Rafiki, Huwa tuna tabia fulani ya kukosoa kwenye maisha yetu. Wako watu ambao huwa hawaoni mazuri ya mtu hata siku moja. Hata mtu akifanya kitu, hata kiwe kizuri yeye ataona upande hasi.Katika falsafa ya Ustoa tumejifunza kwamba, kiasili kila kitu kipo sawa, hakuna kitu kizuri wala kibaya bali mtazamo wetu ndiyo unapelekea kitu kuonekana kizuri …
Watu Wananunua Kwa Sababu Hii Hapa
Rafiki, Kwenye mauzo, watu wananunua kwa sababu zao binafsi na siyo kwa sababu ya kukuonea wewe huruma kwenye kile unachouza. Huwezi kumkuta mtu amekaa zake, na kumwambia naomba ununue kwa sababu nataka nipate hela ya kumlipia mtoto ada.Watu wanapokuwa na mahitaji yao ndiyo yanawasukuma kununua. Watu hawanunui kwa sababu ya bei, wananunua kwa sababu ya …
Chagua Kimoja Kati Ya Hivi
Kwenye haya maisha ni bora uchague kimoja, upambane ushinde kweli au usipambane kwa uhakika uteseke kweli. Maandiko ya kiimani yanasema, ni heri kuwa moto au kuwa baridi lakini usiwe vuguvugu, maana kuwa vuguvugu ni kubaya kuliko hata kuwa baridi. Hata kwenye mafanikio pia, ni heri uweke juhudi zako zote kabisa na ufanikiwe kwa uhakika au …
Mauzo Ndiyo Njia Ya Maisha
Rafiki, Mauzo ndiyo njia ya maisha, mauzo ni hitaji muhimu la maisha, ili ule lazima uuze, na lazima pia watu wakuuzie kitu.Huwezi kukwepa mauzo kwenye maisha yako. Kila mtu anauziwa na anauza. Yaani UZA au utauziwa. Kama uko hai basi kuna kitu unauza, hakuna mtu ambaye anaendesha maisha yake bila kuuza. Kama kuna kitu kimoja …
Njia Rahisi Ya Kukuza Kipato Chako
Rafiki, Mtu ambaye ameondoka hapa duniani miaka 2 iliyopita, akifufuka leo atakutana na mabadiliko makubwa sana.Mabadiliko yanatokea kwa kasi sana, kama mabadiliko yanatokea na sisi pia tunapaswa kubadilika ili kunufaika na mabadiliko yanatokea. Na kuwa mbele kwa mabadiliko yanatokea ndiyo fursa kubwa lakini ukiwa nyuma ya mabadiliko inakuwa hasara. Gharama za maisha zimekuwa juu ni …
Ukiwa Na Maandalizi Lazima Utakutana Na Bahati
Rafiki yangu nikupendaye, Sisi binadamu ni miongoni mwa viumbe ambavyo tumebarikiwa sana. Hongera sana kwa kustahilishwa na kuwa na baraka hizo. Kila mmoja wetu tayari ana baraka ndani yake. Yaani kitendo tu cha mimba yako kutungwa, tayari una baraka. Maana rahisi ya baraka ni nguvu ya asili ya kutenda miujiza ambayo ipo kwa kila mmoja …
Continue reading "Ukiwa Na Maandalizi Lazima Utakutana Na Bahati"
Miaka 20 Ijayo
Mchekeshaji Mark Twain aliwahi kunukuliwa akisema, miaka 20 Ijayo utajutia zaidi vitu ambavyo hujafanya leo kuliko vitu ambavyo umevifanya. Acha kuahirisha kufanya vitu kwa sababu yoyote ile kwa sababu baadaye utakuja kujuta zaidi. Acha kuogopa changamoto au kushindwa na jaribu vitu vingi uwezavyo. Ni bora ukashindwa ukiwa umejaribu, kuliko usifanye kabisa halafu ukajiambia umeshindwa. Usisubiri …
Mawimbi Yakitulia Ndiyo Tutajua Nani Anaoga Uchi
Ni kauli ya Bilionea na mwekezaji Warren Buffett. Maana halisi ya hii kauli ni kama vile kusema, muda ukifika utasema ukweli wote. Mtu anaweza akakuambia kitu kwamba anafanya na kumbe hafanyi lakini muda ukifika matokeo yataonekana tu.Mawimbi yakitulia ndiyo tutajua nani anayeoga uchi. Mtu anaweza kukuambia yeye ni mwaminifu lakini ukitaka kuamini hilo, subiri mawimbi …
Continue reading "Mawimbi Yakitulia Ndiyo Tutajua Nani Anaoga Uchi"
Tambua Michango Ya Watu Wengine
Rafiki, Hakuna jeshi la mtu mmoja kwenye maisha yako. Isifikie mahali ukasema umefika hapo ulipo wewe mwenyewe. Kuna watu ambao wamekusaidia wewe kufika hapo ulipo. Tambua michango ya watu wengine kwa namna ambavyo wamekusaidia wewe hapo ulipo sasa. Wako ambao wanafanikiwa kwa bahati, kwa sababu bahati nayo inahusika katika mafanikio lakini hujaipata bahati hiyo bure …
Epuka Kuwa Mzigo Kwa Wengine
Rafiki, Sehemu yoyote ile unayokuwepo, penda kuonekana mtu wa msaada na siyo mzigo.Kuwa mzigo ni ile hali ambayo watu wanakuona kama vile huna thamani.Mtu ambaye hana thamani maana yake ni mtu ambaye hana mchango anaotoa sehemu fulani. Kuwa mtu wa thamani na siyo mzigo.Anzia kwa mwenza wako, asikuone ni mzigo kuwa na wewe bali akuone …