Sababu Inayowapelekea Watu Wengi Kufanikiwa

Rafiki, Kuna watu ambao wanakuwa kama wana "aleji" ya kufanikiwa kwenye maisha yao. Hata uwaoneshe ushuhuda, kwa kuwa hawataki bado wataendelea kushikilia msimamo wao. Kuna watu ambao wanapenda ushindi, wanapenda kufanikiwa kwenye kila wanalotaka. Na watu hawa kwa sababu wameamua kupata ushindi, lazima watatafuta sababu ya ushindi. Mtu akiamua kufanya jambo fulani, lazima atahakikisha anafanikiwa.Mtu …

Jinsi Ya Kupata Hamasa

Rafiki, Sisi binadamu ni watu ambao tuna uwezo mkubwa ndani yetu. Lakini uwezo huu, hauwezi kuonekana mpaka hamasa fulani iwepo. Hamasa huwa inawasukuma watu kufanya kinyume na mazoea yao. Ili uwe na hamasa, unahitaji kuwa na shauku. Shauku ndiyo mama wa hamasa. Watu ambao hawana shauku ya kile wanachofanya, wanakuwa wamepoa. Na ukipoa kwenye kile …

Jinsi Ya Kuepuka Kupata Matokeo Duni

Rafiki, Kila mmoja wetu anapenda kupata matokeo mazuri. Hakuna anayependa kupitia hali ya kupata matokeo duni hata siku moja. Lakini, kuna wakati sisi wenyewe huwa tunachangia kupata matokeo hayo duni. Tunachangiaje sisi wenyewe kupata matokeo duni? Ni kupita kukosa maandalizi mazuri juu ya kitu fulani.Maandalizi mazuri huwa yanazuia kupata matokeo mabaya. Mara zote pendelea kuwa …

Jinsi Ya Kufanya Yasiyowezekana

Rafiki, Kuna vitu ambavyo unataka kufanya kwenye maisha yako, lakini ukiangalia wanaokuzunguka hakuna aliyewahi kufanya. Na kama hiyo haitoshi, watu wanakuambia kabisa kwamba unachotaka kufanya hakiwezekani kabisa. Hapa ndipo ndoto za wengi zinapofia na wanarudi kuishi maisha ya kawaida. Usikubali ndoto yoyote uliyonayo ife kizembe kiasi hicho. Unachohitaji ni kuwa na imani isiyoyumbishwa juu ya …

Kumbuka

Rafiki,Watu walioshindwa wanapenda kuona na wengine nao wanashindwa. Watu wenye mtizamo hasi wanapenda kuona na wanaowazunguka nao wana mtizamo hasi. Kitu muhimu sana unachotakiwa kufanya ni kuepuka sana watu ambao wana mtizamo hasi. Maana watakurudisha nyuma na hutaweza kufanikiwa. Wakimbie haraka watu hawa. Unachotakiwa kufanya ni;Wakati wote kuwa chanya.Watu ambao wako chanya wanatengeneza nguvu chanya …

Heri Watu Wakuchukie Kuliko Kukupuuza

Chochote kile utakachofanya kwenye maisha yako, hutakosa watu ambao watakuchukia. Ukifanya mazuri au mabaya lazima utachukiwa.Ukifanya kitu ambacho ni cha tofauti kuliko wengine, wako ambao watakupongeza na wako ambao watakuchukia. Ukiwa na hela, ukipambana kufanya makubwa, wako watu ambao watakuchukia tu pasipo sababu. Sasa ipi bora, uchukiwe ukiwa nacho au upuuzwe ukiwa huna?Ni bora uchukiwe …

Sifa Moja Unayopaswa Kuwa Nayo

Rafiki, Kuna wakati mwingine hupati kile unachotaka kwa sababu tu ya sifa ulizokuwa nazo. Unaweza kuwa na sifa ambazo zikakusaidia kupata kitu fulani au kukosa kitu fulani. Mara zote unapaswa kujijengea sifa zinazo kufanya uaminike bila shaka, kiasi cha kupata dili nzuri. Sifa moja unayopaswa kuwa nayo ni; Uaminifu usiotiliwa shaka kwa mara zote kufanya …

Ikatae Hii Sauti

Rafiki, Ingekuwa ni mtu wa kupanga na kufanya basi suala la mafanikio kwako siyo shida kabisa. Kuna wakati unakosa ushindi kwa sababu tu ya kuahirisha yale uliyopanga kufanya. Na ya kitu kinachokuzuia usikamilishe uliyopanga ni ile sauti unayokuambia kwamba nitafanya baadaye. Wewe ni shahidi, umeshajiambia utafanya baadaye na hata hujakamilisha kufanya kile ulichopanga kufanya hiyo …

Yafanye Maisha Yako Kuwa Rahisi

Rafiki, Kiasili maisha tayari ni magumu, lakini sisi wenyewe ndiyo huwa tunafanya maisha kuwa magumu zaidi. Huwa tunakataa uhalisia wetu, na kuhangaika na mambo ambayo yako nje ya uwezo wetu kabisa. Pale tunapohangaika na mambo ambayo yako nje ya uwezo, tunajikuta tunajilaumu baadaye kwa sababu ya kushindwa au matokeo tunayopata. Hapa duniani, kuna mambo ya …

Ukiambiwa Maneno Haya Utajisikiaje?

Rafiki yangu nikupendaye, Kama leo utaambiwa una miezi sita tu ya kuishi, baada ya hapo utakufa, je vitu gani utabadili kwenye maisha yako? Je utaendelea kupoteza muda wako kuzurura kwenye mitandao au kufuatilia habari?Je utaendelea kusumbuka na mambo madogo madogo yasiyo na tija kwako? Je utaendelea kuahirisha yale ambayo umekuwa unasema utafanya kesho lakini hufanyi?Ni …

Design a site like this with WordPress.com
Get started