Kama Unataka Kuuza Sana, Tumia Sheria Hii Ya Halber Kwenye Masoko

Kwenye kitabu cha barua kutoka gerezani mwandishi alikuwa anamwandikia mtoto wake wakati yeye akiwa gerezani.Alikuwa ana mshirikisha misingi mbalimbali ya mafanikio. Mwandishi anamshirikisha mtoto wake sheria ambayo alikuwa anaitumia kwenye masoko na kufanikiwa. Sheria hii tunaweza kuitumia hata sisi na ikatusaidia kupata masoko na kuongeza mauzo. Unajua mauzo ndiyo kila kitu katika biashara, kama huuzi …

Usiwalazimishe Wengine Kuwa Kama Wewe

Kifupi hatuwezi kufanana na pale tunapokazana wengine wawe kama sisi tunakua tunafanya kazi ambayo iko nje ya uwezo wetu. Usiwalazimishe wengine wawe kama wewe lakini pia usijione wewe ni bora kuliko wao. Lengo kubwa la kujifunza ni kuyafanya maisha yako kuwa bora na siyo kuwalazimisha wengine maisha yao kuwa bora. Utakapojifunza na maisha yako yatakapokuwa …

Vyovyote Utakavyojichukulia Uko Sahihi

Aliyewahi kugundua magari ya kifahari yanayojulikana kwa jina la Land cruiser V8 anayejulikana kwa jina la Henry Ford,Aliwahi kunukuliwa akisema,"Kama unafikiri unaweza au unafikiri huwezi uko sahihi." Wewe unajifikiriaje? Unaweza au huwezi? Ukijichukulia unaweza uko sahihi na ukijichukulia huwezi uko sahihi pia. Yaani vyovyote vile unavyojichukulia uko sahihi. Wewe ndiyo mkurugenzi wa maisha yako, hivyo …

Hakuna Unachofanya Ambacho Kitakosa Matokeo Haya

Kuna vitu vingine viko nje ya uwezo wetu. Unaweza ukajituma kweli, ukachukua hatua ya ziada lakini kuna kitu ambacho huwezi kukipanga kitokeeje ambacho ni matokeo. Hakuna mwenye udhibiti wa matokeo, asili huwa inaamua matokeo na hakuna mtu wa kuipangia. Unapofanya kitu chochote kile, kuwa tayari kwa matokeo yoyote yale maana hatuna udhibiti wa matokeo gani …

Kabla Hujakutana Na Mtu Jifunze Mambo Haya Muhimu

Ukitaka kuwa mtu wa ushawishi sehemu yoyote ile pendelea kuwa mtu wa kujifunza watu wanataka nini. Wape kile wanachotaka na wewe utapewa kile unachotaka. Huwezi kuwashawishi watu kama wewe ni mtu wa kujali mambo yako na kusahau mambo ya wengine. Kama ni msomaji wa kitabu jitahidi usome kitabu cha how to win friends and influence …

Kama Unaona Elimu Ni Ghali, Jaribu Hiki Hapa

Kuna msemo mmoja unaosema kwamba kama unafikiri elimu ni ghali sana jaribu ujinga. Ukiona vya elea ujue vimeundwa. Kumbe basi, kila kitu kizuri tunachokiona ujue kimefanyiwa kazi. Kama hutaki kupata vizuri basi tumia vibaya. Hapa ndiyo ule msemo unakuja kama unafikiri elimu ni ghali sana jaribu ujinga. Watu huwa hatuko tayari kulipia gharama ya vile …

Fanya Kazi Hii Kwanza Kabla Hujaanza Majukumu Mengine

Akili zetu huwa hazipendi vitu vigumu kabisa, akili huwa inapenda vitu virahisi na haijisumbui kwenye vitu vigumu. Usishangae kuona watu wengi wakiahirisha vitu vigumu na kufanya vitu vyepesi. Pale unapokuwa na kazi mbili moja rahisi na nyingine ngumu wewe utachagua kuanza na ipi? Watu wengi watachagua rahisi na matokeo yake ile ngumu wanakuja kuiahirisha kufanya. …

Ni Wakati Wake Wa Kukirudisha Kwa Wenyewe

Huwa tunajidanganya kwamba sisi ni wa miliki wa milele wa vile ambavyo tunavyo kumbe siyo. Sisi ni wa miliki wa muda tu wa vile ambavyo tunavyo. Kwa mfano, ni wangapi wanaendesha magari na siyo yao? Wanaazima au kukodi lakini inapofikia muda analirudisha kwa mwenyewe, aliyeomba au kukodi hawezi kujimilikisha gari hilo bali anajua amepewa kwa …

Hiki Ndiyo Kitu Ambacho Ukipata Asubuhi Kinakwenda Kubadili Siku Yako Nzima

Huwa unaianzaje siku yako? Je unainza siku yako kwa kuangalia simu yako kujua nani amekutafuta na nini kinaendelea kwenye mitandao ya kijamii? Au unainza siku yako kwa kusali, kufanya mazoezi, kusoma kitabu, kuandika, kusikiliza vitabu vilivyosomwa vinavyokupa hamasa ya kwenda kufanya kazi? Au pengine unainza siku yako kwa kusikiliza uchambuzi wa magazeti, kusikiliza BBC, taarifa …

Jinsi Ya Kuwa Mtu Wa Tofauti Katika Karne Ya 21

Iko njia rahisi sana ya kuwa mtu wa tofauti katika jamii unayoishi.Dunia ya leo, tumezoea kuwaona watu wakiishi maisha ya kawaida yaani maisha ya kimazoea ambayo hayawapi makubwa wala hata hayawasaidii kulipa bili. Kama unaishi maisha ya kimazoea ambayo hayakusaidii hata kulipa bili hayo siyo maisha, wengi wanaishi maisha ya kimazoea kwa sababu hawataki kufanyia …

Design a site like this with WordPress.com
Get started