Kuna kitu ambacho kinataofautisha maisha yetu kuanzia kila eneo la maisha yetu. ili maisha yetu yaweze kuonekana vizuri basi kuna nguvu inayotusukuma kuwa hivyo. Tukitaka kuwa watu makini basi tunatakiwa tujenge urafiki na nidhamu. Maisha yetu yanakuwa hayana uhuru kama yakikosa kuwa na nidhamu. Hakuna uhuru pasipo kuwa na nidhamu. Maisha yetu yamekosa uhuru kwa …
Hakuna Kazi Ngumu Kama Hii Kwenye Maisha Yako
Natumaini kila mmoja wetu anafanya kazi. Kazi ndiyo msingi wa maendeleo na hata imeandikwa kuwa asiyefanya kazi na asile. Na mara nyingi hata kazi tunazozifanya huwa tunaona matokeo yake lakini kuna kazi nyingine ni ngumu kweli na inahitaji moyo wa kuendelea kufanya. Tunaweza kujiuliza je ni kazi gani hiyo? Je kazi ngumu ni ipi kubeba …
Continue reading "Hakuna Kazi Ngumu Kama Hii Kwenye Maisha Yako"
Kama Ukijua Kitu Hiki Umeshatatua Matatizo Yako Yote
Kama uko hai maana yake unaendelea kuvuta pumzi hivyo binadamu yoyote ambaye yuko hai hawezi kukosa changamoto. Kama huna changamoto maana yake huna kitu kikubwa unachofanya. Kama una mambo makubwa unayafanya lazima yatakuchangamotisha. Mara nyingi kama unaishi kila siku maisha yale ya kimazoea ni ujinga kwa sababu hakuna jipya unalojifunza. Kuna zile changamoto unazojipa wewe …
Continue reading "Kama Ukijua Kitu Hiki Umeshatatua Matatizo Yako Yote"
Zawadi Inayodumu Kuliko Zawadi Zote
Maisha ni kuacha alama hapa duniani. Maisha ni kugusa watu wengine hapa duniani, hatujaja duniani kujiangalia sisi ila tumekuja duniani kwa ajili ya wengine. Kila mmoja amekuja kujaza nafasi yake katika hii dunia, tumekuja kukamilishana, kila mtu ana nafasi yake na uzuri ni kwamba dunia bado haijaja kabisa inahitaji watu waendelee kuijaza. Ule msemo wa …
Huyu Ndiye Adui Mbaya Wa Mafanikio Yako Yoyote Yale.
Yuko adui ambaye anatufanya turudi nyuma badala ya kwenda mbele. Ni adui hatari sana kiasi kwamba ukiwa naye katika maisha yako lazima utaanguka tu kama siyo kubaki hapo hapo ulipo. Maisha yetu ni safari na kama tunavyojua safari ina mambo mengi na mwisho wa safari ni pale tutakapokuwa tunavuta pumzi yetu hapa duniani na habari …
Continue reading "Huyu Ndiye Adui Mbaya Wa Mafanikio Yako Yoyote Yale."
Tegemea Fedha Zote Lakini Siyo Hii Hapa
Linapokuja katika suala la fedha, fedha ambayo uko nayo mkononi mwako ndiyo una uhakika nayo. Lakini pesa ambayo haiko mikononi mwako siyo kabisa ya kuitegemea hata siku moja. Huwa tunapanga mipango mingi kwa kutegemea pesa ambazo haziko mikononi mwetu, tunaweka bajeti mbalimbali na muda mwingine tunawaahidi watu wetu wa karibu nitakupatia kiasi fulani cha pesa …
Hata Kama Ni Mtoto Wako Wa Kumzaa Usimfanyie Kitu Hiki
Watoto ni zawadi kutoka kwa Mungu. Wote ambao tuko hai sasa hivi hatujawahi kuandika barua ya kuomba kuzaliwa na tena hatujawahi hata kuomba kuzaliwa na wazazi fulani lakini sisi wote tumejikuta tumezaliwa na wazazi ambao tunao sasa. Hakuna zama ambazo zinasumbua katika changamoto za malezi kama hizi, hii ni kwa sababu ya dunia inazidi kukua …
Continue reading "Hata Kama Ni Mtoto Wako Wa Kumzaa Usimfanyie Kitu Hiki"
Jinsi Ya Kupata Bahati Katika Maisha Yako
Njia nzuri ya kutaka kupata bahati katika maisha yetu ni kujiandaa tu. Hakuna njia nyingine kwa sababu bahati yoyote inakuja pale inapokutana na maandilizi. Kama ulijiandaa kukabiliana na mabadiliko mapema kabla ya mabdiliko kutokea basi yakija kutokea utajiona mwenye bahati. Watu wanaweza kukushangaa katika maisha yako una bahati kiasi gani kumbe ni maandalizi uliyofanya wewe …
Continue reading "Jinsi Ya Kupata Bahati Katika Maisha Yako"
Hakuna Hatari Mbaya Katika Masuala Ya Kifedha Kama Hii Hapa
Hata kama wewe ni mzalishaji mzuri kiasi gani lakini ukikosa kuishi na kufuata misingi ya fedha lazima utashindwa. Tuna watu wazuri wanaopambana kila siku kuhakikisha wanapata kile wanachokitaka lakini tumekuwa na watu ambao wanaishi kinyume na kile wanachokifanya. Hakuna hatari mbaya katika masuala ya kifedha kama kuishi juu ya kipato chako. Hata kama wewe ni …
Continue reading "Hakuna Hatari Mbaya Katika Masuala Ya Kifedha Kama Hii Hapa"
Jinsi Unavyojikatisha Tamaa Wewe Mwenyewe
Kama tunaishi maisha ya kujilinganisha ni rahisi kujiona maisha yetu kuna kitu yamekosa na ya wengine ndiyo yamekamilika. Kumbe tungejua ya kuwa kila mtu ana maisha mazuri kama akiwa anaishi maisha yake. Pale tunapoanza kujiona sisi hatuna hiki na fulani anacho tunaanza kupoteza ladha ya maisha na kuweka maisha yetu katika thamani ya vitu. Kila …
Continue reading "Jinsi Unavyojikatisha Tamaa Wewe Mwenyewe"