Njia Saba za Kujitofautisha na Kuwa wa Kipekee (Sehemu ya Kwanza)

Kuna matatizo mawili makubwa kwenye zama tunazoishi sasa.Tatizo la kwanza ni watu kuishi kwa mazoea na kufuata mkumbo . Wanafanya kile ambacho kila mtu anafanya, kwa sababu wengine wamezoea kufanya hivyo. Hapo ndipo upekee wao unaofaa kung’aa unazimwa. Tatizo la pili ni watu kutokujali kile wanachofanya . Iwe ni kazi au biashara, wengi wanafanya tu …

Huwezi Kujua Nani Yuko Mbele Yako

Kila siku tunakutana na watu wapya—katika kazi, biashara, safari, hata mitaani. Wengi huwa tunawapima juu juu: mavazi yao, kazi wanazofanya, au maneno yao ya kwanza. Lakini ukweli ni huu: huwezi kujua nani yuko mbele yako. Ndiyo maana ni hekima kubwa kumchukulia kila mtu kwa adabu, heshima, na uaminifu. Yule mtu unayemdharau kwa sababu anaonekana hana …

Siri Kuu ya Kufanya Makubwa

Kila mtu ana ndoto kubwa moyoni mwake. Wengine wanataka kuanzisha biashara kubwa, wengine kutengeneza mali ya kudumu, na wengine kubadilisha maisha ya jamii zao. Lakini siri kubwa ya kufanikisha hayo yote siyo kusubiri kesho, siyo kuanza pale kila kitu kitakapokuwa sawa, bali kuanza sasa – kidogo ulipo, na kwa kile ulicho nacho. Ukikaa ukifikiria ukomo, …

Mitazamo 4 ya Kubadili ili Kupata Fedha na Utajiri Mkubwa – Sehemu ya Nne

Katika sehemu zilizopita tuliona mitazamo mitatu inayoweza kukuzuia kupata fedha na utajiri mkubwa: Uhaba – kuamini fedha ni chache na lazima uzifiche. Kufa na kupona – kuamini ukizikosa fedha ni mwisho wa maisha. Ushindani – kuamini mafanikio yako lazima yatokane na kushindwa kwa wengine. Leo tunakamilisha kwa Sehemu ya Nne: mtazamo wa kuchukua. Mtazamo wa …

Mitazamo 4 ya Kubadili ili Kupata Fedha na Utajiri Mkubwa – Sehemu ya Tatu

Katika sehemu ya kwanza tulizungumzia kuhusu uhaba na namna ya kuubadili kuwa utele. Kisha kwenye sehemu ya pili tuliona mtazamo wa kufa na kupona na namna ya kuubadili kuwa mtazamo wa mchezo na utulivu.Leo tunaendelea na Sehemu ya Tatu: ushindani. Mtazamo wa Ushindani Wengi wamefundishwa kuamini kwamba ili wao washinde, basi wengine lazima washindwe. Huu …

Mitazamo 4 ya Kubadili ili Kupata Fedha na Utajiri Mkubwa – Sehemu ya Pili

Katika sehemu ya kwanza tulianza na mtazamo wa uhaba na jinsi wa kubadilisha kwa mtazamo wa utele. Leo tunaendelea na Sehemu ya Pili — mtazamo unaoendelea kuwakwamisha wengi kifedha: kufa na kupona. Mtazamo wa "Kufa na Kupona " Wengi wanaona fedha kama kitu cha kufa au kupona — kama ukipoteza, maisha yamekamilika. Wazo hili linajenga …

Mitazamo 4 ya Kubadili ili Kupata Fedha na Utajiri Mkubwa – Sehemu ya Kwanza

Kila mtu anatamani kuwa na fedha nyingi na maisha bora. Lakini mara nyingi tatizo si fedha yenyewe, bali mtazamo wetu kuhusu fedha. Kuna mitazamo minne ambayo lazima uibadili kabisa kama kweli unataka kufanikisha safari yako ya kifedha. Mtazamo wa Uhaba Wengi huamini fedha ni haba. Wanafikiri njia pekee ya kuendelea nazo ni kuzificha na kuzikumbatia.Matokeo …

Maana Halisi ya Aibu

Robin Sharma aliwahi kushirikisha mstari alioupokea kwa nguvu kubwa kutoka kwenye kitabu Meditations cha Marcus Aurelius. Anasema: "Aibu: roho kukata tamaa wakati mwili bado una nguvu ." Ukikaa na kuutafakari huu mstari, unagundua mara ngapi tumewahi kujiwekea aibu sisi wenyewe. Mara ngapi umekata tamaa haraka ilhali bado ulikuwa na uwezo, nguvu, na nafasi ya kusonga …

Mbinu ya Kujijengea Kujiamini

Huwezi kufika kwenye mafanikio makubwa kama hujiamini. Kujiamini ni nguzo ya kila mafanikio, kwa sababu bila kujiamini hata fursa kubwa ikikujia, utaiona ni kubwa sana kuliko uwezo wako. Lakini kujiamini hakujengwi kwa maneno matupu. Kujiamini kunajengwa kwa vitendo na hatua za kila siku. Anza kwa kujitambua Jiulize: Nataka kuwa mtu wa aina gani? Ukishajua jibu, …

Tafuta Furaha, Shida Huwa Zinakuja Zenyewe

Kuna ukweli mmoja wa maisha ambao kila mmoja wetu anaouona kila siku: shida huwa hazihitaji mwaliko. Hazihitaji ratiba, wala mipango. Zenyewe hujitokeza—mara nyingine kwa ghafla, mara nyingine kwa taratibu—lakini bila shaka huja. Lakini furaha siyo kitu kinachokuja yenyewe. Furaha ni kitu kinachohitaji kutafutwa, kutengenezwa na kulindwa. Watu wengi hukaa wakisubiri mazingira yabadilike ndipo wawe na …

Design a site like this with WordPress.com
Get started