Badilisha Gia Na Weka Gia Namba Moja Kwenye Awamu Hii Ya Pili Ya Mwaka

Rafiki, hongera kwa zawadi ya miezi ya sita kuendelea kua hai na heri ya mwezi juni. Salamu nyingi rafiki zikufikie hapo ulipo lakini pia nikutakie kila la heri katika awamu hii ya pili ya mwaka huu. Rafiki, huenda mwaka huu ulipoanza uliuanza kwa gia namba nne, na kama tunavyojua kwa wale madereva ukianza kuendesha gari …

Kabla Ya Kuingia Katika Maisha Ya Ndoa Jiandae Kisaikolojia Kukutana Na Kitu Hiki

Siyo kila mtu ameitwa katika maisha ya ndoa hivyo kama unajiona hutoweza kufiti ni bora ubaki katika maisha ya useja nao ni wito kama wito mwingine lakini sharti uwe mwaminifu siyo unajifanya huishi katika maisha ya ndoa lakini una bingwa wa maisha ya uzinifu. Ukiamua kuwa mtu fulani ishi uadilifu wako. Usiingie katika maisha ya …

Ukitaka Kufanikiwa Acha Tabia Hii

Tumekuwa ni watu wa kujali sana miili yetu kuliko hata ndoto tulizonazo. Tunakubali kuendeshwa na miili yetu badala ya sisi kuiendesha miili yetu. Muda mwingine tunachelewa hata katika maeneo muhimu ya kazi kwa sababu ya kuuti mwili kitandani. Usingizi unawatawala watu kiasi kwamba hata ndoto zao walizokuwa nazo wanaziona hazina maana. Hatuwezi kupiga hatua kama …

Ifahamu Fedha Ambayo Huruhusiwi Kuitumia

Fedha huwa haihitaji unafiki kama unaipenda nayo itakupenda  kama ukifuata masharti yake. Mwanafunzi yeyote anayesoma kama hapendi somo analosoma ni rahisi kufeli kuliko hata yule mtu anayelipenda. Jaribu kuangalia na kuvuta picha tu wewe mwenyewe ulivyokuwa unasoma somo ulilokuwa unalipenda na lazima mwalimu wake ulikuwa unampenda na ulikuwa unaliwekea juhudi kweli kulisoma na lilikuwa halikuangushi …

Changamoto Tatu Zinazoikabili Dunia Ya Leo

Unapozungumzia maisha basi huwezi kuacha kuepuka kuutumia au kukutana na msamiati wa changamoto, sijawahi kuona maisha ambayo hayana changamoto na wewe ukiona huna changamoto basi unafanya kitu cha kawaida sana au hujaribu kwenda hatua za ziada katika maisha yako. Lakini zipo zile changamoto ambazo ni chanya zinatupa hamasa ya sisi kusonga mbele lakini zipo zile …

Sababu Zinazopelekea Mtoto Kufanya Vibaya Shuleni Na Nyumbani

Yuko mtoto mmoja  ambaye alikuwa hafanyi vizuri shuleni na akipewa kazi za shule analia tu. Akiwa nyumbani anapenda kujifungia chumbani. Wazazi wake wakaamua kumpeleka mtoto wao kwa mwanasaikolojia ili awashauri mtoto ana matatizo gani. kila mzazi alipata nafasi ya kuhojiwa na mwanasaikolijia kuelezea tatizo la mtoto na mtoto naye alipata nafasi ya kujielezea kwa mwanasaikolojia. …

Kitu Muhimu Cha Kuzingatia Pale Unapotaka Kuajiri

Changamoto kubwa sasa hivi duniani kwa waajiri wengi ni watu. Watu sahihi wamekuwa ni changamoto kubwa, watu wanalalamika hakuna kazi lakini ukija kumpa mtu kazi hawezi kufanya kazi kama vile unavyotaka wewe. Watu wamekuwa changamoto ndiyo maana dunia inapambana kutengeneza maroboti kuchukua nafasi za kazi za watu. Kupata watu waaminifu imekuwa ni adimu sana na …

Kwanini Hupigi Hatua Katika Maisha Yako

Kila binadamu ana mawazo mazuri sana. Kila kitu tunachokiona hapa duniani vilivyotengenezwa na watu basi vilianza na mawazo. Kuandika kwangu nilianza na wazo la kuandika na huenda na wewe kusoma kwako hapa umeanza na wazo la kutaka kusoma ili ujue ni sababu gani hiyo inayotufanya tusipige hatua katika maisha yetu. Akili yako ni kiwanda kinachozalisha …

Kwanini Fedha Ni Muhimu Kwako

Ni muhimu kwa sababu inakubalika kila sehemu, kwa mfano, inakubalika serikalini, kwenye nyumba za ibada, hospitali, na karibu maeneo mengi ya maisha yetu inakubalika. Ni jawabu la mambo yote na ni muhimu sana katika maisha yetu siyo kitu kingine hicho bali ni fedha. Fedha ni mfalme wa karne hii kwa sababu anakubalika kila mahali. Ni …

Zijue Faida Za Kuanza Vizuri

Mwanafalsafa Aristotle aliwahi kunukuliwa akisema, mwanzo mzuri ni nusu ya kumaliza vizuri. Ni kweli pale tunapoanza vizuri tunakuwa tuna uhakika wa katika kile tunachofanya. Kwa mfano, timu za mpira zinapoanza vizuri katika ligi basi wanakuwa wanajiweka katika nafasi nzuri. Tunapokuwa tunaanza vizuri siku yetu kwa kuamka mapema na kuanza kujitumikia sisi wenyewe kabla ya kwenda …

Design a site like this with WordPress.com
Get started