Huwa tunadanganyika sana na mwonekano wa nje. Pale tunapoona mwonekano wa mtu wa nje au kazi anayofanya tunaweza kuhitimisha kwamba mtu huyo ni tajiri au ana hela.Utajiri ni kile kisichoonekana. Mtu anaweza kuwa na mali nyingi inayoonekana kama vile nyumba, mashamba na nk, lakini utashangaa mtu huyo huyo katika hali ya kawaida hana hela taslimu.Usidanganyike …
Jinsi Ya Kujua Dalili Za Mtu Kutaka Kukuumiza
Watu wanaotaka kunufaika dhidi ya wengine hufanya mambo kuonekana magumu. Watu wanapotaka kunufaika dhidi ya wengine, pale wanapotaka kutengeneza mfumo ambao unawanufaisha wao na kuwanyonya wengine, hufanya mambo ambayo ni rahisi kabisa kuonekana magumu. Kitu ambacho hata hakiitaji ukiritimba, utashangaa vile mtu anavyofanya mambo kuwa magumu.Anatengeneza ugumu wa kazi ili atumie nafasi hiyo kutengeneza mazingira …
Continue reading "Jinsi Ya Kujua Dalili Za Mtu Kutaka Kukuumiza"
Usijisahau Wewe Mwenyewe
Ni kawaida ya watu wengi kufanya kazi na kuwasaidia watu wengine lakini wao wenyewe hawajisaidii.Hii siyo nzuri, pale unapofanya kazi mtu wa kwanza kumkumbuka unapaswa kuwa wewe mwenyewe.Unapata hela, unawalipa watu wengine, lakini unajisahau hata kujilipa wewe mwenyewe. Watu watafurahia vile unavyowapa sasa lakini baadaye utakapokua huna nguvu za kufanya kazi hawatakukumbuka kama vile unavyowafanyia …
Njia Hii Inafanya Kazi
Rafiki, Watu wanapenda namba lakini hawapendi hesabu. Watu wanapenda matunda ya kazi yaani fedha lakini hawataki mchakato wa kazi. Habari njema ni kwamba, kwa mtu yeyote anayefanya kazi na kama kitu anakitaka kwenye maisha yake, lazima akipate kweli. Hii ni kwa sababu, inafanya kazi kama ukiifanyia kazi. Hakuna kitu ambacho hakifanyi kazi kama ukikifanyia kazi. …
Demokrasia Itakuchelewesha
Kama unataka mafanikio kwenye maisha yako binafsi, basi unapaswa kuondokana na demokrasia kwa sababu itakuchelewesha kwenye mambo yako mengi.Hata mwili wako binafsi ukiupeleka kwa demokrasia hauwezi kwenda. Yaani ukiusikikiliza sana mwili wako, huenda hata usikamilishe kile unachotaka kwenye maisha yako. Ili ufanikiwe, hutaki hiyari na maridhiano na kuweka demokrasia kwenye kila jambo, bali unahitaji kuwa …
Mfahamu Baba Wa Vitendo
Tokea uje duniani ulishawahi kuona mtu anapata tuzo ya kuwa mlalamikaji bora? Kuna namna fulani maisha yako hayaendi vile unavyotaka na unaona kila sababu ya kulalamika. Na habari njema ni kwamba, ukiwatafuta watu wa kuwalaumu kwa sababu ya maisha yako kuwa hivyo ulivyo leo, huwezi kukosa wako wengi tu. Swali la kujiuliza, nini haswa unapata …
Jinsi Ya Kushika Vitu Vingi Kichwani Na Kuvikumbuka
Changamoto mojawapo inayowasumbua watu wengi kwa sasa ni watu kukosa utulivu na hivyo kushindwa kushika vitu na matokeo yake kukosa kukumbuka vitu. Hata ukiangalia shuleni kwa sasa, watoto wengi wana changamoto ya kushika vitu na uwezo wa kutunza kumbukumbu. Iko njia nzuri ya kuweza kutatua changamoto hiyo nayo ni kurudia kitu unachotaka kikae kichwani na …
Continue reading "Jinsi Ya Kushika Vitu Vingi Kichwani Na Kuvikumbuka"
Ombeni Nanyi Mtapewa
Kwenye dunia hii, ukishindwa kwa sababu ya kukosa msaada ni kama vile kufa na kiu huku ukiwa kisimani.Pale unapoona mwenzako yuko bora kwenye kitu fulani, omba msaada akusaidie na wewe kuwa bora kama yeye. Kila kitu kinawezekana kama ukiiomba dunia. Usipoomba hupati.Wewe hujiulizi kwa nini Mungu alisema ombeni nanyi mtapewa? Iko wazi, hata wewe mwenyewe …
Kuwa Na Dhana Ya Ushindi Ndani Yako
Rafiki, Kiasili sisi binadamu ni watu wa mashindano. Kwa mfano, ukiwa unatembea au unaendesha gari, mtu akija kukupita utajikuta na wewe unaongeza mwendo ili mtu asikupite. Ushindani ndiyo asili ya binadamu. Ndiyo maana tuna ushindani kwenye kila eneo la maisha yetu. Ushindani ndiyo hali ambayo inawafanya watu wajitume na hata wengine kupata ridhiko ndani yao. …
Usiwe Na Hasira Na Hawa Watu
Kwenye haya maisha ukiwa mtu wa hasira, basi kila wakati utakuwa ni mtu wa kukasirika na hutaweza kuelewana na mtu.Kila mtu utamwona mbaya kwa sababu ya kushindwa kuendana na wewe. Tunapatwa na hasira pale ambapo sisi tunakuwa tunapata matokeo tusiyotarajia kutoka wengine. Lakini tukipata matokeo ambayo tunayotaka sisi wenyewe tunakua hatuna hasira. Hasira ni hisia …