Silaha Unayopaswa Kutembea Nayo Kwenye Zama Hizi

Ni umakini wako. Mtu ambaye hana umakini ni rahisi kudanganywa na hata kutapeliwa. Kwa chochote kile unachofanya kwa sasa weka umakini wako wote kwenye kitu hicho. Watu wanakosa umakini ndiyo maana wanapata matokeo ya ajabu. Mtu anaenda kwenye nyumba ya ibada lakini hana umakini kwenye sala na matokeo yake anatoka akiwa mtupu. Ukiweka umakini wako …

Unaweza Ukaanza Vibaya Lakini Ukamaliza Vizuri Sana

Iko mifano ya watu ambao historia yao imeanza vibaya lakini wakaja wakazimaliza vizuri. Kweli njia za Mungu siyo za kwetu. Unaweza ukaanza vibaya lakini Ukamaliza vizuri sana. Kwa mfano, sauli ambaye ndiyo Paulo alianza vibaya lakini alimaliza vizuri kwa kusema vita nimevipiga vizuri, mwendo nimeumaliza na imani nimeilinda. Wangapi wanazaliwa katika familia masikini lakini baada …

Kuwa Makini Na Vitu Hivi Asubuhi Kabla Hujaianza Siku Yako

Maelfu ya watu wamekimbia makazi yao na watu 20 wameuawa na huko afaghanistan. Hali ni mbaya sana huko watu wanakufa, wanateseka na kuumia kweli na wengine wametekwa na kundi la Taliban. Hebu pata picha unaianza siku tu na kufungulia radio unakutana na habari kama hiyo unafikiri utakua na mwanzo mzuri wa siku yako? Akili yako …

Hizi Ndizo Mali Unazopaswa Kuzijenga Ili Kuwa Na Maisha Bora

Huwa tunapoteza muda mwingi kwenye mambo ambayo hata hayatusaidii kulipa bili. Kila mtu anapaswa kutumia muda wake kujenga ujenzi wa mali ili kuwa na maisha bora. Badala ya kuhangaika na vitu ambavyo havikusaidii kujenga mali unapaswa kutumia muda na nguvu zako kwenye kujenga mali zitakazokusaidia kuwa na maisha bora. Kama unawekeza kwenye biashara au kazi …

Huwezi Kwenda Mbele Huku Ukiwa Umeangalia Nyuma

Usijutie kwa yale ambayo tayari umeyafanya kwa sababu utakua uliondoka na vitu viwili kushinda au kujifunza. Kwenye maisha hakuna kushindwa bali kuna kujifunza. Watu wanataka kwenda mbele lakini mambo yaliyopita bado yanawavuta nyuma. Yaliyopita huwezi kuyabadilisha na yajayo hayawezi kutabirika. Unachotakiwa ni wewe kufokasi katika wakati ulioko na kusahau yaliyopita. Huwezi kwenda mbele wakati umeangalia …

Huu Ndiyo Mchepuko Unaopaswa Kuwa Nao

Kiasili kila binadamu anapenda vitu vizuri lakini pia vitu vizuri vinahitaji gharama kubwa. Siyo kwamba watu hawapendi vitu vizuri, tatizo ni kwamba hawana fedha za kupata kitu kizuri. Watu wameendelea kupokea kile wanachopokea kila siku bila kuwa watu wa kubadilika. Kama vitu vinapanda bei na maisha yanabadilika kwa nini na wewe usipande sasa? Hakuna hatari …

Design a site like this with WordPress.com
Get started