ni kitu kizuri na utajiri kitu kibaya. Mtu anapokuwa, tayari anakuwa ameshajijengea mtazamo hasi juu utajiri na mafanikio kwa ujumla. Na kama kitu …

Kanuni Ya Kwanza Ya Fedha

Fedha ni jawabu la mambo yote hilo halina ubishi.Kila mmoja wetu anajua umuhimu wa fedha kwenye maisha yake. Ni kawaida matumizi kuongeza pale kipato kinapoongezeka. Usipokuwa makini na hili, utajikuta pale pale.Haijalishi unapata kiasi gani, unapaswa kuishi chini ya kipato chako. Na shule ya kwanza ya fedha ni matumizi yasizidi kipato.Hii ni kanuni ya msingi …

Jenga Kitu Hiki Muhimu Kwenye Maisha Yako

Kila mwaka watu huwa wanahangaika na njia mpya za mafanikio. Na kwa uhalisia hakuna njia mpya za mafanikio. Ili uweze kufanikiwa kwenye maisha yako, unapaswa kujenga kitu kimoja tu na kitu hicho ni tabia. Watu wengi wanataka kufanikiwa lakini wanakosa kitu kimoja tu ambacho ni tabia.Chochote kile ambacho unaona watu wanafanya, ni kwa sababu ni …

Huu Ndiyo Wakati Mzuri Wa Kubadili Mambo

Rafiki yangu nikupendaye, Kama kitu hakipo sahihi, kirekebishe kabla mambo hayajaharibika. Chukua hatua mapema, usisubiri mpaka mambo yaende ndivyo sivyo ndiyo uchukue hatua. Wakati mzuri wa kubadili mambo yaliyoharibika ni kabla hayajaharibika, na unaweza kufanya hivyo kwa kuchukua hatua kwenye mambo madogo ambayo hayana madhara na yanaweza kupuuzwa, lakini baadaye yanatengeneza madhara makubwa. Usifiche chochote …

Nguvu Ya Orodha

Bilionea Charlie Munger aliwahi kunukuliwa akisema, hakuna rubani makini, hata awe na kipaji na uzoefu kiasi gani, ambaye atapuuza nguvu ya orodha ya mambo ya kuzingatia.Kwenye kila kazi unayofanya, hakikisha unakuwa na nguvu ya orodha ya mambo ya kuzingatia.Ukiwa na orodha ya mambo ya kuzingatia, itakua kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa. Huwezi ukasahau, kwa sababu …

Hiki Ndiyo Chanzo Cha Hekima

Rafiki, Baba wa falsafa, mwanafalsa Socrates aliwahi kunukuliwa akisema, hekima pekee niliyonayo ni kwamba sijui kitu. Socrates ni mtu ambaye alikuwa anachukuliwa ni mtu mwenye hekima.Mtu anayejua lakini watu walishangaa pale alipoulizwa hekima yake na majibu aliyotoa. Pata picha, unaenda kwa mtaalamu wa kitu fulani halafu anakuambia, yeye anachojua ni kwamba hajui kitu utajisikiaje? Kujua …

Hii Ndiyo Dhambi Ambayo Hupati Raha Wakati Wa Kuifanya

Rafiki, Kuna watu huwa wanajisikia raha pale wanapoona wengine wakipitia magumu.Na hiyo ndiyo inakuwa furaha yao kuu. Na waswahili wanasema, Dua la kuku, halimpati mwewe.Ukiwa unawaombea wengine wapate mabaya, mabaya hayo hayawapati na huenda yakakurudia wewe mwenyewe. Dhambi ambayo watu wengi huwa hawapati raha wakati wa kuifanya ni wivu. Tukirejea kwa mtu mwenye hekima kutoka …

Kitu Ambacho Kila Mwajiri Huwa Anapenda

Kiasili kila mmoja wetu ni mwajiriwa, kama umeajiriwa utawajibika kwa bosi wako na kama umejiajiri utawajibika kwa mteja wako.Kila mtu anawajibika kwa mtu. Hakuna ambaye hawajibiki kwenye haya maisha. Iwe umejiajiri au umeajiriwa. Kitu ambacho kila mwajiri huwa anapenda sana ni mtu ambaye anaweza kutatua matatizo na siyo anayesababisha matatizo. Kama umeajiriwa, jitahidi sana kupunguza …

Sheria Tatu Za Kazi

Kama unataka kufanikiwa kwenye kazi au biashara unapaswa kufuata sheria ambazo zitakuongoza. Ukiwa na sheria, wewe ni kuzizingatia na ili kupata matokeo mazuri. Sheria tatu za kazi kadiri ya hekima ya Bilionea Charlie Munger ni kama ifuatavyo; Moja, usiuze kitu ambacho wewe mwenyewe haupo tayari kukinunua. Mbili, usimfanyie kazi mtu ambaye humheshimu na kumkubali. 3. …

Design a site like this with WordPress.com
Get started