Hiki Ndiyo Chanzo Cha Kutokuwa Na Matokeo Mazuri Kwenye Kila Eneo La Maisha Yako

Mpendwa rafiki yangu, Kama bado hujapata kile unachotaka kuna chanzo kimoja ambacho ndiyo ninakwenda kukuelezea hapa kwanini bado hujakipata. Sisi binadamu ni wazuri sana kwenye kupanga lakini kuchukua hatua ndiyo kuna shida kubwa, kama ingekuwa tunakuwa vile tunavyotaka kwa njia ya mdomo tu basi kila mtu angekuwa tajiri kwenye kila eneo analotaka kwenye maisha yake. …

Hii Ndiyo Asili Ya Tabia Zote Unazojua

Mpendwa rafiki yangu, Hakuna mtu anaamka anajikuta anadaiwa milioni kumi. Mwanzo wa kitu chochote ulianza kidogo kidogo. Hakuna mtu aliyezaliwa na tabia fulani ila tabia zote tulizonazo tumezitengeneza sisi wenyewe. Asili ya tabia zote tunazojua ni matokeo ya kuanza kufanya kidogo kidogo na matokeo yake kuja kuwa tabia ya kudumu. Waulize watu wote walioingia kwenye …

Ushuhuda Wa Miaka Mitatu Ya Kuandika Kila Siku Na Mambo Matano Ya Kujifunza

Mpendwa rafiki yangu, Safari yangu ya kuandika kila siku kupitia mtandao wa Kessy Deo ilianzia tarehe moja octoba mwaka 2016. Hivyo basi, leo hii namshukuru Mungu kwa kuniwezesha kuandika kila siku bila kuacha tokea mwaka 2016. Kuandika kila siku ni kazi, lije jua au mvua ,kuwepo na changamoto au la lazima makala iende hewani.  Leo …

Hiki Ndiyo Kitu Kinachotusaidia Bila Hata Sisi Kujua

Natumaini imeshawahi kukutokea siku moja au mara nyingi umepanga kwenda sehemu fulani kwa muda fulani halafu likatokea jambo ambalo hata hukutegemea na ukajikuta umechelewa sehemu husika. Hiyo haitoshi, siku nyingine unajikuta unamuwaza rafiki yako au mtu fulani kabla hata hujajua la kufanya utashangaa yule mtu uliyekuwa unamuwaza anakupigia simu au kuja nyumbani uliko na unamwambia …

Sababu Kuu Moja Kwanini Unatakiwa Ujisukume Wewe Mwenyewe

Mpendwa rafiki yangu, Katika maisha yetu ya kila siku jifunze kujitegemea, tunapokuwa tunajitegemea katika mambo yetu ni ngumu watu wa nje kutuangusha. Unatakiwa kutambua kuwa jukumu la maisha yako ni lako mwenyewe hivyo usisubiri watu waje wakupambanie. Je kwanini unatakiwa ujisukume mwenyewe  au ujitume? Iko sababu kuu moja ambayo imenihamasisha siku hii ya leo nikuandikie …

Huu Ndiyo Mfumo Mzuri Wa Mafanikio Wa Kuishi Kila Siku

Tumekuwa ni kama wakulima ambao wanapanda leo na kesho wanafukua hata kabla mbegu haijaota. Hebu chukulia mfano, mkulima anapanda leo mbegu ya mahindi kesho anaifukua na kutaka tena kwenda kupanda kitu kingine. Je kwa mtindo huu, unafikiri ataweza kufanikiwa kweli? Ataweza kuona hata mbegu ikichipua? Hawezi kuiona, unapopanda unatakiwa uwe na subira mbegu ikae chini …

Hasara Moja Utakayoipata Pale Utakapoianza Siku Yako Bila Kipaumbele

Mpendwa rafiki, Usipopangilia muda wako vizuri utaishia bila kujua umefanya nini cha maana na huku ukijikuta umechoka. Ukianza siku yako kwa kutumikia mitandao ya kijamii, bila kujipangilia wewe mwenyewe yale muhimu kwako ni lazima utapoteza siku yako. Kiufupi rafiki yangu, hasara moja utakayoipata pale utakapoianza siku yako bila kipaumbele ni ; Kila kitu kitakuwa kipaumbele …

Jinsi Ya Kuandika Upya Hadithi Ya Maisha Yako

Kila mtu ana uwezo mkubwa sana ndani yake lakini watu wengi hawatumii vizuri uwezo mkubwa walionao. Ni kama vile watu wanavyoenda kununua kompyuta yenye uwezo mkubwa kusikiliza mziki. Hapa tunakuwa tunaua uwezo wa kompyuta kwa sababu ina uwezo mkubwa wa kufanya mambo lakini wewe unaitumia kwa kusikiliza mziki pekee. Ndivyo ilivyo hata sisi katika maisha …

Sababu Mbili Zitakazokufanya Ushindwe au Ushinde Kwenye Jambo Lolote

Mpendwa Rafiki yangu, Sisi wenyewe huwa tunachangia sana maisha yetu au sisi binafsi kuwa kama tulivyo leo. Kama ni mafanikio makubwa au hali ngumu kwenye maisha yetu sisi ndiyo tumekuwa chanzo namba moja. Hadithi ni nyingi sana kwenye maisha yetu. Kila mtu ana hadithi yake ambaye akikuelezea unaweza kujifunza kitu fulani. Tumepewa uwezo mkubwa na …

Kwenye Jambo Lolote Hakikisha Unakuwa Na Kitu Hiki

Mpendwa rafiki yangu, Mara nyingi kila kitu hapa duniani kinaongozwa na kanuni za asili. Huwa tunapokuwa tunakwenda kufanya kinyume na kanuni za asili, asili huwa inatuadhibu vibaya bila huruma. Kila kitu kwenye maisha yetu kinahitaji kiasi. Na kiasi ndiyo asili sasa ya dunia. Tunapozidisha sana asili huwa haituachi salama. Hebu angalia sana, yule anayekula sana …

Design a site like this with WordPress.com
Get started