Utapata Nafasi Kulingana Na Hiki

Rafiki, Nafasi nyingi ambazo watu huwa wanapata ni kwa sababu ya nafasi zao. Yaani unapata nafasi kulingana na nafasi yako.Hakuna maneno zaidi. Nafasi yako ikoje? Watu wengi wanaopata nafasi mbalimbali ni kwa sababu wana nafasi hizo.Usitegemee kukutana na bahati kama hujatengeneza mazingira ya kukutana na bahati unayotaka. Tengeneza nafasi, ili upate nafasi kadiri ya nafasi …

Uzuri Wa Kazi Ya Mauzo

Rafiki, Kwenye maisha, kila kitu kinaamuliwa na mauzo.Na mauzo ndiyo kila kitu.Kwenye kila makubaliano unayofanya, maana yake mauzo yamefanyika. Ukitaka upate kile unachotaka au ulipwe kiasi gani, nenda kwenye mauzo. Mauzo ndiyo yanaamua wewe ulipwe kiasi gani. Njia rahisi ya kukuza kipato chako ni kupitia kuuza.Kwenye mauzo huwa hakuna kipato cha ukomo. Kama unataka fedha …

Epuka Kiburi Kwenye Safari Ya Mafanikio

Rafiki, Kuna hali fulani huwa tunakuwa nayo sisi binadamu. Pale tunapoanza kuona tayari unajua na unaweza kila kitu. Unaona hakuna mtu anayeweza kukushauri au kukufundisha chochote.Unakuwa na hali ya ujuaji mwingi na kupelekea kuwa na kiburi. Unaona wewe ndiyo unayeweza kila kitu na hakuna mwingine kama wewe. Ukiwa kwenye kilele cha mafanikio ni rahisi kuingiwa …

Kinachoua Mafanikio Yako

Rafiki, Kabla hujafanikiwa ulikuwa umejiwekea viwango vya juu na kuhakikisha unavifikia mara zote. Lakini baada ya kufanikiwa unaachana na viwango hivyo na kuruhusu mazoea. Mazoea yanaua mafanikio makubwa. Angalia watu ambao kabla ya kuingia kwenye mahusiano walikuwa makini kuhakikisha kila mmoja anajali maslahi yake. Watu wakishakuwa kwenye kilele cha mafanikio kwa muda, wanaanza kufanya mambo …

Hivi Ndivyo Unavyopaswa Kuwa

Rafiki, Maisha ni yako. Ishi vile utakavyo ili mradi usivunje sheria za asili, nchi na kanuni za maadili. Kundi linapokulazimisha uwe kama wao, kataa na baki kuwa wewe halisi, kuwa mkweli kwako. Siyo kosa lako kujikuta katika kundi fulani kwa sababu sisi binadamu ni viumbe vya kijamii, tunapenda kuwa ndani ya kundi.Lakini,kama umejitambua na kuona …

Mazuri Unayofanya Yanadumu Milele

Rafiki, Kuna mazuri mengi unayofanya na wakati mwingine unaweza kuona hakuna anayejali.Hata kama watu hawakuambii kuhusu mazuri unayofanya jua mazuri yako wanayaona na wananufaika nayo. Kuna wengine hata uwaguse vipi kamwe hawawezi kushukuru. Kuwa kama asili au Mungu anatufanyia mengi lakini siyo wote wanaomshukuru kwa mazuri hayo.Hata wewe unapaswa kulielewa hivyo. Ng'ombe wanazalisha maziwa kila …

Naomba Unisaidie Kitu Kidogo

Rafiki yangu nikupendaye, Sisi binadamu ni viumbe vya ushirikiano. Hakuna jeshi la mtu mmoja. Ili mambo yako yaende, yanahitaji watu wengine.Maisha ni watu. Hivyo tunaishi kwa ushirikiano. Ushindi au mafanikio unayoyatafuta kwenye maisha yako utayapata kutoka kwa wengine. Kuna vitu ambavyo wewe unavyo mwingine hana. Vivyo hivyo kwa mwingine. Mwingine ana kitu, ila hana fedha. …

Siri Kuu Ya Kufanya Makubwa

Rafiki, Kila mmoja wetu anapenda kufanya makubwa. Na wakati mwingine tunapokuwa tunaangalia makubwa waliyofanya wengine, tunaona na sisi hatuwezi kufanya. Lakini iko njia rahisi ya kufanya makubwa. Na siri kuu ya kufanya makubwa ni ; Moja ni kuwa na ndoto kubwa. Mbili ni anza kidogo. Na tatu chukua hatua. Acha kufikiria ukomo au unachokosa na …

Ondoa usumbufu Huu ili kupata Ufanisi Kwenye Kile Unachofanya

Rafiki, Tunaishi kwenye zama za usumbufu. Usipokuwa makini na zama hizi utajikuta unahangaikia vipaumbele vya wengine na kusahau vya kwako vile muhimu. Bila kuwa na mbinu sahihi za kuweka kujitawala na zama hizi utajikuta kila siku unapata ufanisi hafifu kwenye kile unachofanya. Watu hawapumziki wala hawafanyi kazi. Muda wa kazi watu wanawaza kupumzika na muda …

Design a site like this with WordPress.com
Get started