Hizi Ndiyo Nyimbo Za Kusikiliza Pale Unapokuwa Na Huzuni

Mpendwa rafiki yangu, Kila mmoja wetu anapenda furaha na ndiyo maana  watu wengi wanaitafuta furaha kwa nguvu ila wengi furaha zao zimebebwa na vitu na siyo kutoka ndani. Sijui kama kuna mtu anaamka kitandani kila siku na kwenda kutafuta huzuni katika maisha yake. Akili za watu zinatafuta raha na furaha na wala siyo huzuni. Asili …

Jinsi Ya Kuvaa Baraka Zako Vizuri

Rafiki, Kila mtu ni zawadi hapa duniani na kama unajiona wewe siyo zawadi basi ungekuwa umeshakufa siku nyingi au usingezaliwa kabisa. Kuwa tu hai mpaka leo ni zawadi hivyo tumia zawadi ya uhai wako vizuri ili uweze kuacha alama hapa duniani. Tumezaliwa tayari tuna baraka sasa je unajua jinsi ya kuvaa baraka vizuri? Kuna wengine …

Vishinde Vitu Hivi Vitatu Na Maisha Yako Yatakuwa Bora Sana

Mpendwa rafiki, Heri ya mwezi disemba mwanamafaniko, Mafanikio ni kujua siri ya ndani ya mchezo na siyo ya nje. Ndani ya mchezo kuna mambo mengi unaweza kuona maisha ya mtu fulani kwa nje ni marahisi lakini hujui maisha yake ya ndani yakoje. Kuna siri kubwa sana ndani ya maisha ya mtu, maisha ni mchezo wa …

Huu Ndiyo Msamaha Adimu Kuwahi Kutokea Hapa Duniani

Mpendwa rafiki yangu, Hivi kuna mtu ambaye hakosei? Kila mtu anakosea na hivyo basi kama tunakosea pia kuna watu tunaowakwaza yale makosa yetu tunayofanya. Wako ambao wanajiona wao ni watakatifu ambao hawakosei lakini kama huwa tunakosea kwanini tunakuwa tunawahukumu wengine kama vile sisi hatufanyi makosa? Kila mmoja wetu anahitaji msamaha ili aweze kuachilia yote yaliyomo …

Jinsi Ya Kumshinda Goliati Wako

Mpendwa rafiki yangu, Unajua kwamba kila mtu ana goliati wake? Kuna hadithi moja kutoka katika kitabu cha Biblia inayomhusu goliati ambaye anasemekana alikuwa jitu la miraba minne. Na mwingine alikuwa ni daudi ambaye alikuwa ni kijana mdogo mchunga kondoo. Goliati ni mtu ambaye alikuwa anaogopeka sana na ili uweze kupambana naye ilikuwa inahitaji moyo kwa …

Usisahau Kutembea Na Fedha Hii Kule Unakokwenda

Mpendwa rafiki yangu, Hakuna mtu anayeamka na kujua kuwa leo anakwenda kukutana na changamoto gani huko mbeleni. Hatujui  hata dakika za mbele yetu nini kitatokea lakini nguvu yetu iko sasa na siyo wakati ujao.  Unaweza kujivunia kile ambacho unacho sasa na siyo kile ambacho huna unakitegemea huko mbeleni. Huwa tunajiandaa kwa mazuri tu na tunasahau …

Wakumbushe Watu Kwenye Kile Unachotaka Kufanikiwa

Mpendwa rafiki yangu, Sisi binadamu tunaasili ya kusahau. Muda mwingine tunaweza kuwaambia watu kitu na wasikitekeleze badala ya sisi kuwambusha tunaanza kuumba mambo mengine mengi. Wengine watasema mtu fulani anajisikia au ana dharau na mengine. Ukweli ni kwamba watu wana mambo mengi. Na hakuna mtu anayefikiria mambo yako muda wote. Kila mtu ana mambo yake …

Kubali Kufanya Hiki Kama Unataka Mabadiliko

Rafiki, Kila mtu anataka mabadiliko katika maisha yake lakini, Asili ya mabadiliko ni maumivu na watu kwa kuwa hawapendi kujisumbua na hawapendi maumivu basi ndiyo maana hawataki kusikia kitu kinachoitwa mabadiliko. Habari njema ni kwamba mabadiliko yoyote huwa hayamwachi mtu salama. Aidha unataka au hautaki mabadiliko lazima yatakuathiri kwa namna yoyote ile. Ukikataa kujibadilisha mwenyewe, …

Haya Ndiyo Maisha Mzigo Kwako

Rafiki, Kukosa kutumia maarifa sahihi karibu sehemu nyingi ya maisha yetu inatulazimu kupata kile ambacho hatukutakiwa kukipata. Maisha bila kutumia maarifa yanakuwa hayana maana, kwa kifupi yanakuwa ni maisha ya mazoea. Jamii yetu imekuwa inaishi maisha ya kawaida sana. imekuwa inaishi maisha ya mazoea kiasi kwamba mtu anayeishi maisha yake inakuwa inamnyanyasa sana. Jaribu kuangalia …

Siri Tatu Za Fedha Unazopaswa Kuzijua

Mpendwa rafiki yangu, Fedha ni jawabu la mambo yote. Kila mtu analitambua hilo bila ubishi wowote ule. Kama tunavyojua kuna aina nyingi za michezo na bahati nzuri ni kwamba kila mchezo una sheria zake na kama ilivyo michezo hiyo mingine kuwa na sheria hata fedha nayo iko hivyo hivyo ina sheria zake na anayeshindwa kwenda …

Design a site like this with WordPress.com
Get started