Hii Ndiyo Biashara Kichaa Inayowaumiza Watu Wengi

Rafiki,  kabla ya kuja kwa ajira watu walikuwa wanajitegemea wao wenyewe kwa kujifanyia shughuli zao kama vile kufanya biashara au kulima ili waweze kupata kipato. Tokea ajira au mfumo wa ajira uanzishwe mpaka sasa unazaidi ya miaka mia mbili lakini kabla ya hapo watu walikuwa wanaendesha maisha kawaida tu bila hata kutegemea ajira. Mapinduzi ya …

Njia Ya Kuwazuia Watu Kuongea Juu Ya Maisha Yako

Kitu ambacho huwezi kukizuia ni kuwazuia watu kuongea. Hata ufanye kitu gani kizuri lazima tu watu wataongea ndiyo maana hakuna kazi ngumu kama ya kumfurahisha kila mtu hapa duniani. Mtu pekee ambaye unaweza kumfurahisha basi ni wewe mwenye. Binadamu ni viumbe vya hisia na kila mmoja ana matatizo yake hivyo basi unachotakiwa kufanya popote pale …

Uaminifu Wa Kwanza Unaopaswa Kuwa nao

Kuna mambo ambayo ukifanya unakuwa  unajipunguzia heshima sana katika maisha yako. Mara nyingi watu wanajipunguzia heshima na kuonekana siyo watu makini kwenye kitu kimoja. Mtu yeyote anayekuwa mwaminifu katika kitu hicho huwa anaonekana amestarabika sana lakini katika jamii yetu ni watu adimu sana kuwapata. Watu huwa wanalalamika sana pale wanapokuwa wanakwenda sehemu na kukuta watu …

Chochote Unachofanya Fanya Kwa Sababu Hii Moja

Rafiki, Unapokuwa unafanya kitu chochote fanya kwa moyo lakini siyo kwa unafiki. Huenda kuna misaada unawasaidia wengine au kuna mtu unamsaidia kitu lakini ndani yako hupendi kufanya hivyo ila kwa nje unajionesha unapenda kufanya hivyo sasa huo ndiyo unafiki wenyewe. Au muda mwingine mtu anaweza kabisa kujua kitu fulani lakini ataweza kuja kwako na kujifanya …

Jinsi Ya Kupima Imani Yako Juu Ya Kitu Chochote Kile

Mpendwa rafiki na msomaji wa mtandao wa KESSY DEO, Kwanza imani haipimwi kwa mizani au kwa wiingi au kwa uchache kama ilivyo vitu vingine. Imani inapiwa kwa njia kuu mbili ya kwanza ni; Ukweli, unaweza kupima imani ya mtu fulani ni yakweli au la hivyo kupitia ukweli unaweza kupima imani lakini huwezi kuipima ndiyo maana …

Jinsi Ya Kupata Matokeo Tofauti

Mwanasayansi Albert Einstein aliwahi kusema ujinga ni kufanya kitu kwa mtindo ule ule na kutegemea kupata matokeo tofauti. Huenda unategemea kupata matokeo tofauti lakini kila siku utendaji wako wa kazi ni ule ule. Mfumo wa maisha yako ni ule, watu unakutana nao kila siku ni wale wale na hadithi mnazopiga kila siku ni zile zile. …

Faida Za Kumsomesha Mtoto Wako Shule Za Karibu

Mpendwa rafiki, Wazazi wengi wamekuwa wakiendeshwa na fasheni ya kuwapeleka watoto wadogo sana shule hii inawapelekea hata kudumaa katika ukuaji wao. Inawapelekea watoto kuchukia shule mapema hata hajafika madarasa ya kati kati. Kila mzazi anayesoma hapa hakuna aliyewahi kupelekwa shule akiwa na miezi sita, mwaka, miaka 2, 3,4,5 wengi walipelekwa wakiwa wanajitambua kabisa na walikuwa …

Hakuna Mtu Anayeweza Kuubeba Msalaba Wa Mtu Huyu Hapa

Habari Rafiki na msomaji wa mtandao wa KESSY DEO? hongera kwa zawadi ya siku hii ya leo na karibu sana tuweze kujifunza kile nilichokuandalia siku hii ya leo. Hakuna anayeweza kubeba msalaba wa mtu hata siku moja. Kila mmoja ana msalaba wake na unaweza kuona msalaba wa mwenzako ni mrahisi lakini akikupa kamwe huwezi kuubeba …

Haya Ndiyo Matokeo Ya Kile Unachokimbia Katika Maisha Yako

Mpendwa rafiki, Dunia huwa inaasili ya kumuadhibu kila mtu anayekwenda kinyume na sheria ya asili hapa duniani. Hilo halina ubishi, chochote ambacho unafanya kinyume na misingi ya kitu husika lazima utaadhibiwa tu, unaadhibiwa kwa kosa ulilofanya. Watu wamekuwa ni waajabu sana wanajaribu kukimbia matatizo yao huku wakijua wataendelea kubaki salama lakini asili ya dunia haiwezi …

Ufahamu Mradi Pekee Ambao Haujawahi Kutokea Hapa Duniani

Watu wanaopata shida hapa duniani ni wale wanaokimbia matatizo yao.  Watu wanakimbia matatizo yao badala ya kuyatatua , wanahangaika huku na huko kumtafuta nabii wa ukweli huku wakisahahu kuwa nabii wa ukweli ni yeye mwenyewe. Mbaya zaidi watu wanaopata shida sana katika jamii yetu siku hizi ni wale wanaosema uongo.  Ukisema uongo unatakiwa uwe unakumbuka …

Design a site like this with WordPress.com
Get started