Rafiki yangu nikupendaye, Kamwe usiseme fedha hakuna, fedha zipo.Fedha hakuna kwako kwa sababu moja tu, huna unachouza au huna thamani unayotoa. Ukijikuta huna fedha, tafuta kitu cha kuuza na utapata fedha.Au wasaidie watu kupata kile wanachotaka na wewe utapata kile unachotaka. Kwa lugha rahisi ni kutoa thamani. Bahari hata siku moja kuwa haishiwi maji kwa …
Usijidogishe
Rafiki, Kuna watu wameshajistahilisha kwamba, wanaweza kufanya kitu fulani au wao ni watu wa kupata daraja fulani. Watu wamejiwekea ukomo kwa kauli hii kwamba, hawawezi kufanya kitu fulani au hawawezi kumiliki kitu fulani kwa sababu uwezo wao ni mdogo. Wamejipa mamlaka ya chini, wamejidogisha kiasi kwamba hawawezi kufanya kitu. Kilichobakia ni kupokea kile kidogo ambacho …
Jifunze
Rafiki, Jifunze namna ya kuandika vizuri, kiasi kwamba mtu akisoma ujumbe wako anaelewa na kuchukua hatua. Jifunze namna ya kuongea vizuri, ongea vizuri kiasi kwamba kile unachoongea kinaeleweka na watu.Usiongee kitu ambacho unakielewa wewe mwenyewe.Chochote kile unachoongea, ongea kwa lugha rahisi kiasi cha kueleweka. Jinsi unavyowasiliana na watu wasiliana nao vizuri. Ujumbe wako unapaswa kunasa …
Acha Mambo Yatokee
Rafiki, Hapa duniani kuna mambo ya aina mbili;Moja ni yale ambayo yako ndani ya uwezo wako. Yaani haya ni yale ambayo unaweza kuyadhibiti. Mbili ni yale ambayo yako nje ya uwezo wako. Haya ni yale mambo ambayo huwezi kuyadhibiti. Usijipe msongo wa mawazo kwa jinsi mambo yanavyotokea.Mambo yanatokea kama yalivyopangwa.Hivyo acha mambo yatokee kama yalivyopangwa …
Angalia Hapa Kama Unataka Kufika Mbali
Siku moja mtu mmoja alikuwa anawaangalia wale watu ambao wanatembea juu ya kamba. Baada ya mchezo kuisha, alienda kumuuliza maswali yule aliyekuwa anatembea juu ya kama na kumuuliza.Unawezaje kutembelea juu ya kamba na kuwa na "balansi"? Akamjibu na kumwambia,Ukitaka kupata balansi ya mchezo, usiangalie pale ulipo, bali angalia kule unakotaka kufika. Hii ina maana gani …
Huwezi Kufanikiwa Kwenye Maisha Kama Unafanya Kazi
Rafiki yangu nikupendaye, Huwezi kufanikiwa kwenye maisha kama unafanya kazi. Watu wanaopenda wanachofanya huwa hawafanyi kazi. Kwa nini huwezi kufanikiwa kwenye maisha kama unafanya kazi? Kwa sababu kazi inachosha, kazi ni mzigo na kila mtu anapenda kukimbia kazi. Utafanikiwa kwenye maisha yako, kama unafanya unachopenda kufanya. Kupenda unachofanya inakuwa siyo kazi tena.Bali kwako inakuwa kama …
Continue reading "Huwezi Kufanikiwa Kwenye Maisha Kama Unafanya Kazi"
Matatizo Mengi Yanaanzia Hapa
Rafiki yangu, Watu wazuri au wabaya kwenye jambo fulani wanaanzia katika familia.Ni pale wazazi au walezi kushindwa kuwajibika ipasavyo kwenye majukumu yao. Wale ambao tunawaona ni bora sehemu fulani, ubora wao haujaja kama mvua, bali ubora wao uliandaliwa. Kila mzazi au mlezi, anapaswa kuwajibika ipasavyo kwa mtoto/watoto alionao.Mzazi/mlezi unapaswa kufundisha, kukemea na hata kukaripia kwa …
Poteza Ili Upate
Rafiki, Huwezi kupata kile unachotaka, kwa namna unavyokitaka, kwa wakati unaotaka. Kuna wakati utahitaji kupoteza kitu fulani ili kupata kile unachotaka. Lazima uwe tayari kujitoa kwa ajili ya wengine, wakati mwingine ukose au kupoteza vitu kwa ajili ya wengine. Unahitaji kuona umuhimu wa wengine na kujitoa kwa ajili yao, ndiyo uweze kufanikiwa. Kama una kikombe …
Acha Hii Tabia Kuanzia Sasa
Huwa tunaangalia sana upande hasi wa matokeo tunayopata kuliko upande wa chanya wa matokeo mazuri tunayopata.Unaweza kupata matokeo mazuri sana, ukaishia kufurahia tu, lakini siku ukipata matokeo hasi, unakosa shukurani. Tabia ya kulalamika, ni tabia ya umasikini. Hutakiwi kulalamika hata kama mambo hayaendi vizuri, furahia yale mazuri mengi ambayo unaendelea kuyapata. Kulalamika kunafunga milango ya …
Kama Ni Kweli, Badilika
Marcus Aurelius aliyekuwa mtawala wa Roma na mwanafalsafa wa Ustoa, ana maneno mazuri kwetu kuhusu ukweli. Watu huwa wanafikiri, ukweli unawaumiza watu, lakini kiuhalisia, ukweli haujawahi kumuumiza mtu. Bali, ukweli huwa unamsaidia mtu. Wengi wetu huwa hatupendi kuambiwa ukweli, hasa pale ambapo ukweli unatufanya tuonekane tumekosea au tupo upande tofauti. Lakini Marcus anatuambia kama ukweli …