Hiki Ndicho Kinachowatofautisha Wafuasi Na Viongozi

Aliyekuwa mkurugenzi na mwanzilishi mwenza wa kampuni ya Apple Steve Jobs aliwahi kunukuliwa akisema; Kinachowatofautisha kati ya wafuasi na viongozi ni ugunduzi. Hutakiwi kuwa kiongozi mfuasi bali unatakiwa kuwa kiongozi mgunduzi. Kila siku unatakiwa ujifunze namna ya kuongoza. Usipokuwa wa kujifunza maana yake umechagua kuwa mfuasi na hii maana yake ni kuwa hutoweza kugundua kitu …

Ukiwa Na Ujasiri Huu, Utapata Kile Unachotaka

Siyo kwamba wale wanaofanikiwa kwenye kitu fulani ni wajanja sana au wana bahati sana kuliko wengine. Wana nguvu moja ambayo ndiyo inawasaidia kupata kile wanachotaka. Unapata kile unachotaka kwenye maisha kama umekuwa na ujasiri wa kuomba kile unachotaka.Watu wengi huwa hawana ujasiri wa kuomba kile wanachotaka. Wanaishia kuongea tu kwa mdomo. Shabaha yangu ya kukuandikia …

Hii Ndiyo Kanuni Ambayo Huwa Haishindwi

Ili kupata kile unachotaka, anza kwanza kutoa kile ulichonacho. Haijalishi ni kikubwa au kidogo wewe anza kutoa na wanapopokea wengine na wewe ndiyo utapokea. Usidharau chochote kile ulichonacho. Wewe tafuta watu ambao wanaweza kunufaika na wewe kwa kile ulichonacho. Wafanyie kile unachotaka, kisha watake wakulipe. Hiyo ndiyo kanuni ya asili ambayo haijawahi kushindwa. Kama unatoa …

Hiki Ndiyo Kitu Kichungu Duniani Lakini Matunda Yake Ni Matamu

Sehemu pekee ambayo unaweza kuona nyota ni kwenye giza. Kila kitu kina faida yake kama ukikitumia vizuri. Wako wanaochukia giza lakini bila giza huwezi kuona nyota za angani. Wale wanaochukia giza ni sawa na wale wanaochukia changamoto kwenye maisha yao. Wakati mwingine, jifunze kutokana na kila unachokutana nacho. Mwanafalsafa Aristotle enzi za uhai wake aliwahi …

Eti Ni Kweli Huwezi Kuishi Bila Yeye?

Huwa unapenda kujidanganya kwamba huwezi kuishi bila kitu fulani. Muda mwingine unaenda mbali zaidi kwamba huwezi kuishi bila ya watu wako wa karibu ulionao sasa kwenye mahusiano.Huwa unapenda kujidanganya kwamba huwezi kuishi bila wao je ni kweli? Hayo yote ni uwongo, kitu pekee ambacho huwezi kuishi bila hicho ni pumzi tu. Unaweza kuishi vizuri tu …

Jinsi Ya Kung’arishwa Na Mawimbi Ya Maisha

Kama maisha ni shule, basi changamoto ndiyo darasa lenyewe. Dunia huwa inatupa mafunzo kila kukicha kupitia yale tunayokutana nayo.Dunia inatupa mafunzo ambayo yanatuwezesha kukua, kubadilika na kuamsha madhumuni yako makubwa hapa duniani. Huwezi kufeli katika haya maisha kama uko tayari kujifunza. Kama ambavyo vyombo ili vitakate huwa vinasuguliwa na stili waya. Kusuguliwa kule na stili …

Kama Unajifunza Sana Na Hupati Matokeo Unayotaka Shida Yako Iko Hapa

Vuta picha tokea umeanza kujifunza mpaka leo umeshajifunza vingapi? Angalia yale uliyojifunza yanaendana na mafanikio uliyonayo? Kuna wale watu ambao wananunua vitabu na kulipia maarifa mbalimbali. Wanajifunza kweli lakini, cha ajabu wanaishia kuwa na maisha ya kawaida. Wewe unafikiri shida iko wapi? Kwanini upate maarifa ya kuwa bora na ufanane na mtu ambaye hana maarifa …

Jihamasishe Kwa Mafanikio Unayopata

Kuna njia mbili za hamasa, moja adhabu na mbili ni zawadi. Ukiwachukua watu wawili na mmoja umhamasishe kwa njia ya zawadi atafanya vizuri sana, atajituma kuhakikisha anapata zawadi yake. Lakini, njia ya adhabu huwa haimsukumi mtu kufanya jambo na kama unataka kuwapoteza watu wahamasishe kwa njia ya adhabu lakini zawadi inafanya vizuri sana. Kwa mfano, …

Angalia Usalama Wa Fedha Zako

Wako watu ambao wanawekeza kupoteza na wako ambao wanawekeza kupata.Wale wanaowekeza kupata ni wale ambao wanafuatilia kwa karibu sana kile walichowekeza. Wale ambao wanawekeza kupoteza ni wale ambao wanawekeza fedha zao sehemu na kukosa muda wa kuzifuatilia. Nikupe ushauri wa bure rafiki yangu, popote pale ulipowekeza fedha zako hakikisha macho yako, yako pale. Kuwa mtu …

Usikubali Kushindwa Kwenye Kila Kitu

Ndugu mmoja katika maadhimisho ya miaka 50 ya seminari ya maua ambapo walikutana wale wote waliosoma pale alitoa ushuhuda wake kwa uchungu akasema, huwa anamwambia Mungu kila mara nimeshindwa kuwa Padre na hata wito wa ndoa unishinde? Kauli hiyo inamfanya awe imara kwenye ndoa yake licha ya kushindwa kwenye eneo fulani. Rafiki yangu, usikubali kushindwa …

Design a site like this with WordPress.com
Get started