Usivumilie Kitu Chochote Ambacho Hukipendi

Kila maisha utakayoamua kuishi tayari yana maamumivu yake. Hakuna maisha ambayo hayana maumivu ila ni kuchagua tu aina ya maumivu ambayo uko tayari kuyaishi. Ila nakushauri usivumilie kitu chochote ambacho hukipendi kwenye maisha yako. Hata kama kila mtu anavumilia na anachukulia kawaida. Kama kitu hukipendi au hukubaliani nacho au siyo viwango vyako usikubali kuwa navyo. …

Jinsi Ya Kuwasaidia Watu Wengi

Kiasili kila mtu ni mfanyabiashara, uwe umeajiriwa au la na kuajiriwa ni biashara nayo ila iko katika daraja sifuri katika ngazi ya biashara. Unapokuwa unataka kuwasaidia watu basi kuwa na biashara kwani hata kama umeajiriwa kama mwajiri wako asingefungua biashara leo hii ungepata ajira? Kumbe basi, biashara ni moja ya njia ya kuwasaidia watu wengi …

Dalili Inayoonesha Kuwa Unarudi Nyuma Kiuchumi

Fedha ni jawabu la mambo yote na hilo halina ubishi kabisa kwani kila mmoja analiona hilo katika maisha yake ni namna gani fedha ilivyo muhimu. Anayekuambia fedha siyo muhimu basi akili yake haiko sawa. Ni muhimu sana kujipa tathimini katika kipato chako kila mwezi, siku, wiki au hata mwaka. Kama kipato chako hakiongezeki na matumizi …

Jinsi Ya Kuwa Na Siku Bora

Unapoianza siku yako ni maamuzi yako kutaka siku yako iweje na wewe ndiyo mkurugenzi wa siku yako kwa kupanga kile unachotaka kitokee. Asubuhi unapoamka una amua na kusema leo ni siku bora sana kwangu na nimechagua kuwa na furaha. Kama hujui nguvu ya kukiri, jaribu leo kukiri kuwa leo ni siku bora sana kwangu, nimechagua …

Njia Ya Pekee Ya Kutojiumiza

Katika wakati ambao watu huwa wanajiumiza na kujivuruga basi ni zama hizi tunazoishi. kwa sababu watu wanakuwa wanaweka matumaini yao kwenye vitu ambavyo viko nje ya uwezo wao na ndiyo maana ni rahisi kujiumiza. Iko njia pekee ya kutojiumiza na njia hiyo ni kutumia falsafa ya ustoa ambayo moja ya falsafa zake zinasema kuwa, usiweke …

Tathimini Ya Siku Yangu Ya Kuzaliwa Na Viwango Vitano Vya Kupima Afya Yako Ya Kifedha

Leo ni siku yangu ya kuzaliwa, nilizaliwa miaka 31 iliyopita tarehe 18/7/1989. Huwa nina kawaida ya kujifanyia tathimini katika kusherekea kumbukizi ya kuzaliwa kwangu. Leo asubuhi nilianza siku yangu tofauti kabisa na huwa navyoanza. Huwa ninaanza siku yangu kwa sala au tahajudi, kusoma kidogo, kuandika na mazoezi. Lakini katika vyote hivyo, huwa ninahakikisha kabla dunia …

Huu Ndiyo Msingi Wa Kupata Fedha Zaidi

Huwa tunafikiri ili tupate fedha zaidi tunapaswa kuwadhulumu watu, kuwaibia, kuwa tapeli, mwizi, kupokea rushwa nk.Msingi wa watu uko hivyo, wanaamini kuwa ili upate fedha zaidi lazima uzichukue kwa wengine. Leo tunakwenda kujifunza msingi wa tofauti kabisa wa kupata fedha zaidi. Kabla hatujaingia kwenye kujua msingi huo nikushirikishe msingi wa kupata chochote kile unachotaka kwenye …

Haya Ndiyo Madhara Ya Kutokua Na Kipaumbele Kwenye Maisha Yako

Asili ya dunia ina utele, ina kila kitu unachohitaji na kama hujui unachotaka huenda ikawa ni shida kwako dunia kukusaidia. Pale unapokuwa unataka kitu fulani lazima uwe na chaguo unalotaka, ukitaka kujenga nyumba lazima uwe na ramani ya nyumba unayotaka kujenga.Kwa ufupi, chochote kile tunachotaka lazima tuwe tunajua kile tunachotaka. Huwezi kutoa kile ambacho hukijui …

Hiki ndiyo Kitu Kidogo Kinacholeta Tofauti Kubwa

Huwa tunapenda kuchukulia poa baadhi ya mambo katika maisha yetu. Ni rahisi kuyachukulia poa mambo madogo lakini haya madogo ndiyo huwa yanatuumiza sana. Kwa mfano, mbu huwa ang'ata na kusababisha madhara ya ugonjwa kama vile malaria lakini tembo ni mkubwa lakini licha ya ukumbwa wake yeye wala hang'ati lakini mbu ni kadogo lakini kana leta …

Ukishajua Kipato Chako Kipo Hivi, Usithubutu Kufanya Haya

Moja ya misingi ya fedha ambayo unaalikwa kuijua ni kwamba, haijalishi unaingiza kiasi gani, ishi chini ya kipato chako. Lakini, wengi tunakwama hapa hatujui ya kwamba pale mtu unapokuwa una kipato kikubwa, au kipato kinapoongezeka utashangaa na matumizi nayo yanaongezeka sasa usipokuwa makini na hili utajikuta huna unachofanya. Kwa sababu kuna kawaida ya matumizi kuongeza …

Design a site like this with WordPress.com
Get started