Siyo Uhalisia

Rafiki, Huwa tunatengeneza hofu kisha hofu inatutengeneza.Tunatengeneza mazingira ya hofu ambayo yanakuwa kama breki kwetu. Hofu ni kitu ambacho hakipo katika uhalisia, hofu ni zao la akili ambalo tunalitengeneza sisi wenyewe. Tunatengeneza picha kwenye akili yetu ambayo kiuhalisia hata hicho kitu hakipo. Usiwe na hofu yoyote kwenye maisha yako, kama kitu kimepangwa kutokea kitatokea tu. …

Kila Mtu Anajali Maslahi Yake

Rafiki, Sisi binadamu kiasili kabisa ni wabinafsi. Kila mtu yuko hapa duniani kwa ajili ya maslahi yake. Watu huwa wanaangalia wanapata nini kwanza kisha ndiyo wafanye kile wanachofanya kufanya.Hata kwenye mauzo, watu hawezi kushawishika kuchukua hatua ya kununua kitu fulani kama hawana maslahi wanayoyapata kwenye kile wanachonunua. Usije ukawashangaa watu pale unapowaona wanashindwa kushawishika kuchukua …

Usiamini Katika Hili

Rafiki, Wako watu wanaamini kwamba maisha yao yatakuja kubadilika siku moja.Wengine wanamsemo wao kabisa wakisema, one day yes, wakiwa na maana kwamba siku moja watafanikwa yaani watatoboa. Watu wengi wanaamini katika bahati na siyo katika kazi. Ni kweli, bahati inahusika katika maisha lakini siyo kitu cha kutegemea kwenye maisha yako. Bahati siyo kitu cha uhakika …

Aina Mbaya Ya Kukata Tamaa

Kiasili kila binadamu huwa anakata tamaa katika hali fulani ya maisha yake.Kukata tamaa ni hali ya kutokuona tumaini fulani unalolitarajia kulipata kwenye maisha yako. Kutokuliona tumaini kwenye maisha yetu, ndiyo hali inayowafanya watu kushindwa kuendelea na kile wanachopaswa kufanya. Aina mbaya ya mtu kukata tamaa ni kukata tamaa kiroho. Mtu aliyekata tamaa kiroho, ni mtu …

Usitamani Haya Mafanikio Kabisa

Rafiki, Ni kawaida yetu sisi binadamu kutamani mafanikio ya watu wengine. Ni vizuri kutamani mafanikio siyo kitu kibaya.Lakini mafanikio huwa hayaji kwa kutamani bali kwa kuchukua hatua ya kufikia mafanikio makubwa unayotaka. Mafanikio ambayo sitaki uyatamani ni yale ambayo mtu tayari unayo. Badala ya kutamani matokeo ya mtu. Tamani mchakato mzima aliotumia kupata matokeo mazuri …

Siyo Kwamba Hujui, Tatizo Ni Hili Hapa

Rafiki yangu nikupendaye, Pata picha ukiangalia historia ya maisha yako, ulipotoka, ulipo na utakapoelekea ni jambo la kumshukuru Mungu sana kwa vile ulivyo sasa. Sina uhakika kama itakufaa lakini kwenye maisha yako, huenda ulikwama au unakwama kwa sababu ya kutokujua au kama unajua basi hujafanyia kazi yale unayojua.Na wanasheria nao wanasema, kutokujua sheria si utetezi …

Huwezi Kumpima Mtu Huyu Hapa

Kwenye maisha huwa tunaamini kwamba, pale unapokuwa na mtu karibu ndiyo unaweza kumjua kwa undani na hata kama unataka kumchunguza ni rahisi. Sina uhakika kama itakufaa lakini, huwezi kumpima mtu ambaye anajua anapimwa.Kama unataka mtu sahihi na mchunguze wakati yeye mwenyewe akiwa hajui kama anachunguzwa. Kwa mfano, kwenye usaili wa kazi, mtu anajua anapimwa hivyo …

Ifahamu Tabia Ya Watu

Asili ya binadamu ni kupenda matokeo na siyo sababu. Hata kama watu unaowataka wakupe matokeo lakini wanakupa sababu, usipowasimamia na kutaka matokeo, baadaye watakuja kukulaumu pia. Hata kama mtu yeye ni mvivu lakini licha ya uvivu wake, bado anapenda kuona matokeo mazuri. Wale ambao wako chini yako na unawasimamia kwenye kitu fulani, linapokuja kwenye suala …

Haya Mambo Mawili Ni Faya Kama Ukiyajua

Mwanamafanikio, Bado watu wanaamini kuwa mafanikio ni bahati. Ni kweli bahati inahusika kwenye maisha yako. Hata wewe kuwa hai ni bahati sana ambayo wengine wameikosa.Kwenye suala la mafanikio, bahati inatengenezwa. Bahati inakuja na maandalizi. Usitegemee bahati itakuja ukiwa umeweka mikono mifukoni. Kwa mfano, kwenye mchezo wa mpira wa miguu, kuna timu ambazo zinakuja kupata ushindi …

Ushindi wa Biashara Yoyote Ile Ni Huu Hapa

Rafiki, Wote tunajua kwamba kwenye kila mchezo huwa kuna timu. Timu ndiyo inaleta ushindi kwenye mchezo wowote. Kama unashabikia timu fulani ya mchezo, ukiona namna timu inavyocheza, unajiambia kabisa kwamba tunapata ushindi au hatupati ushindi. Wakati mwingine wewe kama shabiki, unasema kabisa hapa inabidi tubadilishe mchezaji au wachezaji fulani ili kuweza kupata ushindi. Kwenye biashara, …

Design a site like this with WordPress.com
Get started