Kuna vichekesho nimekutana navyo mtandaoni, huenda hata wewe umeviona.Kulingana na mambo ya dunia yanavyoendelea, vichekesho hivyo vinasema, dunia simama nishuke. Wakiwa na maana kwamba, kwa mambo yanayoendelea duniani, ni watenganayo ili waiache. Dunia ina mambo mengi, tokea enzi na enzi, huwezi kuidhibiti dunia. Bali unaweza kujidhibiti wewe mwenyewe. Kuwa mtu sahihi katika dunia yenye watu …
Usijipe Msongo
Mambo tuliyonayo tayari ni mengi. Muda wa kufanya vitu hivyo nao ni mchache. Tunao muda wa kufanya vitu ambavyo ni muhimu tu. Lakini, usijipe msongo na mambo haya. Usijipe msongo kwa mambo ambayo yako nje ya uwezo wako. Usijipe msongo kwamba wewe ni kiranja wa dunia. Kwamba unataka watu waishi kama vile unavyotaka wewe. Usije …
Njia Rahisi Ya Kushinda Mabishano
Mwanamafanikio, Kiasili sisi binadamu ni wabinafsi. Tunapenda kuona mambo yetu ndiyo ya muhimu kuliko ya wengine. Sasa katika suala kubishana, ni kila mmoja anapenda kushikilia msimamo wake.Hakuna anayependa kuonekana mjinga kwenye kile anachokiamini. Mabishano mengi ambayo tunayokutana nayo, mengi hayana mashiko.Hakuna mtu anayeweza kukubali ashindwe kwenye kile anachokiamini.Kila mtu anapenda kuona ni BORA. Njia rahisi …
Muda Mzuri Wa Kufanya
Rafiki, Supu ni tamu pale inapokuwa ya moto.Supu ikipoa, inakuwa haina tena ile ladha ya supu. Na vile vile katika maisha yako, muda mzuri wa kufanya kitu ni pale unapokuwa na hamasa ya kufanya kitu hicho. Pale unapokuwa na wazo, hapo hapo lifanyie kazi kabla halijapoa. Ukimfikiria mtu na ukamkumbuka, usiseme baadaye, chukua hatua na …
Usifanye Kitu Kwa Makubaliano Haya
Jambo lolote unalofanya , hakikisha kila upande unapata ushindi. Makubaliano hatari zaidi ni yale ya wewe kujali maslahi yako kwanza bila kujali maslahi ya upande wa pili. Kitu chochote ambacho unafanya na mtu mwingine, hakikisha mmeelewana vizuri, kuweni na utaratibu ambao upo wazi na kila mtu ajue majukumu yake na matarajio ya mwenzake. Usifanye kitu …
Usiharakishe Kufanya Maamuzi
Kwa kila maamuzi unayofanya, usiharakishe Kufanya maamuzi. Jipe muda wa kutafakari na kujifunza kabla hujaamua ni hatua zipi unazochukua. Unapokuwa una jambo, kuwa mtu wa kutulia na kufikiria namna ya kufanya maamuzi. Usiwe mtu wa kukurupuka, fikiria kwanza kabla kabla hujafanya maamuzi. Usiongozwe na hisia, jitahidi kufanya maamuzi wakati ukiwa na akili iliyotulia.Mwisho, usiharakishe Kufanya …
Kikubwa Uzima
Kama umeamka na kujikuta unapumua, ni jambo la kushukuru.Hata kama mambo yote hayajaenda vile ulivyokuwa umepanga, kama unapumua unapaswa kushukuru kwa sababu wako watu wengi walitamani kupumua lakini leo wameshakufa. Ni vizuri kufurahia ushindi wa uhai, lakini kusherekea uhai bila kuutumia kuzalisha hiyo inakuwa siyo sawa. Watu wengi wamekuwa wanajifisha kwenye mwamvuli wa kushukuru uzima …
Usihukumu Kabla Hujajua Kwa Nini Ya Mtu
Watu wanakuwa na mipango yao kichwani, pale wanapokuwa wanataka kufanya kitu, unaweza kuwahukumu kwa namna unavyoona wewe. Watu wanakuwa na kwa nini zao mwanzoni.Wanapoanza kufanya kitu, unaweza usiwaelewe kabisa.Unaweza kuwahukumu kwa kile wanachofanya. Lakini, usiwahukumu watu kabla hujajua kwa nini yao ya ndani.Watu wanakuwa na kwa nini zao. Kwa nini zinazowaongoza kufanya kitu. Usiwe mtu …
Jinsi Ya Kupata Faida Kwenye Biashara Ndogo
Rafiki, Faida kwenye biashara ndogo ipo kwenye kununua au kuzalisha. Biashara nyingi ndogo huwa ni za reja reja au za kuzalisha bidhaa ambazo hazina tofauti kubwa kwa nje. Hivyo bei huwa hazitofautiani sana. Hii hupelekea ushindani kuwa mkali kwenye bei, kila mtu anaweka bei itakayovutia wateja na hilo kusababisha faida kuwa ndogo. Ili kupata faida …
Continue reading "Jinsi Ya Kupata Faida Kwenye Biashara Ndogo"
Vuta Watu Wa Aina Hii
Kila mmoja wetu ana kitu cha kipekee ndani yake. Jinsi unavyoishi na watu, ndivyo unavyowavuta watu wanaofanana na wewe.Ishi maisha ambayo yanagusa wengine.Ishi maisha ya msaada, wasaidie wengine kupitia kile unachofanya.Watu wakifanikiwa, hawatakuacha. Tengeneza jina, tengeneza marafiki ambao ukiwa na jambo lako ni rahisi kukusaidia.Wavute watu wako kwa upendo nao watavutika.Usitumie mabavu kuwavuta watu, bali …