Kitu Wanachotafuta Watu Wengi Kwenye Maisha

Tumetoka kwenye zama za nenda shule, soma kwa bidii, pata alama nzuri na utapata kazi ya uhakika. Kipindi cha nyuma, AJIRA kwa mtu aliyesoma ilikuwa ni kitu cha uhakika sana. Na watu walivutiwa na hilo kiasi cha watu wengi kupambana na wao wapate elimu nzuri ili wapate uhakika wa kazi. Kwenye jamii, mtu akienda kuajiriwa …

Sijui Hata Nitavaa Nguo Gani Leo?

Asubuhi ndiyo muda ambao unapaswa kuulinda kwa gharama kubwa. Ukipoteza mwanzo wa asubuhi yako maana yake umepoteza siku yako. Muda wa asubuhi siyo muda wa kupanga bali ni wa kufanya yale mambo ambayo ni muhimu tayari ulishapangilia tokea jana. Asubuhi ni muda wa utekelezaji na siyo kuanza kujiuliza nitafanya nini. Lala kabisa ukiwa unajua kesho …

Usipojitambua Unakuwa Mzigo Kwa Wengine

Rafiki, Kujitambua ni zawadi kutoka kwa Mungu. Siyo kila mtu amepata hiyo zawadi. Wako wengi mpaka sasa hawajapata zawadi hiyo na hawajui nini wanachopaswa kufanya kwenye maisha yao. Unapaswa kujitambua, kujua nini unachopaswa kufanya. Wewe kama baba au mama unapaswa kujua wajibu wako wa msingi ni upi na unapaswa kutekeleza majukumu yako ipasavyo bila kuambiwa. …

Kuwa Mtu Wa Kuchunguza

Rafiki yangu nikupendaye, Waswahili wanasema asiyejua maana haambiwi maana.Unapaswa kuwa na njaa ya kujua kile ambacho hukijui kwa sababu watu wanatumia ujinga wako kunufaika. Ukikaa na kuacha kujifunza, utakua mteja mzuri kwenye kila eneo la maisha yako. Badala hata wewe kuuza, utashangaa unaishia kuuziwa kila siku. Ukiwa unajua vitu vingi, utakua bora hata watu ambao …

Unahangaika Na Nini?

Rafiki yangu nikupendaye, Kwenye maisha wewe siyo kiranja wa dunia wa kutaka kuhangaika na kila kitu.Kazi yako moja ni kuhangaika na yale ambayo yako ndani ya uwezo wako. Hangaika na mambo ambayo yanafanya maisha yako yaende. Mambo ambayo yanakupa kipato na siyo kuwa kiranja wa dunia wa kutaka kuhangaika na kila kitu. Kwenye maisha unapaswa …

Wewe Ni Mkombozi Wa Wengine

Kila unapoamka, amka ukiwa na hamasa kubwa sana kwamba wewe ni mkombozi kupitia kile unachofanya, unapaswa uende ukakifanye, ili ukoe watu.Dunia inakusubiria wewe mkombozi kupitia kile unachofanya.Kwa chochote kile unachofanya, jua unafanya siyo tu kwa sababu yako wewe mwenyewe, bali kwa sababu ya wengine. Wewe ni mkombozi, watu wanakutegemea wewe ili maisha yao yaende. Usijichukulie …

Jinsi Ya Kuongeza Kipato Chako Mara Mbili

Rafiki,Chukua wastani wa kipato cha watu watano unaokaa nao muda mrefu na utapata kipato chako. Asilimia tisini ya mafanikio yako yanaamuliwa na watu unaokaa nao muda mrefu. Unajua ni kwa nini? Kwa sababu watu wenye mafanikio wanafikiri tofauti na watu wasiofanikiwa na wewe unafikiri kama wale wanaokuzunguka wanavyofikiri. Kama unataka kuongeza kipato chako mara mbili, …

Jifunze Namna Ya Kuishi Vizuri Zaidi

Mwanafalsa wa Ustoa Epictetus aliwahi kunukuliwa akisema,“Maisha ni sanaa ya kuishi, kila unavyoishi ndivyo unavyojifunza kuishi vizuri zaidi.” Hii ina maana kwamba, kila siku unapaswa kuwa na siku bora zaidi ya jana. Yaani siku zako mbili zisifanane kabisa.Kwa mfano, kila siku jioni kabla hujalala, pata muda wa kuitafakari siku yako. Kisha siku inayofuata unakwenda kuishi …

Athari Za Kutoeleweka Sehemu Moja

Jinsi unavyokuwa kwenye jambo fulani, ndivyo utakavyokuwa hata kwenye maeneo mengine. Kama unaonekana chenga sehemu hata sehemu watu watakuona chenga pia.Kwa namna unavyofanya vizuri kwenye kitu kimoja, hata maeneo mengine utafanya vizuri. Kwa sababu mazoea ya kufanya vizuri sehemu moja, yatasababisha kuathiri maeneo mengine. Hata watu wanakupima, kama wanakuona uko vizuri sehemu, wanaamini hata maeneo …

Jifunze Kujitofautisha

Kama unataka kuwa bora na kupata ushindi kwenye kila eneo la maisha yako, basi jifunze kujitofautisha na wengine. Huwezi ukapata matokeo mazuri kama wewe unafanya mambo yako kikawaida tu.Kujitofautisha kwa mtu, ndiyo kuna upekee wa mtu.Wanaofanya kile unachofanya wewe wako wengi, ili ulete upekee, lazima kwanza uwe tofauti. Mafanikio yako kwenye upekee, kuwa na upekee …

Design a site like this with WordPress.com
Get started