Jinsi Ya Kupata Fedha Zaidi

Mpendwa rafiki, Fedha ni mbadilishano wa thamani. Je unatoa thamani gani?  katika dunia ya sasa mtu unalipwa kadiri ya thamani unayoitoa sokoni kama huna thamani unayoitoa hutoweza kupata fedha. Fedha ni ngumu kupatikana, tunatumia nguvu, muda na tunaipata kwa jasho na maumivu makubwa na hiyo ndiyo asili ya kupata fedha siyo rahisi hata kidogo lazima …

Zoezi Gumu Linalowashinda Watu Wengi Siku Hizi

Mpendwa rafiki, Watu wanaweza kuzingia kila aina ya sababu lakini sijawahi kusikia mtu amesingizia katika zama hizi kuwa amekosa muda wa kushika simu yake ya mkononi. Simu amekuwa anashika nafasi za watu wengi na mahusiano mengi yanazidi kuharibika kupitia simu hizi zetu za mkononi. Watoto, mke, mume , jamaa au marafiki hawana nafasi ya kwanza …

Kama Umekosa Kitu Hiki Usithubutu Kujiajiri

Mpendwa rafiki, Huwa sina laini katika mafundisho yangu yote niliyotoa na ninayoendelea kutoa. Ninasema ukweli pale  ukweli unapostahili. Je unataka kufanikiwa? Kama jibu lako ni ndiyo je unapenda kufanya kazi? Kama hupendi kazi basi huwezi kufanikiwa huo ndiyo ukweli. Hakuna mtu yeyote aliyefanikiwa bila kufanya kazi, kazi ndiyo msingi wa maendeleo kwenye kila eneo la …

Kama Unataka Kushinda Usitumie Fumula Hii

Mpendwa rafiki, Usipojiandaa kushinda basi, unajiandaa kushindwa. Ndiyo asili iko hivyo usitegemee kushinda kama hujajiandaa kushinda, kila kitu katika maisha kinahitaji ulipie gharama yake na waswahili wanasema ukiona vya elea ujue vimeundwa. Hakuna kitu cha bure lazima ukubali kulipia gharama ili uweze kupata kile unachotaka kupata kwa wakati fulani. Ziko fumula nyingi sana katika maisha …

Hii Ndiyo Ahadi Uliyoweka?

Mpendwa rafiki, Pale mwaka mpya wa 2018 ulipoanza kila mtu alikuwa na hadithi nzuri sana ya kusimulia mwaka huu, wengi walisimulia kuwa watafanya mambo mengi na hata kuandika wengine waliandika na wakaanza kufanya siku za mwanzoni. Lakini je hiyo ndiyo ahadi uliyojiwekea na unachofanya sasa hivi? Tulijiwekea ahadi za kufanya makubwa je hicho unachofanya sasa …

Hii Ndiyo Aina Bora Ya Makubaliano Unayotakiwa Kufanya Kila Siku

Mpendwa rafiki yangu, Maisha ni makubaliano bila makubaliano hakuna maisha (bargaining). Ili tuweze kupata kitu chochote lazima kwanza tufanye kwanza makubaliano na makubaliano huwa yanatokea katika pande mbili. Lengo la makubaliano yoyote ni kila mtu kushinda na inapotokea mmoja kashindwa mwingine kashinda inakuwa siyo aina bora ya makubaliano kila mtu anatakiwa aondoke akiwa ameridhika katika …

Kitu Cha Kufanya Kama Umeshajigundua Uko Kwenye Shimo

Mpendwa rafiki, Shimo linaweza kuwa ni matatizo au changamoto fulani. Usiendelee kuvumilia kuwa na mtu mzigo katika maisha yako kama umeshamgundua ni mzigo. Kwa mfano, kama msaidizi wako  wa kazi umegundua ana tatizo fulani,labda hajui hesabu katika biashara, au anakuibia usiendelee kumvumilia hata siku moja. Unapogundua tatizo lolote litatue haraka sana, usisubiri ruhusa, tatizo moja …

Uko Hapo Ulipo Kwa Sababu Hii Hapa

Mpendwa rafiki, Kila mtu yuko hapo alipo kwa sababu fulani. Maisha yako hivyo ulivyo kwa sababu fulani,umechangia maisha yako kuwa hivyo ulivyo leo wala huhitaji kumlaumu mtu kuwa maisha yako hayajakaa sawa kwa sababu ya mtu fulani kwani hujui ya kwamba jukumu la maisha yako ni lako mwenyewe? Iko hivi rafiki, uko hapo ulipo kwa …

Usijenge Urafiki Na Mtu Huyu Kwenye Safari Ya Mafanikio

Mpendwa rafiki, Kuna kitu kinachotufanya sisi tuwe hivi tulivyo leo. Kuna watu ambao wakishapata hela ya kula hawana haja tena ya kujitoa kufauta mpaka kile walichokitafuta kiishe kwanza. Huwa kinachotumaliza mapema katika mafanikio ni kitu kidogo sana,tukishakuwa na kiti hiko tunajisahau tena kuweka juhudi kubwa kama tulivyoweka mwanzo. Unatakiwa usijenge urafiki na mtu huyo ambaye …

Ogopa Kuwa Mtu Wa Namna Hii Katika Maisha Yako

Mpendwa rafiki, Kila mmoja wetu maisha yake ni ushuhuda kwa mwingine. Tumeitwa kuwa mashuhuda lakini je maisha yetu yana ushuhuda gani kwa wenzetu? Jinsi tu unavyoishi ni ushuhuda kutoka kwa wengine, tuna mambo mengi ambayo tunayashudia katika maisha yetu yanakuwa ni mazuri na mengine ni mabaya. Kuna watu ambao maisha yao yanakuwa yameshikiliwa na watu …

Design a site like this with WordPress.com
Get started