Mambo Matano Muhimu Ya Kuzingatia Kwenye Maisha Yako

Rafiki yangu,Kwenye kitabu cha 12 Rules for Life mwandishi Jordan Peterson anatushirikisha mambo muhimu ya kuzingatia katika maisha yetu. Na baadhi ya mambo ambayo mwandishi anatushirikisha ni kama ifuatavyo; Sema ukweli. Nafikiri hili halina haja ya maelezo marefu, sema ukweli mara zote, usidanganye hata kama ni kitu kidogo kiasi gani, sema kweli na kweli itakuweka …

Huhitaji Kuwa Na Anasa

Kama bado hujafanikiwa kwenye maisha yako, huhitaji kuwa na anasa kwenye maisha yako. Kama huna fedha, huhitaji kuwa na anasa ya kuchagua kazi ya kufanya.Unapata wapi UJASIRI wa kuwa na maisha ya anasa wakati maisha yako bado hujayajenga? Kama bado hujafanikiwa huhitaji kuwa na demokrasia kwenye maisha yako.Nini ufanye na nini usifanye.Huhitaji kuwa na anasa …

Matatizo Mengi Ya Kifedha Yanaanzia Hapa

Ukiangalia matatizo mengi ya kifedha ambayo watu wengi wanakutana nayo, mengi yako chini ya milioni moja. Dharura za fedha nyingi katika jamii zetu huwa ni chini ya milioni moja. Hata watu wengi wanaingia kwenye madeni madogo madogo ni kwa sababu ya kukosa kiasi cha fedha cha milioni moja. Hivyo basi, ili kuepukana na mikopo midogo …

Usipofanya Hiki, Kuna Mtu Atakuja Kuchukua Nafasi Yako

Bilionea Mark Cuban aliwahi kunukuliwa akisema, fanya kazi kama vile kuna mtu atakuja kuchukua nafasi yako.Maisha ni vita. Nafasi yoyote uliyonayo, kuna mtu anaitamani. Usipoipambania, kuna mtu ataichukua. Biashara uliyonayo, kuna mtu anaitamani. Wateja ulionao kuna mtu anawatamani.Usiwahudumie vizuri, wataenda kwa mwingine.Kazi unayofanya, nafasi uliyopewa kuna mtu anaitamani. Anakusubiria tu wewe uzingue halafu achukue nafasi …

Ni Bora Kufanya Kuliko Kutokufanya

Makosa mabaya sana kwenye maisha yetu ni yale ambayo unajua nini cha kufanya lakini hufanyi. Ni mangapi ambayo unayajua kwenye maisha yako lakini huyafanyi? Ni bora kufanya hata kama utapata matokeo ya tofauti, kuliko kujua lakini hufanyi kile unachopaswa kufanya. Unapaswa kufanya kila unachojua ili uweze kupata matokeo mazuri. Ni dhambi kujua kitu halafu hufanyi. …

Kwenye Biashara Ya Kwako Ni Hii Tu

Watu huwa wanafikiria kwamba ukiwa na biashara basi kila kitu ni cha kwako na unaweza kufanya kile unachotaka. Unaweza kuwa mmiliki kweli lakini siyo kwamba unaweza ukafanya vile unavyotaka. Kwa sababu biashara ni kitu ambacho kinajitegemea chanyewe. Wale ambao wanafanya vile wanavyotaka huwa wanapata shida kubwa kwenye biashara. Watatumia mali za biashara vile wanavyotaka. Rafiki …

Epuka Kufanya Mambo Haya Ili Biashara Isife

Bilionea Charlie Munger aliwahi kunukuliwa akisema, ninachotaka kujua ni wapi nikienda nitakufa, ili niepuke kwenda hapo. Unapaswa kujiuliza kwenye biashara yako, ni kitu gani ukikifanya biashara yako itakuwa ili uepuke kufanya kitu hicho. Kuna mambo mengi ambayo unakuwa unafanya kwenye biashara yako ambayo yanasababisha biashara yako kufa. Kwa mfano, mauzo kidogo, kutokuwapigia wateja wako simu, …

Una Matarajio Gani?

Watu wengi kila wakati huwa wanapenda kuwa na matarajio makubwa kwenye kitu fulani. Ni jambo zuri kuwa na matarajio juu ya kitu fulani. Tunachokosea kwenye matarajio, ni kujiachilia kabisa kwenye matarajio hayo makubwa bila kujiandaa upande wa pili. Unapata kitu fulani, na unakuwa na matarajio, huo ni mchakato lakini kuwa na matarajio siyo kwamba dunia …

Hii Siyo “Levo” Yako

Kwenye maisha wale ambao tuko levo moja yaani kiwango kimoja cha maisha akifanya kitu huwa tunakuwa na wivu au kuumia. Lakini kitu hicho akifanya mtu ambaye tunajua siyo levo yetu huwa hata hatuumii. Pata picha raisi akipita mahali fulani na magari ya kifahari utamwonea wivu? Wala hutomwonea wivu. Unajua kwa nini? Kwa sababu, raisi siyo …

Usijiwekee Mipaka Ya Kitaaluma

Kama unataka kufanikiwa kwenye maisha, usikubali kubanwa na mipaka ya kitaaluma. Kuna watu ambao maisha yao yanabanwa na mipaka ya kitaaluma kiasi kwamba wanashindwa kwenye maeneo mengine ya maisha yao. Kwenye maisha unatakiwa kujifunza kile unachotaka kujua na siyo vinginevyo. Bilionea Charlie Munger,Aliwahi kunukuliwa akisema, sikuzingatia mipaka ya kitaaluma, badala yake nilijifunza kila nilichotaka kujua. …

Design a site like this with WordPress.com
Get started