Mafanikio Yoyote Yale Kamwe Hayaji Kwa Njia Hii

Kwa asili tu hakuna kitu kinachotokea kwa njia rahisi, asili huwa haifanyi kazi kwa njia za miujiza ya haraka hata siku moja. Kwa mfano, ulishawahi kuona mwembe umepandwa leo na leo uzae? Vipi sisi binadamu tunafanya kazi leo na tunataka mafanikio ya haraka? Asili ndiyo inaleta mafanikio ya kweli na ya uhakika. Hakuna mafanikio yanayokuja …

Usiweke Mayai Yote Kwenye Kapu Moja

Ni usemi maarufu sana katika uwekezaji.Ukiwa na maana kwamba usiwekeze katika eneo moja. Unatakiwa kutawanya uwekezaji wako katika maeneo tofauti tofauti. Inapotokea hatari ya uwekezaji, labda umewekeza kwenye eneo moja utapata hasara sana lakini kama utakua umewekeza maeneo tofauti haiwezi kukuletea shida, haiwezekani maeneo au sekta zote ulizowekeza zikaanguka zote kwa mara moja. Kama uwekezaji …

Jifunze Kujichelewesha Kuchukua Hatua Ukiwa Na Hali Hii

Pale unapojihisi uko kwenye hisia yoyote ile, jicheleweshe kuchukua hatua hapo kwa hapo.Kwa mfano, mtu akikutukana, au akikuambia maneno mabaya kwako, usichukue hatua ya kutaka kumjibu badala yake jicheleweshe ili hasira ziishe kwanza. Jifunze Kujichelewesha, unapojichelewesha unakuwa unazipunguza hasira. Siyo tu kupunguza hasira lakini pia unajifunza kutawala hisia zako. Hatuwezi kuzuia hisia katika maisha yetu, …

Usimchukie Mtu, Bali Chukia Hiki

Katika maisha tunaalikwa tupendane, na pale inapotokea mtu amefanya ndivyo sivyo basi tueleweshane kwa upendo. Kila binadamu ana udhaifu wake, hivyo ukisema umchukie kila mtu kadiri ya udhaifu wake utabaki peke yako duniani na kila mtu utamwona ni mbaya. Chukia dhambi na wala usimchukie mtu. Mtu ataweza kuja kubadilika sasa kama umemchukia maana yake itakuja …

Jinsi Ya Kuwa Mtumwa Wa Sasa

Kati ya viumbe waliopendelewa sana na Mungu basi ni binadamu. Tumepewa akili ambayo inatutofautisha na wengine wote. Ila sasa, changamoto yetu wengi hatutumii uwezo huu mkubwa ulioko ndani yetu. Hebu pata picha hapa, tumeshindwa kuwa kama samaki lakini tukatengeneza vifaa vinavyoelea majini kwa kutumia akili. Tumeshindwa kuruka kama ndege lakini tumetumia akili kutengeneza ndege inayoruka …

Kama Mahusiano Yako Yamekosa Hiki…

Asili ya kila binadamu ametokea katika mahusiano, kila mmoja wetu mpaka tunazaliwa ni wazi tunatokea katika mahusiano ya kama vile kutoka kwa wazazi, ndugu, nk. Mahusiano mengi siku hizi yamekuwa na changamoto kwa sababu ya kutokuishi misingi ya mahusiano. Mahusiano yetu mengi yanajengwa na uaminifu, na sasa kama uaminifu haupo ndani ya mtu maana yake …

Kile Unachohofia Mara Nyingi Kinakuwa Hivi

Mara nyingi kile tunachohofia hata huwa hakitokei. Ni sisi tu binadamu tunapenda kutengeneza mazingira ya hofu ambazo hata kiuhalisia hazipo. Hofu huwa tunaanza kuitengeneza akilini. Tukishaijaza hofu akili na mwili unapokea matokeo yake tunashindwa kuthubutu na kufanya kile tulichochagua kufanya. Dawa ya hofu ni wewe kuingia mzima mzima. Bila kujali nini kitatokea, na hata unachohofia …

Huyu Ndiye Mtu Pekee Ambaye Anaweza Kukuambia Huwezi

Yuko mtu ambaye ana nguvu kubwa sana katika maisha yako ambaye ni wewe mwenyewe.Unajua kiasili hakuna mtu ambaye ana mdharau mtu au kumtukana mtu ila yale maoni au tafsiri tunazojipa kupitia jambo tuliloambiwa ndiyo linaleta mambo kuwa mabaya.Kumbe basi, tafsiri zetu ndiyo machaguo yetu. Watu wa nje wanaweza kukuambia vile wanavyoweza lakini wa kutoa ruhusa …

Jiandae Kwa Fedha Hii Muhimu

Fedh ni muhimu sana katika maisha yetu na hilo halina ubishi. Fedha inatusaidia kulipia bili mbalimbali kwenye maisha yetu. Kwa lugha rahisi fedha ni mfalme. Anayekuambia fedha siyo muhimu huyo ni mnafiki na huenda hata yeye anafikiria hela ya kula ataitoa wapi ndiyo maana anakujibu hivyo. Dunia ina fedha nyingi sana na baadhi ya fedha …

Wewe Hauko Huru Mpaka Uwe Na Uwezo Huu

Changamoto moja ya watu wengi ni kushindwa kujitawala. Watu wengi wanaendeshwa na hisia sana na karibu maamuzi mengi watu wanayofanya wanayaamua kwa kutumia hisia halafu wanakuja kuhalalisha kile unachoongea kwa kufikiri. Watu wanaendeshwa na tamaa nyingi, tamaa ya mapenzi, tamaa ya kufanya anasa na nk. Ni kundi chache sana la watu ambao wanaweza kujitawala. Wewe …

Design a site like this with WordPress.com
Get started