Jinsi Ya Kumbadilisha Mwenza Wako au Mtu Yeyote Yule

Mpendwa rafiki yangu, Mtu mmoja alisema hakuna kazi ngumu kama kuongoza watu, ni bora kuongoza kondoo wataweza kwenda njia moja lakini siyo watu. Kuongoza watu ni kama vile kuswaga paka kila mmoja atakimbilia njia yake anayetaka yeye lakini ukiswaga kondoo wote wataenda njia moja. Hapa unaweza kuona kuwa ni ngumu sana kuwabadilisha watu vile unavyotaka …

Hili Ndilo Hitaji La Kwanza La Mteja Wako

Mpendwa rafiki yangu, Kama tunavyojua biashara ni wateja kama biashara haina mteja ni kazi bure. Wateja ndiyo watu wanaofanya biashara yako ikue. Ndiyo wanalipa bili nyingi na hata kukulipa wewe hivyo ni watu wa kuheshimiwa sana. Kama ukiajiriwa mwajiri ndiyo bosi wako na umejiajiri basi mteja ndiyo bosi wako unatakiwa kumsikiliza na kumpatia huduma bora …

Hiki Ndiyo Kipindi Cha Kufurahia Sana Katika Safari Ya Mafanikio

Mpendwa rafiki yangu, Najua kila mmoja wetu anaposikia mafanikio huwa anafuraha kusikia na hakuna hata mmoja wetu anayeweza kunyoosha kidole chake na kusema kuwa yeye hahitaji maisha mazuri. Asili ya binadamu ni kupenda raha ndiyo maana wengi ni wavivu, uvivu ni mwamvuli wa kupenda raha, kukataa kuutesa mwili kwa sababu ya kuendelea kupata raha fulani. …

Jinsi Ya Kutokubali Kujiingiza Katika Mikopo

Watu wengi wanadaiwa tena madeni mbalimbali tu. Leo hii watu wanadaiwa hata na mitandao ya simu kama vile voda, tigo nk katika simu zao. Kupitia tu mikopo ya kukopa salio kupitia mitandao ya simu ninaona ni jinsi gani watu wanavyopata shida na mikopo hiyo. Hakuna mkopo ambao haukupi fedhea, asili ya mikopo ni adhabu na …

Jinsi Ya Kunogesha Mahusiano Yako

Mpendwa rafiki yangu, Kila mmoja wetu amezaliwa katika mahusiano. Hakuna mtu ambaye anasoma hapa hayuko katika mahusiano. Tuna mahusiano ya kifamilia, kindugu, kirafiki nk. Mahusiano mazuri yananjengwa katika uaminifu. Sijui ni nani atakuwa mjinga kwenda kujenga mahusiano na mtu ambaye siyo mwaminifu. Lakini pia uaminifu unajengwa mahali ambako pana uhakika. Tunajenga uaminifu mahali ambako tuna …

Kitu Pekee Ambacho Huwezi Kukibadilisha Katika Maisha Yako

Mpendwa rafiki yangu, Tunapaswa kuielewa asili vizuri sana kwa sababu asili ndiyo maisha ya kila mwanadamu yapo. Tunaalikwa kuelewa kuwa katika maisha ya binadamu kuna mambo mawili, Moja, yale ambayo yako ndani ya uwezo wetu na yale ambayo yako nje ya uwezo wetu. Jambo lolote linalotokea katika maisha yako unatakiwa kukaa chini na kujiuliza, je …

Epuka Kitu Hiki Katika Masuala Ya Fedha

Mpendwa rafiki yangu, Fedha ni muhimu katika maisha yetu hilo halina ubishi. Tunatumia fedha kuishi maisha tunayotaka hapa duniani na fedha hufanya maisha yetu kuwa bora. Katika mchezo wa fedha eneo la nidhamu limewashinda wengi, unapozungumzia mchezo wa fedha unatakiwa uwe na roho ya nidhmu na siyo vinginevyo. Kuna mambo mengi ambayo tunayafanya katika mchezo …

Hii Ndiyo Faraja Kubwa Wanayopata Wazazi Kutoka Kwa Watoto Wao

Mpendwa rafiki, Mzazi huwa anafarijika pale anapomwona mtoto wake anapofanya mambo mazuri, anajihisi mwenye amani na hata mtoto anapokuwa amelelewa vizuri, malezi mazuri yale malezi mazuri yanakwenda kuwa Baraka siyo tu kwa wazazi hata kwa watu wengine. Watu wanakuwa wanavutiwa na watoto wenye adabu njema na utii kwa wakubwa wao, hivyo anapofanya mazuri katika ngazi …

Jinsi Ya Kumfahamu Mtu Mwenye Hekima Na Mjinga

Mpendwa rafiki yangu, Tunaishi na watu na hivyo tunatakiwa kuwafahamu watu vizuri. Kujua mema ni kutenda mema kama wanafalsafa wavyosema. Tunapowafahamu  watu tutajua jinsi ya kuishi na watu vizuri. Kama ulishawahi kusikia kuwa, kuna mtu mmoja katika hadithi ya vitabu vya dini ambaye alikuwa  ni tajiri na mtu mwenye hekima sana na huyo alikuwa siyo …

Kitu Ambacho Hakitokusaidia Kubadilisha Maisha Yako

Mpendwa rafiki yangu, Tuna muda mfupi sana hapana duniani wa kufanya yale muhimu lakini siyo kufanya kila kitu kinachojitokeza katika maisha yako. unapoianza siku yako unatakiwa kuwa na ratiba ya ushindi ambayo umeandika mambo unayopaswa kuyafanya ndani ya siku husika. Hivyo, yakijitokeza mambo ambayo hayapo katika ratiba yako wala hata usihangaike nayo ni usumbufu tu …

Design a site like this with WordPress.com
Get started