Huu Ndiyo Mtazamo Utakaokusaidia Kufanya Vitu Kwa Ubora

Ushindi wowote ule huwa unaanzia ndani ya mtu. Jinsi akili yake alivyoiandaa na imani yake juu ya kile anachofanya. Ukiingia kwenye mchezo wowote na hisia za kushindwa na kutowezekana lazima utashindwa. Leo tunakwenda kujifunza mtazamo ambao utakusaidia kufanya vitu kwa ubora. Aliyekuwa mwandishi na mhamasishaji Zig Ziglar aliwahi kunukuliwa akisema, mtazamo chanya utakusaidia kufanya vitu …

“Sikuachi Mpaka Unibariki”

Ni kauli ya ung'ang'anizi sana ambayo ilimsaidia Yakobo kupata ushindi na kubarikiwa. Yakobo alimwambia malaika sikuachi mpaka unibariki, aling'ang'ana kuhakikisha anapata kile anachotaka na kweli malaika alivyoona Yakobo amekuwa king'ang'anizi akaamua kumuachia baraka. Hata sisi katika maisha yetu huwa hatuwi vinganganizi ndiyo maana hatupati kile tunachotaka. Wengi huishia njiani pale tu wanapokutana na changamoto, usiishie …

Maeneo Mawili Unayoyachukulia Poa Kwenye Maisha Yako

Ni nadra sana kuwaona watu wakiwa wana mlinganyo sawa katika maisha yao. Yaani kila eneo la maisha yake liko vizuri na kila eneo analipa uzito. Liko eneo moja ambalo kila binadamu aliyehai analipa uzito sana na eneo hilo ni mwili. Wengi matendo ya mwili yametukamata kuliko maelezo, miili yetu inatuendesha na ubaya zaidi wengine tunakubali …

Jinsi Ya Kuona Faida Ya Kazi

Unaweza ukaichoka kazi na kuichukia kama hutumii vizuri kile unachopata kupitia kazi hiyo. Kama huoni matunda ya kazi unayoifanya na kujivunia ni rahisi kulalamika na kuona kama vile hufanyi kazi bali unafanya mazoezi tu. Ukitaka kuona faida ya kazi, kiasi unachopata yaani kama ni kipato au mshahara hakikisha sehemu ya kipato chako unajifanyia maendeleo yako …

Jilazimishe Kufanya Hata Kama Huna Hiki

Wote tunajua umuhimu wa kazi, hakuna asiyejua umuhimu wa kazi maana kazi inatusaidia kupata kile tunachotaka. Hakuna kazi bila kazi, kazi yoyote ile lazima iwe inachosha lakini hatuwezi kukubali kukaa bila kufanya kile tulichopanga kufanya. Kuna wakati ndiyo mwili haujisiki kabisa kufanya kufanya kitu sasa wewe usiusikilize mwili, jilazimishe kufanya hata kama mwili haujisiki kufanya …

Kitu Hiki Nacho Kinahusika Katika Safari Ya Mafanikio

Huwa tunajiona wajanja kwa mafanikio ambayo tunayo na tunasahau kuwa siyo kila mafanikio makubwa ambayo tunayo huwa ni kwa sababu ya juhudi tu hapana. Kama ingekuwa katika maisha ni kuweka kazi tu na juhudi mbona wengine hawafanikiwi? Inakuwaje wengine mnakua mnafanya kitu sawa lakini wanaofanikiwa ni wachache?Chukulia mfano, wanaochimba madini ni wengi lakini siyo wote …

Haya Ndiyo Matokeo Ya Kutowaambia Watu Kile Unachofanya

Bilionea na raisi wa Marekani Donald Trump kwenye moja ya nukuu zake anasema hivi, Kama hutowaambia watu juu ya mafanikio yako basi hakuna atakayejua. Mimi leo nataka nikuambie hivi rafiki yangu, kama hutowaambia watu kile unachofanya au unachouza hakuna atakayejua unafanya nini hivyo ni wajibu wako kuwaambia watu kile unachofanya au unachouza ili upate wateja. …

Hiki Ndicho Kinawafanya Watu Wengi wasifanikiwe

Sheria ya asili inatufundisha kuwa hatuwezi kufanikiwa bila kutoa. Kumbe basi, unapotoa ndiyo unapokea na watu wengi hawaijui siri hii ya mafanikio. Toa nikupe ndiyo asili ya dunia na kama mtu huwa anataka kupokea tu huwa anabaki kama alivyo maana huwezi kupiga hatua kubwa kama wewe ni mtu wa kutaka kupokea bila kutoa. Kinachowafanya watu …

Jenga Tabia Hii Moja Itakayosaidia Kuboresha Mahusiano Yako

Kwa zama tunazoishi sasa kumekuwa na kelele nyingi sana kiasi kwamba zinaweza kukusaulisha hata mambo muhimu unayopaswa kuyafanya katika mahusiano tuliyokuwa nayo. Kwanza kila mtu yuko bize na maisha yake hivyo usipokuwa makini katika kujenga mahusiano yako unaweza kuwapoteza wengi. Leo tunakwenda kujifunza tabia moja tunayopaswa kuwa nayo ili tujenge mahusiano yetu na tabia hiyo …

Hii Siyo Kazi Yako Kujua

Katika misingi ya falsafa tunaalikwa kuishi maisha yetu vizuri kama vile leo ndiyo siku yetu ya mwisho.Tunaalikwa kuishi kikamilifu kila siku badala ya kupoteza muda kufikiri juu ya kesho itakuwaje. Wako watu ambao wanajikuta wanafikiria kesho itakuwaje hii inawafanya washindwe kuishi leo vizuri. Ukweli ni kwamba hakuna anayeijua kesho hivyo kuihofia kesho ni kupotezamuda. Wewe …

Design a site like this with WordPress.com
Get started