Hizi Ndizo Nyakati Mbili Za Kupima Rafiki Wa Kweli

Tumeshazoea kusikia kwa watu kuwa rafiki wa kweli utamjua wakati ukiwa na shida. Hilo ni kweli na wala halina ubishi. Hata waswahili wanasema, akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli. Huwa tunapatwa na changamoto mbalimbali katika maisha yetu hivyo si ajabu yule ambaye unadai ndiyo rafiki wa kweli akaja kukuangusha. Wale waliosimama na wewe wakati …

Jinsi Ya Kufilisika Kimawazo

Kama unamaliza siku bila kuingiza maarifa mapya ni dalili ya kufilisika kimawazo. Kwa zama tunazoishi watu wengi wamevurugwa na maisha. Mitandao ya kijamii inawachosha watu kwa kufuatilia habari mbalimbali ambazo hata haziwasaidii kwenye maisha yao. Jitahidi angalau kila mwezi usome kitabu kinachoendana na eneo moja la maisha yako.Kile unachotaka kikue hakiwezi kukua kama wewe mwenyewe …

Rasilimali Mbili Muhimu Za Kuziheshimu

Kiufupi, hakuna mtu anayeweza kujitosheleza kwa kila kitu. Kila binadamu ana mtegemea mwingine ili maisha yaweze kwenda. Ni asili ya binadamu kutegemeana. Kujitegemea siyo kitu kibaya. Ni kizuri sana lakini huwezi kujitegemea kwa kila kitu, kuna eneo lazima utakua unahitaji msaada na huwezi kujitegemea kwa kila kitu. Kumbe basi, hakuna aliyeweza kusimama bila kutegemea wengine. …

Hiki Ndiyo Kitu Kinachowaumiza Watu Wengi

Hivi kati ya ujinga na ukweli kipi kinawaumiza watu wengi? Watu wengi huwa wanaumia kwa kuambiwa ukweli. Leo hii nakwenda kubadilisha mtazamo uliokuwa nao kwamba ukweli huwa haumuizi bali unamsaidia mtu. Aliyekuwa mtawala wa Roma, Marcus Aurelius aliwahi kunukuliwa akisema, " kama kuna mtu anaweza kunishawishi na kunionesha kwamba nimekosea, nitafurahi na kuwa tayari kubadilika.Ukweli …

Kuwa Makini Na Kile Kilichokupandisha Juu

Rafiki yangu,Ulishawahi kujiuliza nini kitakachokuja kukushusha chini? Kilichokupandisha juu ndicho kitakachokuangusha chini. Hivyo kuwa makini sana na kile kilichokupandisha juu maana ndicho kitakachokuja kukuangusha chini. Angalia kwenye ndoa yako nini kilichofanya ndoa yako iwe juu? Basi kitakachokuja kukuangusha chini ni kile kilichokupandisha juu. Kilichokupandisha juu kwenye biashara yako ndicho kitakachokuja kukuangusha chini. Kuwa makini sana …

Hiki Ndiyo Kitu Pekee Kilichokufanya Ukubali Kushindwa Kwenye Kile Unachofanya

Kwanza nianze kukuambia kitu kimoja rafiki yangu, maumivu yamekuwa ni kikwazo kwa watu wengi kuweza kufikia mafanikio kwenye maisha yao. Wakati mwingine unajiuliza kwanini watu wengine wanafanikiwa licha ya kupitia maumivu makali? Nini kinachowafanya wavumilie maumivu wanayokutana nayo pale wanapotafuta kile wanachotaka? Chukulia mfano, wewe mwenyewe umewahi kufanya vitu vingapi ukashindwa au ukakata tamaa? Ni …

Jicheleweshe Kidogo Eneo Hili

Unatoka nyumbani vizuri huku ukiwa huna hata mpango wa kununua kitu. Lakini mara unakutana na mtu anayeuza viatu na viatu ni vizuri kweli yule muuzaji anakushawishi ununue na ulikuwa huna mpango huo. Unajikuta unaiingiwa na tamaa na kujiambia viatu ni vizuri nisipovichukua sitokuja kuvipata tena. Sasa pale unapojikuta umekipenda kitu na huna mpango wa kukinunua …

Je Una Picha Ya Kile Unachotaka

Unatakiwa kuwa na picha ndani ya akili yako ya vile unavyotaka kuwa. Kwa mfano, kama unataka gari la ndoto yako basi hakikisha unakuwa na picha ya gari hilo ndani ya chumba chako. Kama unataka kujenga nyumba, kuwa na ramani ya nyumba hiyo ibandike hata chumbani kwako uwe unaingalia kila siku na kujinenea mazuri. Hakuna kitu …

Huyu Ndiye Anayepanga Bei Ya Vitu Sokoni

Hivi ulishawahi kujiuliza ni nani anayepanga bei ya maembe sokoni? Kuna kipindi unakuta bei ya kitu fulani iko juu sana, wakati mwingine unaikuta chini je ni nani anayefanya kazi hii ya kushusha na kupandisha bei? Mtu anayehusika kupanda bei ya vitu sokoni ni soko lenyewe na si kitu kingine.Soko huwa linaamua vile linavyotaka na wala …

Kamwe Huwezi Kuwa Masikini Kama Ukiishi Hivi

Kama ukiyaendesha maisha yako kulingana na asili kamwe huwezi kuwa masikini. Kama ukiyaendesha maisha yako kulingana na maoni ya watu kamwe huwezi kuwa tajiri. Aliwahi kusema mwanafalsafa Epicurus Asili huwa haina mambo mengi,inataka mambo machache ambayo yako ndani ya uwezo wa kila mmoja wetu. Asili huwa haijali uko katika hali gani. Kwanini mtu akiishi kulingana …

Design a site like this with WordPress.com
Get started