Kama Siyo Muhimu Usiongee

Kwenye maisha usiwe muongeaji sana. Ongea yale ambayo ni muhimu tu. Unapoongea sana, utajikuta unaongea yale yasiyokuwa na maana.Kama watu walikuwa wanakuheshimu, wanaweza kukushusha kwa yale unayoongea. Hata mpumbavu akikaa kimya, huwa anaonekana mwenye hekima. Ongea kama ni muhimu tu na kama siyo muhimu usiongee. Changia pale unapoona usipochangia mambo yataenda kuwa vibaya. Mara zote …

Usiogope Kushindwa

Kama bado hujapata kile unachotaka, endelea kuweka kazi. Usiishie njiani, atafutaye hachoki na akichoka ameshapata. Je, wewe unataka kuchoka umeshapata?Pambana ufanikiwe na mafanikio yako yatafuta kabisa kushindwa kwako ambako umepitia. Ni kupitia kushindwa ndiyo utafanikiwa na ukishafanikiwa hakuna atakayekumbuka yale uliyoshindwa. Hatua ya kuchukua leo; Nenda kawaoneshe wale wote ambao wanakuambia umeshindwa kwa kufanikiwa zaidi. …

Vitu Viwili Vya Kuzingatia Kwenye Mauzo

Biashara nyingi zinakabiliwa na changamoto ya MAUZO. Na matatizo yote kwenye biashara yanatatuliwa na kitu kimoja tu nacho ni mauzo. Mauzo ndiyo suluhisho la matatizo yote kwenye biashara. Kama unataka kipato zaidi, ongeza mauzo zaidi. Kama unataka watu wazuri, ongeza mauzo na utawapata watu wazuri kwa kuwaajiri. Ili kuongeza mauzo hakikisha unapata wateja wapya kila …

Mtu Anayependa Wengine Wafanikiwe

Mtu aliyefanikiwa, huwa anapenda wengine wafanikiwe. Ni mtu asiyefanikiwa, ndiyo huwa hapendi kuona wengine wakipiga hatua. Mtu aliyefanikiwa kwa njia sahihi, huwa anapenda kuwawezesha wengine kupiga hatua.Huwa wanapenda kuwaelimisha wengine mbinu za kufanikiwa zaidi. Wakati mwingine huwa wanajitoa kwa ajili ya wengine pasipo hata kulipwa ili watimize lengo lao la kuona watu wanafanikiwa. Kuwa mtu …

Jinsi Ya Kuiona Hela Kwenye Maisha Yako

Kwenye kitabu cha Mhubiri 10 mstari wa 19 anasema, fedha ni jawabu la mambo yote. Hilo halina mjadala. Kinachofanya fedha iishe,ni matumizi. Na hatuwezi kuzuia matumizi kwa sababu tunafanya kazi ili kazi itusaidie. Fedha inatusaidia kulipa bili mbalimbali.Ili uweze kuiona hela fanya yafuatayo.Kwanza dhibiti matumizi, kumbuka kinachomaliza fedha zako ni matumizi. Na hapa nazungumzia matumizi …

Kabla Hujafanya Chochote Elewa Kwanza Hii Dhana

Rafiki, Watu wanafeli kwenye maeneo mengi ni kwa sababu ya kukosa kitu kimoja. Nacho ni kushindwa kuelewa vizuri kile wanachopaswa kufanya. Wanafunzi wanafeli mitihani siyo kwamba hawajui bali, hawajaelewa vizuri maelekezo ya swali yanataka nini. Kama ulishawahi kusikia kwenda Chaka, wengi tu kwenye maisha yetu tunaenda Chaka.Kama mitihani ya shuleni ulishawahi kwenda chaka hata kwenye …

Fanya Hivi, Utaona Matokeo

Rafiki, Kama unataka kupata matokeo mazuri, fanya kitu kwa undani. Yaani ingia maziwa, go all in. Usifanye kitu juu juu, yaani mguu mmoja ndani na mguu mmoja nje. Ukiamua kufanya kitu, fanya kwa uwezo wako wote. Kufanya kitu huku ukiwa umejitoa mguu mmoja ndani na mwingine nje huwezi kuona mafanikio ya kitu. Kama umeamua kufanya …

Matokeo Yanaonekana

Mwanamafanikio, Kama unafanya kazi, dunia inaona. Kama unacheza dunia inaona. Warren Buffett aliwahi kunukuliwa akisema, mawimbi yakitulia, tutajua nani alikuwa anaoga uchi.Ikiwa na maana kwamba, kama unafanya kazi kweli au hufanyi, matokeo yataonekana. Kama unafanya kazi au hufanyi kazi, matokeo hayadanganyi kabisa. Tufanye kazi, kila mtu afanye kile anachopaswa kufanya.Pambana kupata ushindi, ushindi ndiyo matokeo …

Jinsi Ya Kujitambulisha Kwa Sekunde 30

Rafiki, Umakini wa watu umeshuka sana katika zama hizi. Hivyo watu hawana muda wa kusikiliza kwa muda mrefu kama hutafanikiwa kuteka akili zao. Pale unapokutana na watu, unapaswa ujitambulishe vizuri ili watu wakujue wewe ni nani, unafanya nini. Ukipata fursa ya kuonana na watu wengi, jitambulishe vizuri na kuibua shauku kwa watu wengine kukutafuta kwa …

Utakumbukwa Kwa Lipi?

Hautakumbukwa kwa namna ulivyogusa maisha yako binafsi, bali namna ulivyogusa maisha ya wengine. Umezaliwa kuja kugusa maisha ya wengine kupitia kile unachofanya. Fanya kila unachoweza, kuishi vizuri na watu kiasi kwamba hata siku haupo duniani, ukumbuke maisha yake. Kuna watu wengi wamekufa unaowajua, lakini leo hii unawakumbuka sana wale ambao waligusa maisha yako. Yaani ukikaa …

Design a site like this with WordPress.com
Get started