Kitu Ambacho Binadamu Hapendi Kufanyiwa Kwenye Maisha Yake

Kisaikolojia binadamu wanapenda kuhisi kuthaminiwa, kuhusishwa, kupendwa na kujaliwa. Ndiyo maana unakuta mtu mwingine anaweza kulalamika kuwa kwanini hajahusishwa katika jambo fulani. Unapomhusisha mtu naye anajisikia kuona anaaminika, anapendwa na kuthaminiwa pia. Kitu ambacho binadamu hapendi kufanyiwa kwenye maisha yake;Ni kufanyiwa MAAMUZI. Kila binadamu anapenda kufanya maauzi yake mwenyewe, anapenda kushirikishwa kwenye mchakato wa maamuzi. …

Eneo Ambalo Watu Wengi Huwa Wanalikimbia

Hakuna kitu kinachopatikana kirahisi. Chochote unachotumia kikiwa tayari unaweza kukiona kama vile kilipatikana kirahisi lakini sivyo. Kwa mfano, umeshazoea kula chakula lakini hujawahi kupitia mchakato wa uandaaji wa chakula. Mwalimu kabla hajaingia darasani lazima apitie mchakato wa uandaaji wa somo. Mwandishi kabla hajaandika lazima apitie mchakato wa uandaaji wa kile anachotaka kwenda kukiwasilisha. Eneo ambalo …

Ujue Ujumbe Muhimu Kwako Kutoka Kwa Aliyekuwa Raisi Wa Awamu Ya 40 Wa Marekeni

Kama una imani kuwa kiongozi fulani atakwenda kubadilisha maisha yako basi bado hujajitambua. Anayehusika kwa asilimia mia moja na maisha yako ni wewe mwenyewe. Hata kama ulimpigia mtu kwa imani kuwa atakwenda kubadilisha maisha yako, hapo umejidanganya. Fanya uchaguzi leo wa kuamua kubadili kabisa maisha yako siku ya leo.Leo ndiyo siku pekee ya kuamua kubadilisha …

Hili Ndiyo Lengo Kuu La Mahusiano

Kila mmoja wetu yuko katika mahusiano kadiri ya vina saba. Hakuna mtu ambaye hayuko katika mahusiano. Ukisema hauko katika mahusiano maana yake wewe hujazaliwa na binadamu. Mahusiano ni muhimu sana maana wewe siyo mti kusema kwamba hutohusiana na watu wengine. Lazima uhusiane na watu wengine ili maisha yako yaweze kwenda. Kwani karibu kila kitu tunachotaka …

Hiki Ndiyo Kitu Ambacho Watu Wanakipata Kwa Shida Sana

Sisi binadamu huwa tunajisahau sana pale tunapofanikiwa kupata kile tulichokuwa tunataka. Ni rahisi kusahau hata maaumivu tuliyopitia mpaka tukafanikiwa. Baada tu ya kupata maumivu nayo yanapotea ghafla. Kuna kitu ambacho watu huwa wanakipata kwa shida na wakikipata wanakuja kukitumia vibaya na kusahau machungu yote. Kitu hiko ni fedha. Watu wanapata fedha kwa shida sana. Wanatoa …

Ukitaka Kufika Mbali Anza Na Hiki

Ili watu waweze kujua una nini ndani yako lazima uanze kwanza kutoa kile ulichonacho ndani yako. Ukitaka kufika mbali kwenye kile unachotaka anza kwanza kutoa kile ulichonacho. Watu hawawezi kujua una nini ndani yako kama hujaanza kukitoa kile unachojua. Usikae na kile unachojua tu bila kukitoa maana usipokitoa huwezi kufanikiwa. Unafanikiwa zaidi pale unapotoa zaidi. …

Hii Ndiyo Sauti Ambayo Mtu Anapenda Kuisikia

Hakuna sauti ambayo watu wanapenda kuisikia kama sauti ya jina lake.Watu wanapenda kusikia wakiitwa majina yao, hii inawafanya wajisikie kuthaminiwa na ni watu wa thamani. Watu huwa wanapenda kufanya kila namna ili tu majina yao yaweze kukumbukwa. Kwa mfano, matajiri wengi wako radhi hata wajenge majengo kwa msaada lakini waitwe majina yao. Watu wanapenda kuitwa …

Jifunze Kumsikiliza Mtu Huyu Na Utapiga Hatua Kubwa

Unakwama wapi? Ni rahisi kufanyia kazi maoni ya watu wengine na kusahau kufanyia kazi maoni yako binafsi. Watu wengi wanajali maoni ya wengine kuliko kujali maoni yao. Ni kawaida ya watu wengi kuishi maisha ya watu wengine na kusahau kuishi maisha ya ndoto zao. Wengi hawafuati mioyo yao. Kama kila mtu angekuwa anafuata moyo wake …

Hawa Ndiyo Watu Ambao Uko Nao Katika Kipindi Cha Mpito

Maisha ya wanandoa huwa wanaanza wakiwa wawili na baadaye wanabarikiwa kupata watoto. Ila baada ya muda watoto wote wataondoka na kuwaacha nyie wawili kama mlivyo. Kama uko kwenye ndoa, mpende mwenza wako maana utakua naye maisha yako yote mpaka pale kifo kitakapowatenganisha. Usigawe upendo wako wote kwa watoto ukifikiri maisha yako yote utakua nao na …

Hiki Ndiyo Kitu Kinachowatawala Watu Wengi

Ni rahisi watu kusema kwa mdomo na kujivunia kuwa wao hawana hofu. Hofu inaendesha dunia kuliko hata unavyofikiria kwenye maisha yako. Kila siku hofu inawafanya watu washindwe kwenda kule wanakotaka kwenda. Ni vitu vingapi umeshindwa kuvifanya kwa sababu ya hofu? Na ukiangalia sababu kubwa ni hofu labda ya kuogopa kushindwa. Unakuwa unaogopa endapo ukijaribu na …

Design a site like this with WordPress.com
Get started