Usipambane Na Mtu Huyu

Iko hivi rafiki yangu, unatoa kile ambacho unacho. Huwezi kutoa kile ambacho huna. Kumbe basi, mtu anatoa kile ambacho anacho. Kama una amani ya moyo wako basi utatoa amani. Kama una chuki utatoa chuki. Kama una upendo ndani yako basi utatoa upendo. Siku zote huwa tunauza kile ambacho tunacho. Mtu akiwa na matatizo yake ya …

Vigezo Vitatu Vitakavyokusaidia Kuchagua Watu Wa Kufanya Nao Kazi

Linapokuja suala la kazi watu wa kufanya nao kazi huwa wanakuwa ni changamoto sana. Ukikosa watu wa kufanya nao kazi ni mtihani, ukiwapata tena nao wanakuwa mtihani. Kila kitu katika maisha kinakuwa mtihani. Tunasema kazi zimekuwa shida karne hii lakini ukweli ni kwamba watu ndiyo wamekuwa tatizo. Watu wakipewa kazi hawawezi kutoa ile thamani ambayo …

Unapaswa Kushukuru Juu Ya Jambo Hili

Huwa kila mtu anapenda mambo yake yaende kama alivyopanga. Wakati mwingine yanaweza kwenda kweli kama ulivyopanga na kuna wakati mambo yanaenda vile yanavyotaka. Pale mambo yanapoenda tofauti na ulivyopanga wala usikarike bali furahia. Kwa sababu wewe ni nani mpaka asili ikuogope? Asili huwa inaamua kufanya kile inachotaka bila kumsikiliza mtu. Hivi asili ingekuwa inawasikiliza watu …

Huu Ndiyo Mzigo Mkubwa Wa Maisha

Ukikutana na watu utaweza kusema wako sawa lakini wengi hawako sawa. Kwanini? Kwa sababu kuna kitu wanakosa kwenye maisha yao. Usione watu wanatembea lakini kiakili wengine hawako sawa. Rafiki yangu, maisha ambayo hayana kusudi ni maisha mzigo kwako. Unakuwa huna tofauti na zombi ukuwa upo upo tu. Mtu ambaye hana kusudi maana yake nini? Hajui …

Hiki Ndiyo Kitu Kinachohitajika Kwenye Kila Eneo La Maisha Yako

Ulipoona kichwa cha makala moja kwa moja ulijua kuwa ni fedha. Kitu ambacho kinahitajika kwenye kila eneo la maisha yako. Japokuwa fedha ni muhimu lakini leo sitoongelea fedha kabisa. Kama unataka upate kitu chochote kile kwenye maisha yako lazima utahitaji muda wa subira. Ukitaka kufanikiwa kiroho utahitaji muda wa uvumilivu. Ukitaka kufanikiwa kiakili, utahitaji kukua …

Jinsi Ya Kuwafanya Watu Kufanya Kitu Kwa Gharama Ndogo

Ulishawahi kujiuliza ni kwanini utakuta watu wanajitoa sana kwenye kazi za kusaidia hata kazi ya kulipwa? Hii ni kwa sababu watu wanajitoa sana kwa sababu kile wanachofanya kina maana kubwa kwao na kwa wengine pia. Kama ulikuwa hujui, leo jua hivi, watu wanapenda kufanya kitu chenye maana kwao na kwa wengine hata kama hawapati malipo …

Usisahau Kufanya Jambo Hili Muhimu Kwako Kama Unapambana Kuongeza Kipato

Fedha ikiwepo huwa haikosi matumizi. Unaweza kupambana kweli kuongeza kipato lakini kama usipofanya jambo muhimu ninalotaka kukueleza leo utakua unafanya kazi bure. Maisha yanapanda kila siku hivyo na wewe unatakiwa kupanda kwa kuongeza kipato. Usiishie kulalamika maisha yamepanda tu, na wewe jiongeze kwa kuongeza kipato cha ziada. Kama umeajiriwa kuwa na kitu cha ziada kinachokuingizia …

Huwezi Kumaliza Siku Bila Kufanya Kitu Hiki

Kila siku unapoamka jiandae kisaikolojia kuwa utaenda kukutana na watu ambao wataenda kinyume na wewe. Wako ambao watakukera, watakuudhi, yako mambo mengi ambayo yanahusiana na hayo. Ndiyo maana nasema, kwa binadamu yoyote yule, ni vigumu sana kumaliza siku hujakwazwa na yeyote yule. Kila siku lazima utakwazwa je utakuwa ni mtu wa kukasirika kila siku na …

Hivi Ndivyo Vitu Rahisi Kukumbuka Kwenye Maisha Yako

Kitu chochote kinachokuja kirahisi kwenye maisha yako. Huwa kinaondoka kiurahisi pia. Pata picha kwenye maisha yako, ni vingapi umevipata kirahisi? Hata katika kujifunza kile unachojifunza kwa njia ngumu huwa ni rahisi kukikumbuka kuliko kile unachojifunza kwa njia rahisi. Vitu rahisi kukumbuka kwenye maisha yako ni vile ambavyo umejifunza kwa ugumu. Hata katika ukusanyaji wa fedha, …

Huyu Ndiyo Mtumishi “Faya” Anayeweza Kufanya Makubwa Kwenye Maisha Yako

Watu ni wagumu kuamini lakini ukiwa na ushuhuda unakuwa unamaliza kazi mapema sana.Ushuhuda unawaaminisha watu kuwa kitu fulani ni kweli na maamuzi yao yatakuwa sahihi endapo wakichukua hatua. Kwenye mambo ya kiimani watu wengi huwa wanatekwa na miujiza inayotendeka. Watu wakisikia mtumishi, nabii fulani ni “faya” na wanapata ushuhuda wengi watahamasika na kwenda huko bila …

Design a site like this with WordPress.com
Get started