Kwenye haya maisha hakuna kitu kizuri kama kuishi kwa amani. Tunaweza kuwa na kila kitu, lakini maisha yetu yakawa hayana maana kama tu tumekosa Amani ya ndani ya maisha yetu. Amani hii hailetwi na vile tulivyokuwa navyo bali Amani hii inakuja kwako pale unapojua maana ya mafanikio kwenye maisha yako.Watu wanaopata shida ni wale ambao …
Kama Unataka Kuuza Fanya Hiki
Kila biashara inataka ukuaji. Moja ya sifa ya viumbe hai ni kukua. Hivyo biashara nayo ina sifa ya ukuaji. Na kama kitu hakikui, maana yake hakuna uhai.Kama biashara haiendi mbele, maana yake inarudi nyuma.Hakuna kusimama. Kwenye biashara, zoezi la kuongeza wateja wapya linapaswa kufanyika mara zote. Sababu ya biashara nyingi KUTOKUUZA ni kwa sababu ya …
Usikubali Mteja Huyu Akukwamishe
Kwenye maisha ili ukue lazima ukuaji wako utawakera baadhi ya watu.Wale ambao wanapenda mambo ya kawaida, watependa kukuona ukiwa pale pale kila siku. Kuna watu huwa hawapendi kitu kinachoitwa mbadala kwenye maisha yao.Wanapenda kuwa katika hali fulani ya kuridhika(comfort zone).Mtu ambaye yuko katika hatua hii, hapendi tena ukuaji anataka kubaki na kile ambacho ameshazoea kukipata. …
Vitu Ambavyo Tunapenda
Rafiki, Vitu ambavyo watu huwa wanavipenda na vinawapa manufaa mazuri kwao, huwa hawakosi muda wa kuvifanyia kazi. Mtu ambaye haoni umuhimu au thamani ya kitu, hawezi kupata muda wa kitu hicho.Kama kitu kinakupa matokeo, maana yake ni kizuri na utaendelea kukifanya. Mara nyingine licha ya kujua vitu muhimu vya kufanya, bado watu wanafanya vitu ambavyo …
Hoji Kila Kitu Kupata Ukweli
Usiwe mtu wa kukubaliana na kila jambo kirahisi bila kuhoji. Uwe mtu wa kufanya udadisi, peleleza mpaka ujue ukweli na kisha fanya maamuzi. Ukishakuwa na taarifa sahihi, zitakusaidia kupata majibu sahihi na kufanya maamuzi. Vitu vingi ambavyo watu wamezoea kufanya siyo sahihi. Ni rahisi kukubali kufanya kitu kwa sababu kila mtu anafanya, na kuona kwa …
Hisia Na Fikra
Kwenye maisha kila kitu kina mtegemea mwenzake.Kiasili, tumeumbwa kwa ushirikiano.Kwa mfano, mwili unafanya kazi kwa ushirikiano. Mfano, mikono, miguu na nk. Vile vile kama binadamu, unahitaji kuwa na hisia na fikra. Huwa tunafanya maamuzi kwa hisia, halafu tunakuja kuhalalisha kwa fikra. Hisia na fikra ni vitu ambavyo vinakwenda pamoja.Mtu asipokuwa na hisia ni shida, na …
Kama Hujajua Hili, Utateseka Sana
Rafiki, Kwenye haya maisha usipojua maana ya mafanikio kwako, utaishia tu kuteseka. Usipojua maana ya mafanikio kwako, maisha yanakuwa hayana maana kwako. Kazi yako kubwa kama binadamu ni kujua maana ya mafanikio kwako na utaishi kwa amani. Kuna lile ridhiko kwako unalolipata baada ya kujua maana ya mafanikio kwako. Unaweza kumuona mtu kwa nje amefanikiwa …
Nafasi Ambayo Hupaswi Kuichezea
Rafiki, Kwenye maisha, chochote kile ambacho umeamua kufanya, basi kifanye kwa moyo kiasi kwamba wale ambao wanakutegemea kwenye eneo hilo, wakufurahie. Timiza wajibu wako, ukipata nafasi fulani, itumie nafasi hiyo vizuri. Hata yule aliyekupa nafasi aje akushukuru baadaye. Mpe mtu thamani kubwa, kiasi kwamba aone anadeni kwako.Watu wakusimulie kwa mazuri na siyo mabaya. Acha alama …
Ukijua Vitu Hivi Viwili Utafanikiwa
Rafiki, Kwenye maisha yetu, kile kinachotupa ushindi ni uwezo wetu wa kukamilisha jambo. Kama hatukamilishi jambo, maana yake hakuna ushindi utakaotokea. Ukitaka ushindi, tokea unaamka asubuhi, hakikisha unaanza kukamilisha kitu.Kitendo tu cha kuamka na kutandika kitanda chako, ni ushindi mkubwa. Kama unataka ushindi wowote kwenye maisha yako, hakikisha unakuwa mkamilishaji mzuri wa kile ambacho umekipanga. …
Jua Kila Kitu Kabla Ya Kuwekeza
Kwenye uwekezaji, jua kila kitu kabla hujawekeza. Popote unapotaka kuwekeza fedha yako, hakikisha unafanya kazi moja kubwa ya kujua kila kitu kinachohusiana na pale unapowekeza. Usiwekeze kwa sababu watu wanasema ni uwekezaji mzuri, usiwekeze kwa sababu kila mtu anawekeza, bali jipe muda wa kujifunza kwa undani kuhusu uwekezaji wowote unaotaka kufanya. Katika kitu ambacho unapaswa …