Kama Linakusaidia Kukua, Siyo Tatizo Bali ni Zawadi

Katika maisha, si kila jambo gumu ni la kulalamikia. Si kila changamoto ni laana. Kuna baadhi ya changamoto zina sura ya matatizo, lakini ndani yake zimebeba zawadi kubwa sana—zawadi ya ukuaji wako binafsi. Ndiyo maana inasemwa:"Kama linakusaidia kukua, siyo tatizo, bali ni zawadi." Watu wengi hukimbia maumivu, hukimbia usumbufu, hukimbia hali ngumu. Lakini wakisahau kuwa …

KILA JAMBO LINALOONEKANA BAYA HUISHIA VIZURI

Wakati mwingine unapopitia hali ngumu, akili yako hukushawishi kwamba hiki ndicho kilele cha maumivu na hakutakuwa na mwisho mzuri. Unaanza kujiuliza: “Nitapona kweli? Nitatoka kweli?” Hofu na wasiwasi huongezeka kwa sababu ya picha mbaya unazozijenga kichwani mwako. Lakini ukweli ni kwamba, kila jambo linaloonekana baya, huisha vizuri. Kumbuka Safari Yako ya Nyuma Angalia maisha yako …

Magumu Ni Sehemu Ya Maisha: Imani Za Kukusaidia Kustahimili Mpaka Ufaulu

Magumu ni sehemu isiyoepukika ya maisha ya binadamu. Haijalishi uko hatua gani ya maisha — mwanzo au kileleni, tajiri au maskini, kijijini au mjini — magumu yatatokea tu. Hakuna anayekwepa changamoto kabisa. Mara nyingine magumu hayo huja kwa kasi ya ghafla, bila onyo, na huweza kutushtua hadi tukajiona hatuwezi tena kusonga mbele. Lakini ukweli ni …

Mungu Tu Tunayemuamini – Wengine Walete Data

Katika ulimwengu wa leo unaoongozwa na taarifa, ushahidi na matokeo, kuna msemo maarufu sana miongoni mwa Wamarekani unaosema:“In God we trust, all others must bring data.”(Tunamwamini Mungu, wengine wote walete takwimu.) Msemo huu unaakisi ukweli muhimu katika maisha ya kila siku – kwamba imani ya kweli inapaswa kujengwa juu ya ushahidi, si maneno matupu. Mungu …

Ubobezi Unavyozalisha Shauku na Mapenzi Katika Kazi

Kuna watu wengi wanahangaika kutafuta "kile wanachokipenda kufanya" kabla hawajaanza kazi yoyote. Wanapoteza miaka wakisubiri hisia za upendo kwa jambo fulani zitokee, ndipo waanze kulifanya kwa bidii. Lakini tafiti na uzoefu wa watu waliobadilisha maisha yao kwa kazi wanazozifanya, vinaonyesha ukweli tofauti kabisa: upendo wa kazi mara nyingi huja baada ya ubobezi, siyo kabla yake. …

SUBIRA — NGUVU ILIYOSAHULIKA, LAKINI YENYE MAMLAKA KWENYE MAISHA

Kuna msemo wa Kiswahili usemao: “Haraka haraka haina baraka.” Zama tunazoishi sasa ni zama za kasi — kila mtu anataka mafanikio ya haraka, fedha za haraka, matokeo ya haraka, hata uhusiano wa haraka. Tumekuwa kizazi kinachokimbia kuvuna kabla hakijapanda. Hii ndiyo sababu wengi wanakatishwa tamaa, kuchoka, kuacha njiani, au kufanya maamuzi ya kuharibu maisha yao. …

FANYA VITU VIDOGO KWA UBORA – HUKO NDIKO MAFANIKIO YANAKOANZIA

Kuna mtu mmoja aliwahi kusema: Kama unashindwa kufanya vitu vikubwa kwa ubora, basi fanya vitu vidogo kwa ubora. Hii ni kauli fupi lakini yenye uzito mkubwa wa maisha. Katika dunia ya leo, watu wengi wanakimbilia mambo makubwa – wanataka kufanikisha miradi mikubwa, kujulikana sana, kuwa matajiri haraka au kubadili dunia. Lakini wengi wao wamesahau ukweli …

KILA MTU ANAYEFANYA MAISHA YAKO YAENDE MBELE NI WA KUMTHAMINI

Kuna vitu vingi vinavyoweza kutafsiri mafanikio, lakini katika msingi wake kabisa – mafanikio yako hutegemea watu. Ndiyo, watu.Unataka mafanikio makubwa? Waheshimu watu. Wathamini wale wanaochangia safari yako. Shukrani ni mbegu – unapoipanda, huvuna neema, heshima, na msaada wa kudumu. Watu Ndio Daraja la Mafanikio Chochote kile unachotaka kwenye maisha yako – iwe ni pesa, maarifa, …

Kwanini Watu Hawafanyi Kile Wanachopaswa Kufanya?

Katika maisha na kazi, kuna malalamiko mengi kama haya:"Nimewaelekeza, lakini hawafanyi.""Nimefundisha mara nyingi, lakini hakuna kinachobadilika.""Wanajua nini cha kufanya, lakini hawaonyeshi matokeo." Hali hii imesababisha wengi kuvunjika moyo, kukata tamaa, au kuamini labda watu hawana uwezo. Lakini hebu tuiweke wazi: kama mtu hafanyi jambo fulani ni kwa sababu mbili tu — ama hajui, au hataki. …

Mafanikio Hayatoki Kwa Kutafuta Kazi Bora Bali Kufanya Kwa Ubora

Watu wengi huamini kuwa mafanikio hutegemea sana kupata kazi au biashara “bora.” Wanaamini mafanikio ni matokeo ya bahati ya kuwa mahali pazuri, kufanya kazi fulani kubwa au kuingia kwenye biashara maarufu. Lakini ukweli ni huu: Siyo kazi au biashara bora inayokupa mafanikio, bali namna unavyofanya kazi au biashara yako kwa ubora. Acha Kutafuta Kilicho Bora, …

Design a site like this with WordPress.com
Get started