Jinsi Ya Kuwa Bora Kwenye Zama Za Mambo Mengi

Rafiki, Muda tulionao ni mchache sana ukilinganisha na mambo ya kufanya. Lakini, Seneca aliwahi kunukuliwa akisema, tuna muda mwingi mpaka tunautumia katika mambo yasiyo kuwa na maana. Hii ina maana kwamba, mtu hawezi kusema hana muda kufanya jambo lenye maana kwake wakati anao muda wa kufanya mambo yasiyo na maana kwake. Katika zama hizi za …

Hujazaliwa Kwa Ajili Yako

Rafiki, Hujazaliwa peke yako, bali umezaliwa kwa ajili ya wengine.Kama uko hai, ni kwa sababu unatakiwa kuwasaidia wengine.Kuna watu wanakuhitaji wewe, ili wao waendelee kuishi. Maisha ni ushirikiano. Watu wanategemeana, peke yako huwezi. Bado unahitaji wengine ili kufanikiwa. Timu ya mpira wa miguu nchini Uingereza Liverpool FC, wana kauli mbiu yao inayosema, you can't walk …

Kama Hupati Matokeo

Rafiki, Siku zote njia sahihi lazima ilete majibu sahihi. Kama unaona hupati matokeo basi kuna kitu hiki;Njia unayotumia siyo sahihi auUnafanya kwa namna ambayo siyo sahihi. Ili upate matokeo mazuri kwenye kile unachofanya, hakikisha njia unayotumia ni sahihi. Wote tulisoma katika hisabati kwamba, njia sahihi lazima ilete jibu sahihi.Kama unatumia njia sahihi kufanya hesabu na …

Jinsi Ya Kufika Pale Unapotaka Kufika

Rafiki, Ukiwa unatoka nyumbani na unataka kwenda kazini huwezi kukaa chini na kufikiria kwamba utafikaje kazini.Ni kitendo tu cha kutoka na kuanza mchakato wa kwenda kazini. Huenda unajiuliza, je, utafikaje kule unakotaka kufika? Jibu ni anzia hapo ulipo sasa. Hakuna mtu ambaye hana mahali pa kuanzia. Kwa sababu unapumua, kitendo tu cha kupumua ni mahali …

Hakuna Kushindwa Bali Kuna Hiki Hapa

Kwenye maisha chochote kile unachofanya na matokeo yoyote yale utakayoyapata ni ushindi kwako. Kwa nini ni ushindi kwa sababu umepata mahali pakuanzia na kuboresha kitu.Matokeo yoyote yale utakayoyapata, utayatumia kuboresha kule unakotaka kwenda. Kama huna matokeo yoyote yale utakosa pa kuanzia.Ni bora ufanye na matokeo yoyote yale utakayoyapata, utayatumia kuboresha zaidi kule unakotaka kwenda. Mafanikio …

Mtu Anayekupenda

Mtu anayekupenda kweli kutoka moyoni, hawezi kukuangusha hata siku moja.Atajitoa kwako kwa hali na mali. Upendo wa kweli hauna kipimo. Mtu anayekupenda anakuwa hana kipimo ndani yako.Mtakatifu Agustino wa Hippo aliwahi kunukuliwa akisema, kipimo cha upendo ni kupenda bila kipimo. Mtu anayekupenda atakupenda bila kipimo. Ukiona mtu anakupenda kwa masharti, jua hapo hakuna kipimo. Tujifunze …

Waondoe Watu Hawa Kwenye Orodha Yako

Rafiki, Dunia inaendeshwa kwa misingi ya nipe nikupe, nikune nikukune. Hivyo basi, wewe unataka kupata kitu fulani, hakikisha na wewe unatoa kitu fulani ili ukipate. Usitegemee kupokea kama hutoi. Kuna aina ya watu ambao una husiana nao, wako wako kama kupe tu. Ni watu ambao wanapenda kupokea kutoka kwako lakini ni wagumu kutoa. Waondoe wote …

Kama Inafanya Kazi

Kama inafanya kazi, rudia tena kuifanyia kazi.Ndiyo, rudia tena kuifanyia kazi. Kama umekutana na kitu chochote kile ambacho kinafanya kazi rudia tena kwa kufanya zaidi ili upate matokeo. Tunakuwa na mbinu mbalimbali za kutusaidia katika maisha yetu, pale unapokutana na kitu ambacho kinafanya kazi, shukuru na endelea kukifanyia kazi zaidi. Kwa mfano, wewe kama ni …

Jua Hiki Ili Usipigwe Hela

Rafiki, Iko hivi, udhaifu wako ndiyo mtaji kwa wengine.Udhaifu wako ndiyo unawapa watu fedha. Na katika hali ya kawaida, kila mtu ana udhaifu wake.Na hakuna kitu kizuri kama kujua udhaifu wako uko wapi ili uweze kujidhibiti au kukabiliana nao. Jua udhaifu wako uko wapi ili watu wasitumie udhaifu wako kupiga hela. Unachopaswa kujua ni wapi …

Kama Unajua Unapokwenda, Dunia Itakupisha

Rafiki, Kabla hujaanza safari ya mafanikio makubwa, unaweza kuona mambo ni rahisi. Lakini, mambo siyo rahisi kama unavyofikiria. Pals unapopanga kufanikiwa na kupiga hatua zaidi kwenye maisha yako, ndipo vikwazo vya kila aina vinaibuka. Na dunia inafanya kwa nini? Dunia inafanya hivyo kwa sababu ni njia ya kukupima kama kweli umejitoa kufanikiwa au unazingua tu. …

Design a site like this with WordPress.com
Get started