Sifa Pekee Inayokutoa Katika Kundi La Wanamafanikio

Mpendwa rafiki, Kuna sifa nyingi ili uwe mwanamafanikio lakini kuna sifa moja inayokutoa njeya kundi kabisa. Mtu yeyote atakayeniuliza leo kama anataka kufanikiwa afanye nini basi mimi nitamjibu mara moja bila kusita abadilishe kwanza mtazamo wake. Hakuna kitu kigumu kama mitazamo ya watu waliyoaminishwa tangu kizazi hadi kizazi. Mitazamo hiyo inaendelea kuwa kama minyororo kwa …

Jinsi Ya Kufanikiwa Kwenye Kila Eneo La Maisha Yako

Mpendwa rafiki, Hakuna mtu ambaye hapendi kufanikiwa katika eneo fulani la maisha yake, natumaini unapenda ndiyo maana kila siku unajifunza. Kufanikiwa kwenye kila eneo la maisha inahitaji uweke kazi kama unavyoweka kazi katika maeneo mengine ya maisha yako la sivyo ni ngumu kufanikiwa. Kila kitu kinahitaji kazi na hakuna eneo ambalo ni rahisi kama unavyofikiria. …

Ndoto Ambazo Hazina Hamasa Duniani

Mpendwa rafiki, Kufanya kitu ambacho hakina hamasa ni sawa na kutaka kuhamisha maji ya baharini. Hivi unakula chakula ambacho hakina chumvi? Unapata ladha gani? unakunywa chai ambayo haina ladha unapata ladha gani? kitu chochote ambacho hakina ladha iwe ni kazi au chakula kinakuwa hakina ladha ya kuendelea kufanya hicho kitu. Rafiki, kuna ndoto ambazo hata …

Kitu Pekee Ambacho Dunia Haiwezi Kushindana Nacho (Makala Ya Tarehe 26/7/2018

Mpendwa rafiki, Unaweza kushindana na vitu vyote lakini kuna kitu ambacho wewe binafsi na hata dunia kwa ujumla haiwezi kushindana nacho. Kitu ambacho kimeweza kudumu tangu enzi na enzi, utajaribu kuficha kitu hiko lakini kamwe hakifichiki. Ushindani bora dhidi yako wewe mwenyewe ni kuwa bora, hutakiwi kushindana na mtu bali shindana na malengo yako uliyojiwekea. …

Sababu Kuu Moja Inayoonesha Huyapendi Maisha Yako

Mpendwa rafiki yangu, Kila mtu ana maisha yake, kila mtu amekuja kukamilisha ripoti yake hapa duniani. Natumaini unaendelea kukusanya ripoti za kwenda kuwasilisha mbinguni na za duniani. Kumbuka hakuna mtu anayependa ripoti za hivyo hata kama mtu ni wa hovyo huwa naye hapendi vya hovyo. Kuna mtu nilikutana akaniambia anatamani ndiyo angekuwa fulani, nilimuonea huruma …

Sehemu Pekee Ambayo Haina Changamoto Duniani

Mpendwa rafiki, Maisha yenyewe ni changamoto tayari halafu nawashangaa watu wanaogopa changamoto za maisha. Kuwa hai pia ni hatari kwa sababu kama ni changamoto zitaendelea kuja kwako kama kawaida. Kutoka kwako tu nyumbani na kwenda kazini unaweza kukutana na changamoto nyingi njiani, ukiangalia katika mtazamo chanya changamoto huwa zinatuimarisha na kutuoa sehemu moja kwenda nyingine. …

Kama Unataka Kuwa Mfanyabiashara Mkubwa Usikwepe Kitu Hiki

Mpendwa rafiki, Maisha ni biashara, kila kitu ni biashara hivyo basi mfumo wa maisha yetu unaendeshwa kibiashara.  Huenda na wewe unataka kuwa mfanyabiashara mkubwa hivyo ili uwe mfanyabiashara mkubwa kuna ngazi ambayo hutakiwi kuikwepa hata siku moja. Kila mtu anayetaka kuwa mfanyabiashara lazima apitie kwenye ngazi hiyo ili awe kufanikiwa. Tukisema tunakwepa hatuwezi kufika na …

Hii Ndiyo Njia Bora Kabisa Ya Kufundisha Watu Chochote Kile

Mpendwa rafiki, Fanya kile ninachosema na siyo ninachofanya ni kauli ambayo imepitwa na wakati katika zama zetu. Siyo njia nzuri kabisa ya kufundisha bali kupotosha, watu wafanye kile unachosema halafu na wewe uishi vile utakavyo. Tunaambiwa kuwa imani bila matendo imekufa sasa usitegemee kuwa hata uwe na imani kubwa kubwa kiasi gani kama huna matendo …

Tafakari Ya Maisha Na Mambo Ishirini Na Tisa (29) Niliyojifunza Katika Miaka Yangu Ya Kuishi Hapa Duniani

Mpendwa rafiki, Tarehe 18 julai mwaka 2018 ilikuwa siku yangu ya kuzaliwa hivyo, nilitimiza miaka 29 na sikuweza kukushirikisha kitu ila nilikuahidi nitakushirikisha hivyo basi,leo nilitenga muda na kutafakari maisha yangu wapi nimetoka na wapi ninakwenda. Mwaka jana niliweza kukushirikisha mambo 28 na leo ninakwenda kushirikisha tena mambo 29 niliyojifunza kupitia maisha yangu hapa duniani. …

Kitu Kinachoua Ndoa Nyingi Siku Hizi

Mpendwa rafiki yangu, Natumaini unajua kuhusu biashara hata kama hufanyi, huenda wewe siyo mfanyabiashara lakini kwa asili wewe ni mfanyabishara kwani unafanya mambo mengi sana katika mbadilishano wa thamani. Katika biashara yoyote lazima kuwepo na mtoa huduma na mteja. Vivyo hivyo katika maisha ya ndoa, ndoa nayo ni biashara ikikosa mteja sahihi lazima itakufa kwa …

Design a site like this with WordPress.com
Get started